UA
WAA WA
ka wA pi Ui
.. ia
KA Aa
UA
- ,, KA
YA yana Ww s
Ka
Ja
NO YAWA
- W IA
ai y- kA
" KRII
TE
ELISI KATIKA
NCHI YA AJABU
LEWIS CARROLL
IMETAFSIRIWA NA
ST Lo DE MALET
(ALICE IN WONDERLAND: SWAHILI)
LONDON
THE SHELDON PRESS
HOLY TRINITY CHURCH, MARYLEBONE ROAD, N.W.I.
1967
First published, 1940
MADE IN GREAT BRITAIN
YALIYOMO
SURA UKURASA
IJI. Pango LA SUNGURA - - - Sa
II. KIidIimbwi CHA Machozi - - Sa
III. Shindano La Kaka - - - - 28
IV. NYUMBA YA SUNGURA - - 3
V. MAsHAURI YA MDUDU - - -. 4
VI. NGURUWE NA PILIPILI - 55
VII. Karamu YA WENYE WAzIimu - - 66
VIII. MachHeEzo YA MALIA - - - aa
IK. Hadithi YA Kasa - - - Aa.
K. Ngoma YA Kamba - - - - AA
KI. Mwizi wA Maandazi - - - - 201
ZII. Ushahidi WA Emsi - - - - 108
ya -
kai
OMOYLIAY
WAR KIA, kaa AA
. 2 amua ka sa T
, masia ano wami
20007 maana aa amamdi VI
; uiudii ay umeamza Mi .V
- anuai aya aweanda JI.
Swai IA waasadi TIC
; " WAZA, AY usasa aa
ki wa wiaarisi BRITAIK
WAA ke 7
n ; H y hi 5 . La
| Y aa ya
ZAMANI sana Mzungu mmoja
Aliyependwa na watoto,
Aliwahadithia kwa umoja
Habari tamu sana za ndoto.
Na mimi basi ninapenda
Watoto Waafrika pia,
Nimefikiri watapenda sana
Kwa lugha yao nzuri kusikia
Habari za mtoto yule
Katika Nchi ya Ajabu.
Tafsiri yake naam ni kazi kubwa
Furaha yao kwangu ni thawabu.
Njoni watoto na kaeni,
Tutafurahi sana sisi !
Sikilizeni nitakaposoma
Maneno na matendo ya Elisi.
Ingawa mimi ni Mzungu
Mniridhie; si mgeni,
Mna bahati nami bila shaka.
Sikilizeni sana, nyamazeni.
E. V. St. L. C.-D.
IK
ajoma nyarsM BIGI IAA
nioe za pwbasgovitA -
siomu zwi sidiibadawilA
moba 83 BABE urani hatali
KA wai ai
Ai adhisswW zai Wa
Kia shaogataw
situ kasa AA adgal swal r ;
NTA vs0am as hadhi wa
WANA BI UTE MAE
#wdud kisi JA wasa EA mida
kaa ha kamaa ani enu wa
Aa ohasisor na asia? SW
ayaseM ia atm swaga!
Jasgm ia zsidhbhioM
'nakada sii kasa waa, ujana
aa Aa
3
Miji
; HATI KUHUL,
y Na aili (
/ Si wali KU,
/
SURA 1
PANGO LA SUNGURA
Hapo kale palikuwa na mtoto mwanamke, jina
lake Elisi. Wakati wa mwanzo wa hadithi hii
Elisi alikuwa amekaa pamoja na dada yake
katika kivuli cha mwembe; mara kwa mara
alikuwa akitazama kitabu alichokuwa akisoma
dada yake, lakini kilikuwa kitabu kisicho picha;
Elisi akasema moyoni mwake, “Kitabu bila
sanamu hakina faida ” akapiga mwayo akanena
“Nataka niondoke nikachume maua, lakini
nimechoka kabisa "!
Hapo yule Elisi alishtuka kumwona sungura
mweupe mwenye macho mekundu aliyekuwa
11
12 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
akikimbia; Elisi hakustaajabu hata alipomsikia
yule sungura akisema, “ Ole wangu, ole wangu !
Nitachelewa kabisa.”
(Halafu alikumbuka ya kwamba sungura
hawasemi, lakini wakati wa hadithi hii haku-
shangaa.)
Sungura alitoa saa mfukoni mwake; mara
Elisi akaondoka akasema “Lo! sungura ana
kanzu na mfuko na saa! Naam hii ni ajabu
kubwa!” Akapiga mbio, akamfuata shambani,
na kwa bahati hakumpotea bali alimwona
akiingia pangoni mwake.
Elisi hakukaa kufikiri bali akaendelea ku-
mfuata sungura. Pango liliendelea moja kwa
moja kwa mwendo wa dakika kumi, kisha njia
ikatelemka kwa ghafula kama inayoingia kisi-
mani, na kwa sababu ya giza lililokuwako Elisi
hakuliona lile shimo, akatumbukia; lakini haku-
lia wala hakuogopa kwa kuwa hakuanguka
kama jiwe, lakini alitelemka kama kwamba
alikuwa akiruka hewani, alikuwa akianguka
pole pole.
Kwanza Elisi alijaribu kutazama chini, lakini
hakuona kitu ila giza tupu, kisha akatazama
kuta za kisima, na kumbe zilikuwa na makabati
mengi na vibao vya kuwekea vitabu; huko na
huko zimetundikwa ramani na sanamu. Katika
kibao kimoja akaona chupa nyingi sana, aka-
twaa moja akasoma katika cheti chake “ Ma-
tunda ya Machungwa.” Halafu aliogopa kuia-
PANGO LA SUNGURA 13
ngusha akasema “Labda pana watu chini,
nitawadhuru nikiiangusha chupa hii.” Lakini
alijitahidi akairudisha katika kibao kingine.
Elisi aliwaza, akasema moyoni ““ Basi, baada
ya kuanguka namna hii sitaogopa tena kua-
nguka, hata nikitoka juu ya dari ya nyumba,
sitalia hata kidogo, jamaa zangu watafurahi
na kufikiri kuwa mimi ni mtoto hodari sana !”
Akatelemka! Akatelemka! Akatelemka !
Akasema “ Bila shaka nimetelemka maili nyi-
ngi sana, labda chini ya kisima hiki ni kati kati
kabisa ya dunia! Au labda hakuna mwisho,
na kisima hiki kitatokea upande wa pili wa
dunia; je, watu wa upande huo wanafanana na
nini? Nikifika huko nitawasujudia, nitawa-
uliza habari za nchi yao.” Elisi akakumbuka
ya kwamba Mwalimu wa chuoni alipata kufu-
ndisha ya kuwa nchi ya Amerika iko upande
wa pili wa dunia, akasema ““ Labda nakwenda
Amerika !”
Akashuka! Akashuka! Akashuka! Elisi
akaanza tena kujizungumza akasema “ Dina
atanililia leo jioni!” ( Dina” ni jina la paka
wa Elisi.) “Ewe Dina laiti ungekuwa nami
kwa wakati huu! Lakini hewani hakuna pa.-
nya! Labda ungependa kukamata popo kama
ungekuwa hapa! Je, paka hula popo? Si-
jui.” Macho yake Elisi yalikuwa mazito kwa
usingizi, akaweweseka akawa kila mara ana-
sema “Paka hula popo”? “Paka hula po
14 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
po” na mara kwa mara “Popo hula paka”?
“Haidhuru nikisema paka hula popo au niki-
sema popo hula paka, mamoja kwangu, maana
mimi sijui kuyajibu maswali haya.”
Elisi akajiona amelala usingizi, akaota ya
kwamba alikuwa akitembea pamoja na Dina,
akamshika mkono akamwuliza sana akisema
“Sasa Dina niambie kweli, unapenda kula
popo ?”
Kwa ghafula Elisi akajiona ameamka tena,
naye amefika mwisho wa kisima; pana majani
mengi sana makavu; na hapa kukawa mwisho
wa kuanguka kwake. Elisi hakuumiwa hata
kidogo, akaondoka mara moja akainua macho
yake, lakini juu hakuona ila giza tu, na mbele
yake pango liliendelea; na tahamaki akamwona
yule sungura mweupe akitangulia kwa haraka.
Elisi akajipa moyo, akapiga mbio sana apate
kumkaribia, lakini alipokuwa karibu kabisa
sungura akazunguka pembe ya njia, Elisi asi-
mwone tena, bali alimsikia mbali kidogo aki-
sema ““ Ole wa masikio yangu na mkia wangu !
nitakuwa nimechelewa sana ” Elisi akazunguka
pembe lakini sungura akawa ametoweka kabisa.
Sasa yule mtoto akajiona yumo katika chu-
mba kikubwa, chembamba, chenye dari fupi;
kiliangazwa na taa zilizotundikwa darini, na
katika kuta za chumba ilikuwamo milango
mingi sana. Elisi akajaribu kufungua kila
mlango, lakini yote ilikuwa imefungwa.
PANGO LA SUNGURA 15
Kati kati ya chumba akaona meza ndogo ya
kioo yenye miguu mitatu, na juu yake upo
ufunguo wa dhahabu mdogo sana. Elisi aka-
furahi akasema “Sasa naweza kufungua mi-
lango,” akajaribu sana asiweze, ufunguo mdo-
go na tundu kubwa, akakata tamaa. Mwisho
akaona mlango mdogo kabisa ambao hajapata
kuuona, akainama akatia ufunguo katika tundu,
na tazama ukafaa! UElisi akafungua ule mla-
ngo mdogo, akapiga magoti akachungulia nda-
ni. Kulikuwa na pango kama la panya, na
mwisho wa pango kulikuwa bustani nzuri ka-
bisa, akatamani sana kutoka chumbani mle
alimokuwamo kwenye giza, ili afike kwenye
jua na maua na chemchemi bustanini; lakini
hakuweza hata kupitisha kichwa pangoni, aka-
16 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
sema “Kama ningeweza kujipunguza kuwa
nyembamba mfano wa bomba ya baisikeli
ningeweza kuingia bustanini.” (Wafahamu
Msomaji, ya kuwa jinsi mambo mengi ya ajabu
yalivyomtokea hata Elisi alidhani kwamba
kwake yeye kila neno liliweza kutokea.)
Elisi akarudi mezani, na sasa akaona chupa
ndogo juu yake, na shingoni limefungwa kara.-
tasi kwa uzi, na juu ya karatasi imeandikwa
“Uninywe.” Elisi alikuwa mtoto mwenye
akili, akasema, “Labda ni sumu” kwanza
nitafute neno “ “sumu” ”; akatafuta sana lakini
hakuliona, akafungua chupa akaionja kidogo
dawa iliyokuwamo ndani yake; ladha yake
tamu kama embe au nanasi au asali, akainywa
upesi.
Mara Elisi alipokwisha kunywa dawa aka-
jiona kuwa amepungua kimo, akafumba macho
akaogopa kidogo, akasema “ Labda nitatoweka
kabisa kama nuru ya mshumaa inapozimwa.”
Alipokwisha pungua alifumbua macho, akajita-
zama sana, urefu wake ulikuwa kama kuku;
akasema “ Nitaweza kuingia bustanini sasa
hivi” Lakini, maskini Elisi, alishindwa kabisa,
kwa kuwa amesahau ule ufunguo mdogo wa
dhahabu, aliuacha mezani; yeye sasa mdogo,
hakuweza kufika mezani, alijaribu sana ku-
panda mguu wa meza bali alishindwa kwa ute-
lezi wake, na alipochoka kwa kujitahidi alikaa
kitako akalia sana; badaye akajilaumu aka-
PANGO LA SUNGURA 17
sema “ Basi, tulia sasa, haina faida katika kulia,
nakuonya unyamaze upesi.” Elisi ilikuwa de-
sturi yake kujipa mashauri mazuri, ingawa
mara nyingi hakuyafuata. Mtoto akazidi ku-
jiambia “Faida gani kusema peke yangu”?
Mara Elisi akaona kisanduku chini ya meza,
ndani yake ulikuwamo mkate mdogo, na ka.-
tika ule mkate yameandikwa maneno wazi
wazi, kwa herufi zilizofanyizwa kwa chembe za
mtama: “UniLe.” Elisi akasema “Ni heri
niule, halafu nitaona matokeo yake yataka-
vyokuwa; labda utaniongeza urefu tena kama
bomba ya baisikeli, nipate kutwaa ufunguo, na
ukinipunguza zaidi nitaweza kutambaa chini
2
AIW—B
18 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
ya mlango kama mdudu, niingie bustanini.”
Akala kidogo ule mkate, akaweka mkono
kichwani apate kuona wakati akipanda au aki-
shuka, akashtuka kuona urefu wake ule ule,
akacheka akasema “Kweli mkate si dawa ya
kugeuza mwili, lakini hapa mahali pa ajabu,
sina haja ya kushangaa nikigeuzwa na mkate.”
Akazidi kula hata akaumaliza.
SURA II
KIDIMBWI CHA
MACHOZI
Euisi akapaza sauti Aa
akasema “Hapa 3 uu
mambo yote yana-
zidi kunishangaza,
kumbe najiongeza
urefu kama bomba
ya baisikeli kubwa
kupita zote”! Aka-
inamisha macho
akajaribu kuvita-
zama vidole vyake
vya miguu, akavi-
ona viko mbali sana,
akasema “Kwa
herini miguu, labda
hatutaonana tena,
nitawapeni zawadi
wakati wa siku-
kuu.” Akacheka akasema “Sasa nitapuuza
kila neno"!
Elisi akajipiga kichwa darini, urefu wake
ulikuwa kama wa watu wawili wakubwa, aka-
19
ya
20 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
twaa ule ufunguo mdogo wa dhahabu, akaenda
upesi kwenye mlango wa bustani. Maskini
Elisi! Baada ya kujitahidi sana aliweza kuu-
karibia mlango, akalala kifudifudi akatazama
kwa jicho moja bustanini, lakini kuingia haku-
weza; akakata tamaa kabisa, akakaa kitako
akalia sana, akajilaumu tena akasema ““ Ni aibu
kabisa kulia namna hii, wewe mtoto mkubwa
sasa, nawe walia kama mtoto mchanga, tulia
mara moja” Walakini akazidi kulia akatoa
machozi mengi sana, hata yakatosha kujaza
mitungi ishirini, akawa amekaa katika kidi-
mbwi cha maji.
Badaye kidogo Elisi alisikia mashindo ya
miguu midogo njiani, mbali kidogo, akajifuta
machozi apate kumwona yu nani ajaye. Ku-
mbe ni Sungura Mweupe aliyekuwa akirudi,
amevaa nguo za umalidadi wa Kizungu, ame-
shika mkononi mwake upepeo na kofia, anapiga
mbio akinungunika na kusema “ Atakasirika
sana nikimkawilisha.” Elisi, kwa sababu ya
hali yake mbaya, na katika kukata tamaa
kwake alikuwa tayari kumwomba msaada mtu
ye yote, basi alipomkaribia Sungura alisema
kwa hofu na kwa sauti ndogo “ Shikamoo
Bwana Sungura, Tafadhali .. .” Sungura
akashtuka sana hata akaangusha vitu alivyo-
kuwa navyo, akakimbia upesi gizani.
Mle chumbani alimokuwamo €Elisi mlikuwa
na joto kidogo, kwa hiyo alitwaa upepeo wa
KIDIMBWI CHA MACHOZI 21
sungura, aliouangusha akaanza kujipepea, aka--
jizungumza tena akisema “ Ole wangu, hii ni
siku ya ajabu! Jana mambo yalikuwa sawa
Aaa
— AA aa
PI
HU!
aa ——- za
Ja ka — Zizi
(AT ANITA my j
| WUE NI zi
HABA KAA niga ha
if z : a > v ; . 5 ni
Btihi KAABA NI AA A
AA ataiti ja L
WI
ja Ki i Di 3 ! di
UPANA aha ea ! ji
i UA |
YA NA !
ii
sawa, labda niligeuzwa usiku, nadhani ya ku-
wa nimesahau yote niliyofundishwa chuoni.”
Akajaribu kusoma kwa moyo mashairi aliyo-
jifunza zamani kidogo, akanena:
22 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Kwa nguvu sana Mamba a—
naling'arisha kila gamba
Katika mto akang'aa
Yu safi sana yule Mamba.
Na Mamba alichekelea,
Akatandika kucha zake.
Samaki walipotembea
Wakahesabu meno yake.
KEY G.
MA IAA AI KATA
Kwa ngu-vu sa-na Mam-ba a-na-ling'-a-ri-sha ki-la
il mimi:s WAN AA AA AA Kaa
gam-ba Ka -ti-ka m-to a - kang'-aa Yu
AA KA KA AI AAA AA WAA
sa-fi sama yu - le Mam -ba. Na
1| AYA WAA AA AA aa AA AA KAA
Mam<-ba a-li-che-ke- le-a, A-ka-tan-di-ka ku-cha
| m:imjo:s | Le: tape: ta | mf:mrim:s, |
za-ke. Sa - ma-ki wa-—li - po-tem-be-a Wa-
| 1,8,:1,4,14:r | dr:mf|s:s | 1.8: £f.m | r.m:f.s |
ka-he-sa-.bume-no ya-—ke..., Sa - ma-ki wa-li-
(II meunzides AA AA AI
po-tem-be-a Wa - ka-he-sa-bu me-no ya-ke.
-
KIDIMBWI CHA MACHOZI 23
Kwa bahati njema wakati ule akaona ki-
chwa na mkono, akashangaa kuona ya kuwa
amevaa ile kofia ndogo ya Sungura, akasema
“Nawezaje kuivaa kofia ndogo namna hii,
ikiwa kimo changu ni kama kile cha watu wa-
wili? Labda sasa nimepungua tena.” Akao-
ndoka akaenda mezani apate kujipima penye
mguu wake; na kumbe, urefu wake ulikuwa
kama wa mtungi, tena alikuwa anazidi kupu-
ngua; akatafuta sababu ya kupungua kwake,
akaona ya kuwa ilikuwa ule upepeo wa Sungura
alioushika, akauangusha upesi asizidi kupu-
ngua, akasema “Bahati kubwa! Kama ni-
ngaliendelea kuushika ningalitoweka kabisa.”
Elisi akaogopa kidogo, lakini alifurahi ya
kuwa maisha yake hayajaisha bado, akasema
“ Vema, sasa nitakwenda bustanini.” Akapiga
mbio akafika mlangoni, lakini umefungwa ka.-
ma zamani, na ufunguo upo vile vile mezani.
A
24 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Akalia sana akasema ““ Mambo yamezidi kuwa
mabaya tena ni mara ya kwanza katika maisha
yangu kuwa mdogo.” Aliposema maneno ha-
ya miguu yake ikateleza akaanguka akatumbu-
kia katika maji ya chumvi mpaka kidevuni;
kwanza alidhani ya kuwa ameanguka baharini,
kisha akafahamu ya kwamba yale maji ya
chumvi ndiyo kile kidimbwi cha machozi yali-
yomtoka alipokuwa na urefu kama watu wawili,
akasema “Adabu ya kulia ndio kufa ndani
ya machozi !”
Kwa ghafula Elisi akasikia kitu kinaruka
majini, akaogelea karibu kidogo apate kuki-
ona, kwanza alidhani ni kiboko, kisha akaku-
mbuka udogo wake akaona ya kwamba ni
panya tu, aliyeanguka majini kama yeye mwe-
nyewe.
Elisi akasema kimoyomoyo akinena “ Labda
inafaa kusema naye, ikiwa sungura wanaweza
kusema katika nchi hii, bila shaka panya nao
wanaweza; Hebu! Nijaribu!” Akapaza sauti
akasema ““ Ewe Panya, nchi kavu iko wapi?
Nimechoka kuogelea.” Panya akamtazama
mtoto kwa makini, akakonyeza jicho, bali ha-
kujibu. Elisi akasema moyoni “ Labda hasi-
kii Kiswahili, nitasema Kiingereza.” Hakujua
ila maneno machache ya Kiingereza, akasema
kwa sauti kuu “ Where is my cat ?” (Maneno
haya ndiyo ya kwanza katika kitabu chake
cha kujifunza Kiingereza, tafsiri yake “ Yuko
KIDIMBWI CHA MACHOZI 25
wapi paka wangu ?”) Aliposikia maneno haya
panya akaruka akatoka katika maji, akitete-
meka kwa hofu; Elisi akasema “ Niwie radhi
Panya, nilisahau kabisa ya kuwa hupendi pa-
ka.” Panya akajibu kwa sauti nyembamba
akasema ““ Kweli sipendi paka; je, wewe unge-
wapenda paka kama ungekuwa kama mimi ?”
Elisi akajibu akasema ““ Ningekuwa kama we-
we labda nisingewapenda, lakini nadhani unga-
. Jimpenda paka wangu, kwani ni mpole kabisa,
jina lake Dina. Kazi yake ni kukaa kitako,
kutoa ngurumo na kujiramba, napenda sana
kumbembeleza naye ni fundi kabisa wa kuka-
mata panya. ... Niwie radhi! Nimesahau.”
Panya alikuwa akitetemeka 'sana, Elisi aka-
mwonea hurumu akasema “ Tusiendelee ku-
zungumza juu ya paka.” Panya akajibu aka-
sema ““ Wasema Sisi tusiseme habari za paka;
kwangu mimi simtaji hata jina lake, watu wa
kabila langu huchukia kabisa paka, wanyama
wabaya, hawana adabu, wakali, nisisikie
tena hata jina hilo!” Elisi akajibu akasema
“Vema, sitalitaja tena. Tuzungumze mambo
menging, je, wapenda mbwa?” Panya haku-
jibu, Elisi akaendelea kusema “ Pana mbwa
mzuri sana anayekaa penye nyumba yetu,
nitapenda kukuonyesha, ana macho makubwa
mazuri sana, rangi yake kama udongo, na
kama ukitupa mpira anaudaka, bwana. wa
mbwa 'huyo anamsifu sana, asema ni mbwa
26 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
wa kufaa sana kunaanza panya wote nyu-
mbani.”
Panya akaogelea upesi kumwacha Elisi, na
kwa hiyo naye akatambua ya kuwa amemwu-
dhi, akamwita akasema “ Ee Panya mpenzi
rudi! Natoa ahadi ya kuwa siwezi kusimulia
tena habari za paka wala mbwa.”
ukuaji
L
za
AI
i
f
'
ai.
Tai 3
AAA
AI
Aliposikia haya panya akarudi pole pole,
akasema kwa sauti ndogo ““ Twende nchi kavu
kisha nitakuhadithia habari za maisha yangu,
upate kufahamu jinsi ninavyowachukia paka
na mbwa.”
Bila shaka wakati wa kutoka kidimbwini
ulikuwa umefika, maana wanyama wengi wa-
KIDIMBWI CHA MACHOZI 27
mekusanyika majini, waliotumbukia humo ka-
ma Elisi na Panya.
Palikuwa na bata mmoja, Doda mmoja,
lauri mmoja, Tai mmoja na wanyama wengine
wa ajabu.
— Elisi akatangulia, wakaogelea wote mpaka
nchi kavu.
SURA III
SHINDANO LA KAKA
Lilikuwa kundi la ajabu sana lililokuwapo
pwani; ndege wote manyoya yao yalikuwa
yamelowa, na maji yalikuwa yanatiririka ka-
tika ngozi za wanyama; wote wamenuna kwa
hali yao mbaya; wote wakahitaji kukauka,
kila mmoja akapiga kelele kupita wenzake ka-
tika kutoa mashauri ya njia za kuweza kukau-
ka. Elisi akafanya kelele kupita wote, ha-
swa alishindana kwa maneno na yule Lauri,
mpaka mnyama huyu akakasirika kabisa aka-
kataa kusema, ila maneno yale, aliyoyasema
mara nyingi sana, ndiyo: “Mimi nimekaa du-
niani miaka mingi kupita wewe, kwa hiyo mimi
najua zaidi.” Elisi akamwuliza umri wake,
lakini akakataa kabisa kumwambia.
Panya alichoka akamwuliza Elisi akasema
“ Waendeleaje mwanangu? Umekwisha kau-
ka?” Elisi akajibu “Sijakauka hata kidogo.”
Doda akapaza sauti akasema ““ Kwa hiyo nawaa-
muru wote wafikiri shauri jingine la kufaa, kwa-
ngu mimi shauri ni kupiga “ Shindanola Kaka.”
Elisi akauliza akasema “Shindano la Kaka ni
nini?” Doda akasema “Namna ilyo bora ya
kueleza kitu ni kukitenda.”
28
SHINDANO LA KAKA 29
Kwanza Doda akapiga mstari chini kwa dua-
ra mkubwa, hii ndiyo njia ya kutembelea,
kisha wote wakasimama mstarini, huko na
huko, wakakimbia wanapopenda, kwa hiyo
ilikuwa si rahisi kujua kikomo cha shindano
hilo; walakini wote walipiga mbio kwa nusu
saa, na walipokuwa wamekwisha kukauka Do-
da akasema kwa sauti kuu “ Shindano lime-
kwisha.” Wote wakatulia wakamsogelea Doda
wakitweta, wakamwuliza wakisema ““ Tuambie
Doda, nani aliyeshinda ?” Doda akakaa aka-
fikiri saaaaaana, kidole kinywani, na wote wa-
likuwa wamengoja, mwisho Doda akapiga ke-
lele kwa furaha akasema ““ Wote wameshinda,
wote watapata tuzo.” Kwa sauti moja wa-
nyama wakauliza wakasema “ Nani atakaye-
toatuzo”? Doda akajibu “ Huyu.” Akamwe-
lekezea kidole Elisi, makutano ukamgeukia
Elisi wakasema “Tuzo! Tuzo! Twataka
tuzo.” Elisi akaogopa kidogo lakini aliku-
mbuka ya kuwa zamani kidogo alifunga senti
chache za moja moja katika pembe ya shiti
yake, akaifungua fundo upesi, akaona ya
kwamba kwa bahati alikuwa na senti za kuto-
sha kumpa kila mtu moja; akazitoa kwa uta-
ratibu, wote wakapendezwa sana. Panya aka.-
mwambia Elisi “ Wewe pia, lazima upate tuzo.”
Doda akaitikia ““ Ndio, lazima upate tuzo vile
vile; je, unazo nyingine fundoni mwa kanga ”?
Elisi akajibu “Sina, ila pete tu”! Doda aka.-
30 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
nena “Itafaa,nipe.” Elisi akampa ndege ile pete,
huyu akamrudishia kwa heshima kuu akasema
“ Pete hii iwe na kibali kwa Mama.” Na alipo-
kwisha kusema maneno haya wote wakapiga
Ni.
4 WA
Ww : AI UA
Na ndi Wa f, Yaa v
kaa AI v
“ wa WA Na .
NI pa wako v
r zi Ka
pa,
ka
AI
NG
by —
Y, AI
za . y WA
WIN I Ia Aa WA z
LIPIA >
wa AH zi
Nu
.. WA
makelele ya kushangilia. Elisi akafikiri kuwa
matendo haya hayana maana, lakini akawasa-
limu wanyama akapokea pete, akaivaa kidolini.
Elisi akamwita Panya akamwambia kwa
sauti ndogo akasema ““ Ewe Panya zamani ki-
SHINDANO LA KAKA 31
dogo uliahidi kunisimulia hadithi ya maisha
yako, na kwa nini wachukia sana wanyama
wa namna fulani (Siyataja majina yao),” Panya
akamjibu Elisi kwa huzuni akasema ““ Hadithi
yangu ndefu sana. Katika nchi yetu desturi
ni hii: Fulani akiwa na mkia mrefu, husemwa
ana bahati ya kuishi siku nyingi, tena ana ruksa
kusimulia hadithi ya maneno mengi; mkia wa
fulani ukiwa mfupi, maisha yake mafupi pia,
na hadithi yake lazima iwe na maneno macha-
che tu. Katika nchi yangu “ MKIA ' na ' HA-
DITHI ' ni neno moja, nikisema '“ Mkia wangu
mrefu ' au ' Hadithi yangu ndefu ” maana ya.-
ke sawa sawa; na mkia wangu ni mrefu
mno. “Hadithi” au “Mkia' wangu ni hii””:—
32 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
“Mama yangu
WA UA USAIOA
Mbwa wali --
kuwa rafiki.
Mbwa akamshtaki
mama yangu. A-
kasema, wewe
umeiba cha-'
AA AUA
Bwana wa-
ngu wewe mwivi
nitakushtaki kweli
serikalini --
Mwamuzi aka-
sema “Kweli
Panya wewe mtu
mbaya sana, wa-
stahili kuuawa
Mbwa na paka
wamepewa ruk-
sa kukurarua,
Mbwa na Paka
wakafurahi
wakamkamat
a mama
yangu, wa-
kamwua u-
pesi, tena
wakawa-
kamata
ndugu za-
ngu wote,
mimi nilikaa peke
yangu, nikihuzunika saaaana.”
SHINDANO LA KAKA 33
Panya akajikatiza maneno akamwambia Elisi
akasema “ Husikilizi! Unafikiri nini?” Elisi
akajibu kwa unyenyekevu akasema “ Sifikiri
kitu Panya, nasikitika sana, tafadhali uni-
samehe.” Lakini yule mnyama alikasirika ka-
bisa akaondoka, Elisi na wanyama wengine
wote pia wakamwita, lakini alikataa kurudi,
akazidi kukaza mwendo.
Elisi alisema “ Dina angekuwapo hapa ange-
mrudisha upesi Panya.” Lauri akauliza “ Dina
nani”? WElisi akajibu kwa furaha akesema
“Dina ni paka wangu, ni hodari kabisa kuka.-
mata panya, tena anaweza kukamata ndege,
ni paka mwenye akili nyingi.”
Maneno yake Elisi yaliwatia hofu wale we-
nzake ndege; wengi wakaondoka wakaenda
mara moja bila kuaga, wengine wakasema
“Baridi kali sana, lazima turudi nyumbani.”
Hawakumtaka Elisi awasindikize. Kwa saba-
bu mbali mbali wote wakaenda zao; Elisi
akabaki peke yake kabisa, akasema kwa huzuni
“Wasa nasikitika ya kuwa nilisema habari za
Dina, imebainikia ya kwamba wenyeji wa nchi
hii wanamchukia, ingawa ni paka mwema kupita
wote. Ee Dina nina haja nawe sasa, je, sitakuona
tena?” Elisi akatoa machozi, maana amekuwa
mpweke, mwenye huzuni, walakini baadaye
kidogo alisikia tena mashindo ya miguu midogo
njiani, akatulia akidhani kuwa ilikuwa Panya
aliyekuwa anarudi. Kumbe halikuwa yeye!
; : -
AIW—C
SURA IV
NYUMBA YA SUNGURA
ALIKUWA Sungura Mweupe aliyekuwa akirudi,
akitafuta huko na huko alimokuwa akienda,
kana kwamba amepotelewa na kitu, akanu-
ng'unika akisema “Mama Mkubwa! Mama
Mkubwa! Maskini miguu yangu, masikio na
midomo yangu! Bila shaka nitakatwa kichwa!
Nimeviangusha wapi?” Mara Elisi akabahati-
sha ya kuwa alikuwa anatafuta upepeo na
kofia yake, aliyoangusha zamani kidogo; aka-
msaidia katika kutafuta kwake, bali hakuviona.
Mahali pamebadilika tangu kuogelea kwake
Elisi kidimbwini, na kile chumba kirefu chenye
meza ya kioo, na mlango mdogo kimetoweka
kabisa.
Kitambo kidogo Sungura akamwona Elisi,
ambaye alikuwa akitafutatafuta, akamwita
kwa hasira akisema ““ Ewe Meriana, wafanyaje
hapa? Rudi nyumbani upesi, kaniletee upe-
peo na kofia nyingine.”
Elisi akaogopa sana akakimbia kwa hima
njia aliyoielekeza Sungura, hakukaa wala ha-
kumwonyesha Sungura kosa lake, na alipo-
kuwa akitembea alisema moyoni “ Amenidhani
mimi ni yaya, atashtuka atakapoona kuwa si-
3
NYUMBA YA SUNGURA 35
ye, lakini afadhali nimletee upepeo na kofia.”
Kabla hajamaliza maneno akaona nyumba
ndogo safi, na mlangoni imeandikwa na herufi
za shaba: “ BWANA S. MWEUPE.”
Elisi hakupiga hodi, akaingia nyumbani aka-
panda ngazi kwa hofu, akadhani ya kuwa ata-
kutana na huyu yaya mwenyewe, atupwe nje
kabla hajapata upepeo na kofia ya Sungura.
Elisi alicheka alipofikiri ya kwamba ametumwa
na sungura, akasema “ Nitakaporudi kwetu
labda Dina atanituma pia.” Akaingia ndani
ya chumba kidogo, safi kabisa, chenye dirisha
na meza; na mezani akaona upepeo na kofia
ndogo.
Elisi akafurahi, basi alipokuwa katika kuvi-
twaa, aliona chupa mezani, na ingawa haina
cheti cha maelezo kama cha ile ya kwanza, au
neno “ uninywe ” aliinywa dawa iliyomo ndani,
akasema ““ Sasa nitapata mambo gani?” Maa-
na Elisi alifahamu siku zile kuwa anywapo
cho chote hufikiwa na mambo mbali mbali.
Elisi akasema “ Labda dawa hii itaniongeza
urefu, nimechoka kuwa mbilikimo namna hii!”
Dawa ilimfaa upesi kabisa, na kabla hajaweza
kutoka chumbani alijidunda kichwa darini,
akairudisha chupa mezani akasikitika ya kuwa
amekunywa nyingi, sababu alikuwa hajaacha
kukua, akakaa chini akanyosha mkono diri-
shani, na mguu katika bomba la moshi, apate
kuwa na nafasi, akasema ““ Nitokeje sasa ?”
36 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Kwa bahati wakati ule ule nguvu ya dawa
ilipungua, lakini alikuwa hana wasaa hata wa
kugeuka, amebanwa kabisa, hakujua njia ya
kuokoka, akasema moyoni “ Kwetu maisha
yangu mazuri kupita ya hapa, huko siku-
punguka wala sikuongezeka kila nilapo au
niywapo, tena situmwi na sungura wala pa-
AA AAA AA
yi
1
“
j |
j!
i!
i
hi
v
Ba
i
iJ
A
YA
“
AS RI
Ny
nya. Sasa nasikitika ya kuwa nimemfuata
sungura pangoni, nasikitika kama sisikitiki.
Zamani nilisoma hadithi za namna hii, siku-
dhani ya kuwa mimi nitakuwa mtu wa hadithi.
Ni heri kiandikwe kitabu juu ya habari hizi,
au labda nitakiandika mwenyewe nitakapo-
kuwa mtu mzima.” Kabla hajamaliza kusema
akasikia sauti ya Sungura nje, aliyekuwa aki-
NYUMBA YA SUNGURA 37
mwita yaya, akisema “ Ewe Meriana, niletee
kofia upesi!” Elisi akasikia mashindo ya mi-
guu midogo ngazini, akatetemeka kwa hofu,
akasahau ya kwamba yeye ni mkubwa kabisa
kuliko Sungura na wenzake, wala hakuna
haja ya kuogopa. Sungura Mweupe akafika
mlangoni akajaribu kuufungua, bali alishi-
38 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
ndwa, maana Elisi alikuwa ameuzuia kwa
kisigino, mnyama akasema ““ Vema, nitaingia
dirishani.” Elisi akajibu moyoni akasema
“ Haingii, nitamzuia.” Akangoja mpaka aka-
msikia nje, chini ya dirisha, akatoa mkono
kwa kumdaka, lakini alimkosa, akasikia ki-
shindo kama cha kuanguka kitu penye mitungi
mingi, kikaivunjavunja, tena alisikia yowe
ndogo, na halafu sauti kali, (Ilikuwa ile ya
Sungura Mweupe.) akiita akisema ““ Ewe Patriki,
umekwendapi?” MKisha Elisi akasikia sauti
asiyopata kusikia, ya mtu mmoja akijibu aki-
sema ““ Nipo Bwana, nafukua matunda.” Su-
ngura akasema “Maana yake nini kufukua
matunda? Mjinga we! Njoo upesi unisaidie
nitoke katika mitungi.” Elisi akasikia tena
kelele za vyombo vikivunjika; Sungura aka-
sema “Sasa, niambie Patriki, waona nini
dirishani ?”
“ Naona mkono Bwana.”
“ Haiwezekani! Sijapata kuona mkono mku-
bwa namna hii. Mpumbavu we! Tazama
umeenea dirisha lote !”
“Kweli Bwana, lakini ni mkono ujapokuwa
mkubwa.”
“Vema, Lakini unafanya nini dirishani ?
Hauna ruksa kuwapo huko, nenda kauondoe,
kautupe.”
“Mimi naogopa Bwana, tena sitaki kuutupa.”
“ Fuata maneno yangu upesi, mwoga we!”
NYUMBA YA SUNGURA 39
Elisi akataka tena kumkamata Sungura lakini
akashindwa, alisikia mayowe mawili memba.-
mba, na tena ke-
lele za mitungi
inayovunjika,
akasema kimoyo-
moyo “ Mitungi
mingi iko kule,
haiwezekani mimi
kuvutwa katika
dirisha, lakini ni-
mechoka kulala
hapa.” Akasiki-
liza sana, haku-
sikia kitu, ila
kimya tu, aka.-
ngoja kwa dakika
chache, halafu
akasikia sauti
nyingi za watu wa-
liokaribia; mara
kwa mara maneno
yao yalifuatana,
ndiyo: “Iko wapi
ngazi?” “Lete
mbili, kazifunge
. pamoja.” “ We-
we, shika kamba hii.” “lItafaa, ina imara.”
“ Mathubuti kabisa.” “Nani atakayetelemka
bombani?” “Si mimi.” “Mimi sitaki.”
40 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
“Mimi naogopa.” “Mimi nakataa.” “Wi-
lyam, hii ni kazi yako, umetumwa na Bwana,
panda upesi!” , Wakumbuka Msomaji ya kwa-
mba mguu wa Elisi ulikuwa bombani, kwa
hiyo aliposikia shindo darini alisema moyoni
“ Wilyam ndiye atakayeshuka bombani, lija-
pokuwa jembamba nadhani ya kuwa naweza
kumpiga teke.” Akaukweza mguu kama ali-
vyoweza, akangoja mpaka akasikia mnyama
bombani, ndipo akapiga teke kwa nguvu.
Hakujua hata kidogo ni mnyama wa kabila
gani.
Palikuwa na ghasia kabisa nje, Elisi aka-
sikia maneno haya: “ Tazama Wilyam!” “Loo
anaruka kama ndege!” “ Uchawi gani huu ?”
“ Mkamate Patriki we.” “Mimi nitampa da-
wa.” “Mshike kichwa.” “Waonaje Kaka.”
“Mambo gani umepata ?” “ Tuambie yote.”
Wilyam akajibu kwa sauti ndogo akasema
“Mimi siwezi kueleza, kiti kikubwa, kama
mguu wa binadamu kimenipiga nilipokuwa
bombani, nikatoka kama mshale uliotoka ka.-
tika upindi.” Wenzake wakamjibu “ Kweli,
umeruka kama mshale.”
Sauti ya Sungura Mweupe ikasikilizana, wote
wakanyamaza; Bwana Sungura akasema “ La-
zima tuichome nyumba hii.” Elisia kapaza
sauti sana akasema ““Mkichoma nyumba nita-
mtuma Dina awakamate ninyi nyote.” Mara
wote nje wakatulia, baadaye wakaanza tena
NYUMBA YA SUNGURA 41
kutembeatembea. Sungura Mweupe akasema
“ Kikapo kimoja kitatosha kwanza.” Elisi aka-
fikiri “Ndani ya kikapo mna nini?” Mara
akatambua, maana mawe mengi madogo yali-
ingia dirishani, machache yakampiga usoni;
akasema ““ Tulieni sasa hivi.” Mara watu wa nje
wakasita kuyatupa. Elisi akayatazama mawe
yaliyokuwa chini, akaona ya kuwa yame-
geuka kuwa pelemende, akadhani akasema
moyoni “ Nikila pelemende labda urefu wangu
utapungua.” Akaila moja, akafurahi sana kwa
kuwa amepunguka mara, akawa mdogo wa
kuweza kuondoka; akatoka nyumbani.
Nje palikuwa na makutano ya wanyama na
ndege; Wilyam alikuwa Mjusi, alikuwa kati
kati ya kundi, akibembelezwa na Komba
wawili, waliokuwa wakimpa dawa.
Walipomwona Elisi wanyama wote wakapiga
kelele sana, wakafukuza upesi wapate kumka.-
mata; Elisi akapiga mbio akawashinda, aka-
jificha kati ya miti mikubwa mizuri sana
mwituni.
Elisi alitembeatembea mwituni, akasema
“ Kwanza afadhali nifikiri jinsi ya kutengeneza
urefu wangu, niwe sawa sawa, kisha niingie
katika bustani niliyoiona zamani kidogo.” Ma-
shauri haya yalikuwa mazuri lakini Elisi haku-
jua jinsi ya kuyatimiza.
Ghafula yule mtoto alishtuka kusikia kilio
cha mbwa juu yake, akainuisha macho akaona
42 — ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
mtoto wa mbwa aliyekuwa akimtazama kwa
makini; mbwa akanyosha mguu mmoja aka-
jaribu kumgusa mtoto; Elisi akapiga uruzi
au YA
UNE 5. Ba | )
A
akasema “Basi mbwa, pole pole!” Lakini -
aliogopa sana akasema “ Akiwa na njaa ata-
nila.” Akatwaa fimbo akacheza na mbwa
NYUMBA YA SUNGURA 43
akijilinda nyuma ya maua yenye miiba, aka-
sema kimoyomoyo “Ni kama kucheza na
tembo!” Akawa na hofu kuwa atavunjika
na miguu yake, lakini hakuthubutu kukimbia
mpaka mbwa akawa amechoka kabisa, alipo-
kwisha kuchoka mbwa akalala akitweta sana,
akafumba macho; mara Elisi akakimbia, na
hakukaa mpaka kilio cha mbwa kilisikilizana
kwa mbali sana.
Elisi alipumzika penye kivuli cha njugu,
akajipepea kwa jani moja, akasema “ Wala.-
kini ni mbwa mzuri sana, bali mimi mdogo,
sikuweza kumtiisha, lazima nijiongeze urefu,
lakini hapa chakula hakuna, sijui nitakacho-
kula.” Elisi akatafutatafuta bila kuona cha-
kula hata kidogo.
Mara Elisi aliona uyoga, urefu wake kama
yeye mwenyewe, akatazama chini yake, hala-
fu akataka kutazama juu ya ule uyoga, aka-
chuchumia akaona juu Mdudu mkubwa wa
rangi ya buluu, alikuwa amekaa amejikumbatia
akivuta kiko cha Kihindi; hakujishughulisha
na Elisi kwa neno lo lote.
Kaa
La,
4
IS
4
4
II,
Ki | KA
N ”
am LI
aa SI
SURA V
MASHAURI YA MDUDU
ELisi na yule Mdudu walitazamana kwa dakika
chache, bila kusemezana. Mwisho Mdudu ali-
toa kiko kinywani akasema kwa ulegevu “ Ja-
mbo mwanangu, nani wewe?” Elisi akajibu
kwa hofu kidogo akasema “Sijui Bwana,
saa ile nimegeuka mara nyingi sana, na sasa
labda ni mtu mwingine!” Mdudu akajibu
4
MASHAURI YA MDUDU 45
“Sielewi, eleza tena.” Elisi akasema ““ Siwezi
kueleza, maana sijifahamu mwenyewe, lakini
najua hili, ya kuwa ni vigumu sana kuwa na
urefu mbali mbali katika siku moja.” Mdudu
akavuta kidogo akasema “Si vigumu.” Elisi
akajibu “Wewe mwenyewe kama utakuwa
kama kipepeo utafahamu kuwa ni vigumu.”
Mdudu hakukubali akasema “La! Hasha!”
Elisi akajibu akasema “Labda sisi mambo
yanatudhihirikia, lakini kwangu mimi naona ni
vigumu kugeuka.” Mdudu akamtazama Elisi
kwa dharau akasema “Nani wewe?” Elisi
akakasirika akasema ““ Umeturudisha mwanzo
wa mazungumzo yetu, nadhani ni juu yako
kwanza kuniambie habari zako.” Mdudu aka-
mtazama akasema “Kwa nini?” ELlisi aka-
shindwa kabisa kujibu, akaenda kidogo, lakini
yule mdudu akamwita akasema “ Rudi. Nina
neno.” Elisi akakubali akarudi. Mdudu aka.-
sema “ Usikasirike. Basi.” Elisi akazidi ku-
kasirika akasema “ Neno lako ndilo hili tu ?”
Mdudu Mdudu akajibu “La.” Yule mtoto
akafikiri ya kuwa anayo nafasi, kwa hiyo
akangoja, apate kusikia maneno ya Mdudu;
akakaa kwa uvumilivu; muda wote huyu
Mdudu alikuwa akivuta kiko kwa pole pole,
halafu alinyosha mkono akaondoa kiko mdo-
moni akasema ““ Je, wadhani kuwa umegeuka ?”
Elisi akajibu kwa huzuni akasema “ Kweli
nimegeuka, kwa hiyo nasikitika sana, tena kwa
46 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
sababu hii siwezi kukumbuka elimu niliyoji-
funza chuoni, na urefu wangu umwbadilika
mara nyingi.” Mdudu akamtiisha Elisi kama
mwalimu, akasema “Soma kwa moyo “ We
mzee Baba Wilyam.'” Elisi akasimama wima
akajifunga mikono nyuma, akanena
wi Y WI DI Y Mza
Bi ya Y 5 LA
SI f KUZUA j AN
” NI
TA -
Nd ia
YA EN WAL
YA
NI wa
| N ua
YA,
A wa
YA
“We mzee Baba Wilyam,” 'kasema mwanake,
“< Nyeupe kabisa nywele,
Kusimama kwa kichwa imekufalia ?
Je, utacheza. milele ?””
Baba Wilyam 'kajibu “ Katika utoto
Nilihofu kudhuru ubongo,
Bali sasa najua kichwani ni tupu,
Nikazidi pindua mgongo.”
MASHAURI YA MDUDU 47
KEeEv g.
Ma AA AA WATU AU |
“Wem - zee Bamba Wil-yam,” 'ka - se- ma mwan-
UJANA | aa Wa
a-ke, “N-ye - u-peka - bi —- sany - we - le,
| kani EN TUI
Ku-si - ma-makwa ki-chwai - me- ku-fa-
1| aw AWA NUNA
-Ti - a? Je, u-ta - che-zami - le - le?”
TI
lA
Jialaa 3
KA Aa ”
J7Ph ji ;
j UE.
C AI ; | ua Z
v AU iji | AI Y . yA
(mp i j ji ai l
yy IJI Wi
Mwana 'kasema ““ We mzee baba yangu,
Kama nilivyosema zamani,
Walakini ingia kwa kichwani chini
Ni desturi ukija nyumbani.”
48 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Mzee akasema ““ Katika utoto
Nilijilainisha mwili
Kwa dawa katika sanduku za chuma
Na nitakuuza mbili.”
WAS
- ”
Aa
:
—
————
AI
Kijana 'kasema “ Wewe kibogoyo,
Huwezi kula ila wali,
Lakini wameza mbuzi mzima
Jinsi gani? Nijibu maswali.”
“Nilikuwa Mwamusi zamani kidogo,
Na Mwamusi ni mtu wa cheo,
Kila siku mashauri, na tayani mwangu
Nguvu hukaa hata leo.”
MASHAURI YA MDUDU 49
Kijana 'kasema ““ We mzee Baba Wilyam,
Lakini najua, waweza
Simamisha samaki mkubwa puani
Namna gani mzee ? Nieleza.”
Mzee akasema kwa nguvu na chuki
“ Nimejibu maswali matatu,
Itatosha mwanangu uache ujinga,
Nenda! Nisikupige kiatu.”
am VINA CIA wa SA
YA Au YA YA
ad KU ; AL
4 ? nn
YA ERA
y AN A WI
# AA
;
ka
”
-
Ga
ULA MITA
TA 15 ”
IT aa WI “ AU
wai WA AZI
”
Ii
A
iE
Mdudu akasema ““ Maneno haya si sawa sa-
wa.” Elisi akajibu akasema “ Hata mimi nao-
na si sawa sawa kabisa.” Mdudu akaitikia
“Si sawa sawa hata kidogo.” Wote wawili
wakanyamaza muda wa dakika chache, hala-
>
AIW—D
50 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
fu Mdudu akasema “ Wataka kuwa na urefu
gani?” Elisi akajibu “Habari za urefu ni
mamoja kwangu, lakini sipendi kugeukageu-
ka hivi. Umefahamu?” Mdudu akajibu “ Si-
jui.” Elisi akanyamaza kwa kuwa maisha
yake yote hajapata kupingwa na maneno na-
.mna hii, akakasirika; Mdudu akamwuliza “ Je,
u radhi sasa?” Elisi akajibu “ Ningependa
kuwa mkubwa zaidi kidogo, maana kuwa na
urefu kama uyoga tu si vizuri.” Mdudu aka-
simama wima akasema kwa nguvu “ Urefu wa
uyoga ni kimo kizuri kabisa ' (huu ndio urefu
wa Mdudu mwenyewe). Elisi akapiga mguu
akasema kwa hukumu “ Mimi sijazoea kuwa
mdogo.” Akawaza ya kuwa vyumbe vya nchi
aliyokuwamo hawakawii kuchukiwa. Mdudu
akasema “Baadaye utazoea.” Akatia kiko
midomoni akavuta. Elisi akangoja kwa uvu-
milivu hata Mdudu aliposema tena. Mdudu
akaendelea kuvuta tumbako, halafu akapiga
mwayo mara mbili tatu, akajitetemesha, aka-
shuka juu ya uyoga, akatambaa katika ma-
jani; alipokuwa akienda akasema “ Upande
mmoja utakuongeza, upande wa pili utaku-
punguza urefu.” Elisi akasema ““ Asante Mdu-
du.” Akanena kimoyomoyo. “ Pande za ni-
ni?” Mdudu akajibu kana kwamba anawaza
tu, akasema “ Pande za uyoga.” Akatoweka
mwituni.
Elisi akakaa akautazama ule uyoga, apate
MASHAURI YA MDUDU 51
kutofautisha pande zake, kazi hii ilikuwa ngu-
mu maana uyoga ulikuwa mviringo kamili;
akanyosha kabisa mikono akashika ukingo wa
uyoga kwa mikono miwili akaumega vipande
viwili, kimoja katika mkono wake wa kulia na
kingine katika mkono wa kushoto, akajiu-
liza “Kipande kipi kitaniongeza, na kipande
kipi kitanipunguza ?” Akala kidogo kile ki-
pande cha mkono wa kulia, Kabla hajamaliza
kula alijipiga vidole vya miguu kwa kidevu;
akaogopa sana, akaanza upesi kula kile kipande
cha mkono wa kushoto kazi hii ilikuwa ngumu
sana maana kidevu kilikuwa kimekaribia sana
vidole vyake vya miguu, ilikuwa hakuna nafasi
ya kutafuna, lakini kwa shida akaweza, aka-
sema kwa furaha “ Sasa kichwa kimeokoka.”
Lakini kabla hajamaliza kusema aliogopa tena
kwa kuwa hakuweza kuona mabega, hata
kidogo, alipoinamisha macho hakuona kitu
ila shingo tu; shingo ilikuwa refu sana kupita
ile ya twiga, na shingo yenyewe ilitokeza juu
ya majani ya miti, juu kabisa, kama mnazi
katika mashamba. Elisi akafikiri “ Majani yale
ya nini? Tena mabega yangu ya wapi? Si-
wezi kujiona, hata mkono.” Alipokuwa aki-
sema maneno haya alinyosha mkono lakini ha-
kuuona, aliona tikisiko la majani tu. Kwa
sababu hakuweza kuufikisha mkono kichwani
alijaribu kuinamisha kichwa kifikie mikono,
akaona furaha ya kuwa aliweza kuipindapinda
52 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
shingo kama mwili wa nyoka, akaona ule
uwanda wa majani, na kumbe ulikuwa vilele
vya miti tu.
Ghafula ndege kubwa aliruka usoni mwake
Elisi, akampiga sana kwa mabawa, akasema
kwa sauti nyembamba “Nyoka! Nyoka!”
Elisi akajibu kwa hasira ““ Usinipige hivi, mimi
si nyoka.” Lakini Ndege akazidi kufanya ma-
tata na kusema “Nyoka! Nyoka!” Akatoa
machozi akasema “Kila mahali nimetafuta,
lakini hapana mahali pa kuwafalia watoto wa-
ngu.” Elisi akajibu akasema “Sielewi hata
kidogo.” Ndege akasema “ Nimejaribu ma-
shina ya miti; nimejaribu dari za nyumba, ni- '
mejaribu maboma ya shamba, bali wale nyoka
wabaya wamenifuata kila mahali.” Elisi aka-
zidi kushindwa, lakina hakumkatiza maneno
ndege, mpaka alipokwisha kusema. Ndege
akaendelea kunena akasema “Ni kazi kubwa
kuangua mayai, tena imenilazimu kuyalinda
kutwa kucha, sikuupata usingizi tangu juma
tatu, nimechoka kabisa.” Elisi akaanza ku-
fahamu akamjibu akasema “ Nasikitika sana
ya kuwa umesumbuka hivi.” Ndege akasema
“ Wakati nilipouchagua mti mrefu kupita yote
mwituni na nilipodhani ya kuwa mayai yangu
yatakuwa salama mara nilimwona nyoka ali-
yetoka mbinguni. ... Ewe Nyoka! Nenda
zako.” Elisi akajibu akamwambia ““ Mimi si
nyoka, mimi... mimi...mimi....” Ndege
MASHAURI YA MDUDU 53
akasema “Sasa nani we? Naona ya kuwa
wajaribu kusingizia kitu.” Elisi akajibu “ Si-
singizii; mimi binadamu.” Ndege akamtazama
Elisi akacheka akasema “ Nimeona watoto
wengi sana, lakini sijapata kuona mtu mwenye
shingo refu kama yako, huwezi kukana ya
kwamba wewe u nyoka, je, huli mayai?”
Elisi akajibu “ Nala mayai, lakini ni desturi
ya wanadamu kula mayai, kama ilivyo desturi
ya nyoka.” Ndege akasema “ Sikusadiki, la-
kini ikiwa kweli kwamba wanadamu wanakula
mayai kama nyoka, basi mimi nawachukia
kama nilivyowachukia nyoka.” Elisi akajibu
akasema ““ Mimi sitafuti mayai yako, hata kama
ningetafuta nisingependa yako, wala mimi sili
mayai mabichi.” Ndege akatulia akasema
“Vema, nenda zako.” Akarudi kiotani. Eli-
si akaendelea kuinamisha kichwa kama alivyo-
weza, ilikuwa kazi ngumu, maana mara kwa
mara shingo yake ilikwama matawini. Mwisho
akafaulu akakumbuka ya kwamba alikuwa
ameshika vile vipande viwili vya uyoga. Akaa-
nza kula, kimoja kwanza, kisha kingine mpaka
urefu wake ukawa sawasawa, akajichangamsha
akasema “Sasa limetimia shauri langu nusu
yake, lililobaki kwangu ni kuona bustani.”
Akatembeatembea mwituni. Kitambo kidogo
Elisi akaona nyumba ndogo, kimo chake kiliku-
wa kama cha meza; akajiuliza ““ Nyumba ya
nani hii? Lakini haifai kabisa kupiga hodi,
54 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
maana mimi mkubwa! Mwenye nyumba atao-
gopa sana kama akiona jitu kama mimi?”
Akala kidogo kipande kile cha uyoga cha
mkono wa kulia, wala hakuthubutu kukaribia
nyumba mpaka alipokuwa amejipunguza akawa
na urefu wa inchi tisa.
UMO
YA ka
SURA VI
NGURUWE NA PILIPILI
ELisi alisimama akatazama nyumba muda
wa dakika chache, akaona kuwa ilikuwa nyu-
mba ya Kizungu, safi kabisa; na alipokuwa
akisimama akaona askari aliyetoka mbio mwi-
tuni; alimjua kuwa ni askari kwa ajili ya ma-
vazi yake; lakini usu wake ulifanana na ule
wa samaki. Askari Samaki akaenda mlangoni
akabisha sana, akapiga hodi mara nyingi;
55
56 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
mlango ukafunguliwa na askari mwingine mwe-
nye uso wa chura, alitoka nyumbani. Elisi
akasogea kidogo apate kusikia maneno yao.
Askari wa kwanza alikuwa na barua kubwa
sana, akampa askari wa pili kwa heshima
akasema ““ Barua hii inatoka kwa Malkia Mzu-
nguwapili, inakwenda kwa Mama Mkubwa,
ataka acheze Kriketi naye.” Askari mwenye
uso wa chura akayakariri maneno yale aka-
sema ““ Barua hii inakwenda kwa Mama Mku-
bwa, inatoka kwa Malkia Mzunguwapili, ataka
acheze Kriketi naye.” Askari wakasujudiana
sana, na kwa hiyo Elisi alicheka mno, akaki-
mbia tena mwituni wasiweze kumsikia. Ali-
potazama tena aliona ya kwamba Askari Sa.-
maki alikuwa amekwisha kwenda, na mwingine
alikaa penye mlango akitazama mbinguni ka.-
na kwamba ni mpumbavu; Elisi akaenda mla-
ngoni akabisha akapiga hodi; Askari Chura ha-
kumzuia, akamwambia “Unapiga hodi bure
kwa sababu mbili; ya kwanza kwa kuwa sisi
sote wawili tupo upande wa nje wa mlango;
ya pili kwa kuwa wale waliomo ndani wana-
fanya kelele sana, hawawezi kusikia sauti yako.”
Elisi akasikiliza na bila shaka palikuwa na
ghasia kubwa ndani; alisikia kilio cha mtoto
mchanga, na chafya nyingi, na mara kwa mara
shindo kubwa kana kwamba sahani au birika
limevunjwavunjwa. Elisi akasema “ Nataka
kuingia.” Chura akajibu “ Mlango ungekuwa
NGURUWE NA PILIPILI 57
kizuio kati yetu ingefaa kupiga hodi.” Ali-
pokuwa akisema Askari hakuacha kutazama
mbinguni; Elisi akasema kimoyomoyo “ Labda
na lazima afanye hivi, maana macho yake ni
juu ya kichwa chake, lakini sharti anijibu.”
Akapaza sauti akasema tena ““ Nataka kuingia.”
Chura akajibu ovyo akasema “Mimi nitakaa
hapa mpaka kesho.” Alipokuwa akisema mla-
ngo ulifunguliwa na sahani kubwa (iliotupwa
na mtu ndani ya nyumba) ikaruka ikampiga
chura puani, ikavunjika penye shina la mti
nyuma yake; Askari akaendelea kusema kana
kwamba hakupigwa, akanena “... au labda
kesho kutwa.” Elisi akajibu kwa hasira aka-
sema, “Namna gani! Nipe ruksa kuingia.”
Askari akanena “Je, umepewa ruksa kuingia
na mwenye nyumba?” Elisi akanyamaza akao-
na haya. Chura akaendelea kusema “Mimi
nitakaa hapa mara kwa mara kwa siku nyingi
sana.” Elisi akasema “ Na mimi je?” Aska-
ri akapiga uruzi akasema ““ Fanya upendavyo.”
Elisi akasema kimoyomoyo “ Hakuna faida
kuzidi kusema naye, yeye mjinga kabisa.”
Akafungua mlango mwenyewe akaingia nyu-
mbani.
Ndani palikuwa na jiko la Kizungu; lililotoa
moshi nyingi sana. Mama Mkubwa alikuwa
amekaa kitini akimbembeleza mtoto. Mpishi
alikuwa akikoroga chakula katika chungu kiku-
bwa. Elisi akaenda chafya akasema “ Zimo
58 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Pilipili nyingi sana katika chakula!” Hata
Mama Mkubwa alienda chafya mara kwa
mara, na yule mtoto hakuacha kuenda
chfaya na kulia. Walikuwa watu wawili tu
waliokuwa hawaendi chafya, walikuwa Mpishi
na Paka mkubwa aliyekuwa amekaa penye
p
Maa aa an
AA
moto akichekelea sana. Elisi akasema ““ Shi-
kamoo Mama Mkubwa. Tafadhali niambie kwa
sababu gani Paka wako ametoa meno hivi?”
Mama Mkubwa akajibu akasema “ Kwa saba-
bu ni Paka Mcheshi. Nguruwe We!” Alise-
ma maneno yale ya mwisho kwa nguvu sana,
Elisi akashtuka akadhani ya kuwa mama ame-
NGURUWE NA PILIPILI 59-
msema yeye ““ Nguruwe ”” lakini alifahamu ya
kuwa amemwita yule mtoto, akajipa moyo
aksema “ Sikujua ya kuwa paka huweza ku-
chekelea!” Mama Mkubwa akajibu “Ana-
weza. Tena wengi wametenda hivi.” Elisi
akanena “Mimi sijapata kuona paka ache-
kaye,” Mama Mkubwa akajibu “ Pana mambo
mengi ambao wewe hujapata kuona.” Mpishi
alikiepua chungu jikoni, akatwaa vijiko na
sufuria na sahani akawatupia Mama Mkubwa
na mtoto, Mama hakumjali mwanawe ambaye
alikuwa akilia sana wakati ule wote, wala
haikujulikana kama amepigwa ama siyo. Elisi
akasema “ Angalia Mpishi wee umempiga mto-
to!” Mama Mkubwa akasema “ Watu wote
wakishika lao ulimwengu utaendelea vizuri.”
Mpishi akarudi mekoni akakoroga chakula kwa
nguvu, akazidi kunyunyiza pilipili. Elisi aka-
sema ““ Tafadhali Mama, niambie ...” Ma-
ma Mkubwa akamkatiza maneno akasema “ Usi-
niudhi.” Akambembeleza sana mtoto aka-
mwimbia akisema:
Mkaripie mwana wako,
Na akienda chafya,
Atenda hivi kusumbua,
Hajambo, ana afya.
Wote, pamoja na Mpisha na Mtoto Mchanga
wakaitikia: “ Wawawawawa ” Mama akaimba
ubeti wa pili, akamrusha mno mtoto, aliyelia
60 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
hata Elisi alisikia kwa shida maneno ya
wimbo.
Namkaripia mwana wangu,
Nampiga akilia
Apenda sana pilipili
Na moshi chafu pia.
Mama Mkubwa akamtupia Elisi mtoto mcha.-
nga akasema ““ Mshike wee, maana imenilazi-
mu nijiweke tayari kucheza Kriketi na Malkia
KEY G minor.
li ka IA WA AA AA
M - kari - pi-e mwa-na wa-ko, Na
MA kaa Aa .m|fimirid
a-ki - en-da chaf-ya, A - tenda hi-vi
l miri dis | AWA aaa KA kii |
ku-sum-bua, Ha-jam-bo, a-na af - - ya.
Mzunguwapili.” Akatoka chumbani, Mpishi
akamtupia sufuria.
Elisi alimshika kwa shida mtoto, maana ali-
kuwa ajinyonganyonga, mwisho akamshika sa-
na kwa mguu wake wa kushoto na sikio la
kulia, akamchukua nje mwituni apate kupu-
nga hewa, akasema “Lazima nimpeleke nje,
wasimwue kule jikoni. Pole mwanangu, wa
mekupiga sana sivyo? Watu hawa ni waji-
nga kabisa, hawajui kukutunza.” Mtoto aka-
NGURUWE NA PILIPILI 61
guna kama kujibu, Elisi akamwambia “ Usi-
gune! Si vizuri kuguna kama nguruwe.” Yule
Mtoto akazidi kuguna, Elisi akamtazama sana
kwa mashaka, pua yake yalikuwa kama. pua
ya nguruwe, na macho yake yalikuwa madogo.
Elisi akafikiri ya kuwa ni kwa sababu ya kulia
yA.
sana ndipo akavimba pua; akaendelea kute-
mbea akasema “ Ukigeuka kabisa kuwa ngu-
ruwe, basi wewe si mtoto wa kusuhubiana
nawe.” Mtoto akaguna tena, Elisi akatulia
akamtazama kwa hofu, na ilikuwa hakuna
shaka, mtoto alikuwa amekwisha geuka kuwa
mtoto wa nguruwe. Elisi akamsimamisha chi-
62 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
ni, akafurahai kumwona anaweza kutembea,
alimtazama akikimbilia mwituni.
Elisi, alipokuwa peke yake akainuisha ma.-
cho akashtuka kumwona Paka Mcheshi aliye-
kuwa amekaa penye tawi la mti mbali kidogo.
Elisi akamsogelea Paka, naye alikuwa ameche-
kelea sana, yule mtoto akafikiri ya kwamba
sura yake ilikuwa ya upole, lakini meno yake
na kucha zake zilikuwa kali. Akasema kwa
hofu kidogo “ Hujambo Paka Mcheshi?” “Wa-
weza kunionyesha njia?” Paka Mcheshi aka-
jibu akasema “ Wataka kwenda wapi?” Elisi
akajibu “ Po pote nitakapo!”
“Kwa hiyo habari ya njia pia mamoja
kwako.”
“ Afadhali nifike ahali pengine.”
“Ukienda mbali, bila shaka utafika pe-
ngine !”
“ Watu gani wakaao hapa ?”
Paka Mcheshi akaelekeza kwa mguu akasema
“Huko amekaa Mwuza Kofia, na huko Kobe,
nenda kamwamkie ye yote, wote wawili wana
wazimu !”
“ Lakini mimi sipendi kusuhubiana na watu
wenye kichaa.”
“ Kwako wewe mbwa ana akili ?”
“ Naam anayo akili.”
“Vema, mbwa hutikisa mkia akipendezwa
na kitu, hunguruma akikasirika, na mimi,
' nikikasirika natikisa mkia, nikifurai nanguru-
NGURUWE NA PILIPILI 63
Ao
UC io
Nhif
Li
aila ha wa YA
Aa WA
IA
ma, kwa hiyo najua
sana ya kuwa mimi ni
mwenye wazimu.”
“ Lakini wewe hungu-
rumi! waguna tu.”
“Sema kama upe-
ndavyo. Je, utakwenda
Kriketi na Malkia leo ?”
“ Ningependa sana
kucheza, lakini sikui-
twa.” Paka Mcheshi
akajibu akasema
“Tutaonana tena
huko.” Akatoweka
mara. Elisi haku-
shtuka kwani siku zile alikuwa amekwisha
zoea mambo ya namna hii, na alipokuwa
64 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
akitazama mahali alipokuwapo paka yule
mnyama akarudi tena akasema “Je, nini ha-
bari za mtoto? Nilisahau kukuuliza.” Elisi
akajibu akasema ““ Amegeuka nguruwe.” Paka
Mcheshi akacheka zaidi, akasema “Hii si
ajabu kubwa.” Akatoweka tena. Elisi ali-
ngoja kidogo akifikiri ya kuwa labda atarudi,
lakini hakumwona; akatembea kidogo katika
UA
in
.
njia aliyoionyeshwa na Paka Mcheshi, kufikia
penye nyumba ya Mwuza Kofia. Kitambo
kidogo akainuisha macho, akamwona tena Paka
Mcheshi aliyekuwa amekaa katika tawi jingine,
yule mnyama akasema “ Ulisema “ Nguruwe '
au “Ngurubai”?” Elisi akajibu, “Nilisema
“ Nguruwe,' tena usitoweke upesi hivi, imenitia
kizungukizungu.'” Paka Mcheshi akasema
NGURUWE NA PILIPILI 65
“Vema!” Akaanza kutoweka pole pole, kwa-
nza mkia, kisha mwili, halafu uso, na mwisho
kinywa na kicheko; tena kinywa kilionekana
kidogo baada ya kwisha kutoweka maungo
yake. Elisi akasema “Haya! Zamani ni-
liona paka bila kicheko, bali sijapata kuona
kicheko bila paka!”
Kabla hajaenda mbali sana Elisi akaona
nyumba ya Mwuza Kofia, ilikuwa nyumba
kubwa, na hakuthubutu kuikaribia mpaka
alipokwisha kula kidogo kipande cha uyoga
cha mkono wa kushoto, alichokifunga nguoni,
ili apate kuongeza urefu kidogo.
Urefu wake ukawa kama ule wa mtoto wa
miaka miwili, akaikaribia nyumba, akasema
“Naomba Mwuza Kofia awe hana kichaa sana.”
AIW—-E 5
SURA VII
KARAMU YA WENYE WAZIMU
PALIKUWA na meza chini ya mti, mbele ya
nyumba; kwenye meza walikuwapo watu wa-
tatu. Walikuwa: Kobe, Mwuza Kofia, na
Komba.
Komba alikuwa amelala usingizi na wenzake
walimwagimia kwa visigino juu ya mgongo,
walikuwa wakisema kwa kelele. Elisi akafikiri
“Masikini Komba! Lakini kwa kuwa amelala
labda si vibaya.”
Ingawa meza ilikuwa kubwa watu wale
watatu walikuwa wamekaa kwa kusongana
sana penye pembe moja; na walipomwona
66
KARAMU YA WENYE WAZIMU 67
Elisi wote wakapaza sauti, wakisema pamoja
“ Hakuna nafasi, hakuna wasaa!” Elisi aka-
jibu kwa hasira akasema “ Kuna nafasi tele.”
Akakaa penye kiti kikubwa cha Kizungu.
Kobe akasema “ Wapenda kunywa mvinyo?”
Elisi akatazama mezani, hakuona kitu ila chai
tu, akasema “ Sioni mvinyo!” Kobe akajibu
akasema “ Hamna.” Elisi akasema “ Basi si
vizuri kuniitolea.” Kobe akanywa chai aka-
sema “Si vizuri kukaa penye meza yetu
usipoitwa.” Elisi akaona haya kidogo, lakini
kwa kuwa amejua ya kwamba wenzake wali-
kuwa wana wazimu akajipa moyo ' akajibu
“Sikujua kama ni meza yenu, tena pana na-
fasi ya watu wengi zaidi ya watatu.” Mwuza
Kofia akamtazama Elisi kwa makini akasema:
“ Nitamwita mzuzi, nywele zako si sawa sawa.”
Elisi akajibu “Shika lako. Huna adabu!”
Mwuza Kofia akafumbua sana macho akasema
“ Je, Kwa nini kunguru amefanana na meza ?”
Elisi akafurahai akasema “ Haya! Mafumbo!
Mimi najua maelezo yake.” Kobe akasema
“ Wajua maana yake?” Elisi akajibu “ Ha-
swa.” Kobe akamwambia yule mtoto aka-
sema “Sema kama ulivyonia.” Elisi akajibu
“ Kusema kama nilivyonia na kunia kama
nilivyosema ni sawa sawa.” Mwuza Kofia
akafikiri sana akasema “Ni mbali mbali ka-
bisa. Je, kuona ninachokula na kula nina-
choona ni sawa sawa? La!” Kobe akaitikia
68 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
akasema “ Je, kupenda ninachopata, na kupata
ninachopenda ni sawa sawa? La!” Komba.
akafumbua macho akapaza sauti nyembamba
akasema “Je, Kutoa pumzi nilalapo na kulala
nitoapo pumzi ni sawa sawa?” Mwuza Kofia
akajibu akasema “Kwako wewe Komba si
mbali, maana siku zote umelala.”
Wote wakanyamaza kidogo, Elisi akafikiri
sana juu ya mafumbo ya kungura na meza,
asielewe. Mwuza Kofia akasema “ Leo ni siku
gani ya mwezi?” Alipokuwa akisema maneno
haya akatoa saa mfukoni akaitazama sana,
akaitetemesha akaiweka sikioni. Elisi aka-
sema “Ni siku ya nne ya mwezi.” Mwuza
Kofia akamwambia Kobe akasema “Saa hii
imekosa majira kwa siku mbili. Nilikuambia
ya kwambia siagi haifai kwa saa.” Kobe
akajibu kwa unyenyekevu akasema “ Siagi
ni nzuri sana.” Mwuza Kofia akasema “ Na-
jua, lakini palikuwa na vipande vya mkate
ndani yake, ulitia siagi kwa kisu cha kukatia
mkate.” Kobe akatwaa saa, akaitazama kwa
huzuni akaichovya katika kikombe chake cha
chai, akaitazama tena, akazidi kusema ““ Lakini
ilikuwa siagi nzuri kabisa.” Elisi pia aliita-
zama saa, akasema kwa kustaajabu “Hii ni
saa ya kabila gani? Inaonyesha siku za mwezi
tu! Habari ya majira hakuna !”
Mwuza Kofia akamwuliza Elisi akasema ““ Je,
wewe unaya saa ya kuonyesha mwaka mzima ?”
KARAMU YA WENYE WAZIMU 69
Elisi akajibu akasema “Saa za kuonyesha
mwaka mzima hazipatikani maana mwaka
mzima ni kipindi kikubwa.” Mwuza Kofia
akatazama mbinguni akafunga mikono aka-
sema ““ Na mimi vile vile.” Elisi hakufahamu
akasema “' Sielewi.” Mwuza Kofia hakumjibu
Elisi, akawa anamtazama Komba, ambaye
| | It
YI /
yi Ili
amelala tena, akamwagia chai ya moto puani.
Komba akajitetemesha akafumbua macho, aka-
sema ““ Kweli ni kama ulivyosema.” Mwuza
Kofia akamwuliza Elisi akasema “Je, ume-
kwisha fahamu majibu ya mafumbo?” Elisi
akajibu ““ Nimeshindwa kabisa, uniambie ma.-
jibu yake.” Mwuza Kofia akapiga mwayo
akasema “Mimi sijui hata kidogo.” Kobe
70 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
akaitikia “Wala mimi sijui.” Elisi akasema
“Ni kupoteza nafasi kutoa mafumbo yasiyo-
kuwa na majibu.” Mwuza Kofia akashtuka
akatetemeka akasema “ Angalia mtoto! Uli-
pomjua “Narasi” kama mimi nilivyomjua,
ungalimtaja kwa heshima. Je, umepata ku-
sema na Nafasi?” Elisi akajibu ““ Sijapata
kusema naye.” Mwuza Kofia akajificha uso
kwa mikono akasema “ Mimi niligombana sana
na Nafasi, zamani kidogo, wakati wa Machezo
ya Malkia Mzunguwapili, nilipomwimbia ...
Ngoja! Nitawaonyesheni wimbo niliouimba.
Popo popo unang'aje ?
Niambie wafanyaje ?
Je, unajua wimbo huu?” Elisi akajibu “ Nu-
jua kidogo kidogo.” Mwuza Kofia akaendelea,
akaimba hivi:
“ Kama buli, kama kuni
Unaruka mbinguni.
“ Popo Popo unang'aaje ?
Niambie wafanyaje.
Popo Popo, niambie
Wafanyaje ?
Nimekuwa sijamaliza ubeti wa pili ila Malkia
akaondoka akapaza sauti sana akasema “ Amme-
uawa Nafasi. Akatwe kichwa.” Na toka saa
ile Nafasi ni adui yangu, sina bahati naye,
KARAMU YA WENYE WAZIMU 71
hanisaidii hata kidogo, na tangu saa ile siku
zote ni saa kumi na moja.” Elisi akacheka
sana akasema ““ Sasa waeleza maana ya vyombo
hivi vyingi mezani, vichache safi na vichache
vichafu, kwa kuwa kila saa ni saa ya chakula
cha jioni, na hakuna nafasi kuvisafisha.” Mwu-
za Kofia akajibu akasema “Haswa! Hiyo
ndiyo maana yake, nasi hatukai siku zote
Key C.
KIMA | ki WI kiio wide
Po-po po-po u-nang'-aje? Ni-am -bi-e
BB WA YA aa aa ia AA Wa AA KA AI ba wa Wa Wa
wa - fan - ya - je. Ka-ma bu-li, ka-ma ku-ni
Ui AA Kaa WA KAA
U-na-ru-ka m-bing - u- ni. Po-po po-po
(| SA AI AA AAA YA AA.
u - nang'-aje? Ni-am-bi-e Wa-fan - ya-je?
ie aili azi ii
Po-po po-po, ni-am - bi-e Wa-fan-ya-je ?
penye pembe hii ya meza, mara kwa mara
tunazunguka mezani.” Kobe akapiga mwayo
akasema “ Tafadhali Mama, tusimulie hadi-
thi.” Elisi akaogopa akasema “Mimi sijui
hadithi.” Kobe akasema “ Vema. Ni juu ya
Komba. Ewe! Amka Kaka.” Kobe na
Mwuza Kofia wakamfinya sana. Komba aka-
fumbua macho kwa pole pole, akasema kwa
72 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
sauti nyembamba “Mimi sikulala, nilisikia
yote yaliyosemwa nanyi.” Kobe akasema “ Ve-
ma. 'Tusimulie hadithi.” Elisi akaitikia “ Ha-
ya, hadithi Bwana Komba.” Mwuza Kofia
akasema .“ Tena endelea upesi, usilale kabla
hujamaliza hadithi.” Komba akasema kwa
haraka “ Hapo kale palikuwa na watoto wa-
tatu wanawake, majina yao yalikuwa “ Lusi,
Lesi na Tili”; wote watatu walikuwa wa-
mekaa chini ya kisima.” Elisi akauliza kwa
makini “Walikuwa wakila nini?” Komba
akafikiri kidogo akasema ““Wamekula asali.”
Elisi akasema ““ Wangalikuwa wakila asali tu
wangalikuwa hawawezi. Lakini kwa nini
walikuwa wamekaa chini ya kisima?” Kobe
akamwambia €Elisi akasema “ Kunywa chai
zaidi mwanangu.” Elisi akajibu akanena “Si-
janywa chai baado, hata kidogo, kwa hiyo
siwezi kunywa zaidi.” Elisi akatia chai katika
kikombe akanywa, akauliza tena kwa nini
watoto wale watatu walikuwa wamekaa chini
ya kisima. Komba akafikiri sana akajibu “ Ki-
likuwa kisima chenye asali” Elisi akasema
kwa hasira “ Hakuna kisima chenye asali.”
Komba akasema “Kama huwezi kuwa na
adabu afadhali wendelee wewe na hadithi.
Elisi akajibu kwa unyenyekevu akasema Nasi-
kitika Bwana Komba, tafadhali endelea na
hadithi, sitakatiza tena maneno yako, labda
hupatikana kisima cha asali.” Komba aka-
KARAMU YA WENYE WAZIMU 73
vuta pumzi akaendelea akasema “ Watoto wa-
tatu walikuwa wakijifunza kuteka” ... €Elisi
alisahau ahadi yake aliyoitoa, akasema “ Ku-
teka nini?” Komba akajibu kwa uvumilivu
akasema ““ Waliteka asali.” Mwuza Kofia aka-
sema “ Nataka kikombe safi, wote wabadili
viti.” Wote wakasogea kulia, lakini Mwuza
Kofia peke yake ndiye aliyepata faida, maana
wengine walikuwa wamekaa katika viti vya
wenzao. Elisi alikuwa amekaa katika kiti cha
Kobe; sehemu yake ya meza haikuwa safi.
Elisi hakutaka kumsumbua tena Komba, aka-
sema kwa sauti ndogo “ Lakini sijafahamu,
wameteka asali katika nini?” Mwuza Kofia
akasema ““ Mjinga we! Waweza kuteka maji
katika kisima cha maji, na waweza kuteka
asali katika kisima cha asali.” Elisi hakuu-
l
74 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
dhiki akasema “Lakini komba alisema ya
kuwa watoto wenyewe walikuwamo kisimani.”
Komba akasema “ kweli, walikuwamo, tena
walikuwa wakijifunza kuandika herufi “M.””
Elisi akauliza “Kwa nini “M' tu?” Kobe
akajibu “ Maana “M' ni herufi nzuri.” Elisi
akanyamaza, ““ Komba akafumba macho aka-
lala usingizi.” Kobe na Mwuza Kofia wa-
kamfinya, akaamka mara akaitikia “ Herufi
“M.”” Elisi alikuwa amechoka na upumbafu
huu, akaondoka, akawaaga wengine akaenda
zake, Komba akazidi kulala. Alipokuwa mba-
li kidogo Elisi aligeuka akamwona Kobe na
Mwuza Kofia wakimtia Komba bulini. Yule
mtoto akasema ““ Paka Mcheshi alisema kweli,
wote wawili ni wana wazimu. Sitarudi kwao.
Sijapata kuona karamu ya ujinga kupita hii.”
Kabla hajamaliza maneno haya akaona shina
la mti mkubwa lenye mlango; akaingia na
kumbe, alijiona katika kile chumba kirefu
chenye milango mingi, akafurahai sana aka-
sema ““ Sasa naweza kuingia bustanini, lakini
lazima nisisahau ufunguo.” Akautwaa katika
ile meza ya kioo, akaufungua ule mlango
mdogo, akala kidogo kipande cha uyoga mpaka
urefu wake ukawa kama ule wa kuku, akaingia
pangoni, .na mwisho akafika kwenye bustani
nzuri yenye maua ya kila rangi na chemchemi
ya maji baridi.
SURA YAA
MACHEZO YA MALKIA
ALiPornGiA bustanini Elisi aliona mti wa ma-
waridi, wenye maua meupe, lakini watunzaji
bustani watatu walikuwa wakiyatia rangi nye-
kundu. Elisi akakaribia kidogo, apate kuona
vizuri kazi yao, akasikiliza mazungumzo, Mtu
mmoja akasema “Sasa angalia Tano, usini-
mwagie dawa hivi.” ” Tano akajibu kwa hasira
akasema “Si kosa langu, Saba alinipiga kisi-
gino.” Saba akajibu kwa kiburi akasema
“Ni desturi yako kushtaki watu siku zote.”
Tano akajibu “ Wewe huwezi kujisifu, juzi
75
76 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
nilimsikia Malkia akisema kuwa wastahili kuka-
twa kichwa.” Mtunzaji wa kwanza akauliza
“Kwa sababu gani?” Saba akajibu “ Nita-
mwambia Tano. Sababu ilikuwa hii: Saba
alimpelekea Mpishi viazi alipotumwa vitu-
nguu.' Saba akaangusha burashi yake ya
kupakia rangi akasema kwa uhasidi “ Sikusa-
diki, maneno yako ...” Kwa ghafula yule
Mtunzaji alimwona Elisi, akajikatiza maneno,
akamsalamia sana, wengine wakamwamkia pa-
moja. £Elisi akawauliza kwa makini akasema
“ Niambie, ni kwa nini mmeyatia rangi maua ?”
Tano na Saba wakanyamaza, wakamtazama
Mbili, ambaye alikuwa akisema ““ Malkia ali-
tuamuru kupanda miti ya mawaridi yenye
maua mekundu, nasi tulikosa tukapanda miti
yenye maua meupe, na sasa tunapaka maua
rangi hiyo, makusudi kumdanganya Malkia,
asitukate kichwa.” Alipokuwa akisema neno
la mwisho Mtunzaji Tano akapiga yowe aka-
sema “Tazameni! Malkia Mzunguwapili !
Malkia Mzunguwapili! Amekuja.” Watunza-
ji bustani wakaanguka wote watatu wakalala
kifudifudi, Elisi akasikia sauti nyingi kwa mbali
kidogo, akageuka, apate kumwona Malkia.
Watu wengi walikuwa wakifuatana kwa safu.
Kwanza Askari kumi wenye rungu. (Askari ha-
wa wamefanana na Watunzaji bustani isipo-
kuwa mavazi yao, miili yao yalikuwa miraba
batabata, miguu yao imetokeza pembeni cha
MACHEZO YA MALKIA 77
chini, na mikono imetokeza pembeni kwa
juu.)
Kisha katika mfuatano wakapita Mawakili
Y
nA
ZI ai YA yA
kumi, wamepambwa kwa alama ya Huru Ka-
rata, wakaenda wawili wawili kiaskari, halafu
wakaja watoto wa Mfalme Mzunguwanne ku-
78 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
mi,. walikuwa wameshikiana mikono, wote wa-
mepambwa alama ya kopa. Mwisho wakaja
wageni, wote wafalme na malkia, na pamoja na
hawa Elisi alimwona Sungura Mweupe aliye-
kuwa amesemasema sana; lakini yeye haku-
mwona Elisi akampita. Mzunguwatatu, Mja-
nja wa Kopa akawatangulia Mfalme Mzungu-
wanne na Malkia Mzunguwapili wa Kopa, naye
alikuwa amechukua taji iliyowekwa juu ya
takia, na mwisho kabisa wa maandamano ha-
ya maarufu wakaja Mfalme Mzunguwanne na
Malkia Mzunguwapili wa Kopa wenyewe.
Elisi akaona shaka kidogo akafikiri ya kwa-
mba labda ilikuwa desturi ya nchi ile ya ajabu,
kulala kifudifudi mbele ya Mfalme na Malkia
kama walivyolala Watunzaji bustani, lakini
alitaka sana kuyatazama mavazi ya umalidadi
na utukufu wa wakuu hawa, kwa hiyo alisi-
mama kimya akangoja.
Walipokuwa wamemkaribia Elisi, watu wote
wakatulia, Malkia akamwelekeza kidole, aka- '
mwuliza Mjanja Mzunguwatatu akasema ““ Na-
ni huyu?” Mjanja akasimama mbele ya Ma.-
Ikia akacheka akanyamaza. Malkia akasita,
akasema kwa hasira “ Mpumbafu we!” Aka-
mwuliza Elisi mwenyewe akasema “ Jina lako
nani mwanangu?” kElisi akajibu “ Jina langu
Elisi.” Akafikiri akasema kimoyomoyo “ Ha-
ya! Hawa wote ni watu wa karata tu, si-
'waogopi.”
MACHEZO YA MALKIA 79
Malkia akawaona wale Watunzaji bustani
watatu, hata wakate ule walikuwa wamelala
kifudifudi, akawatazama akauliza “ Nani ha-
wa ?” (Wafahanu Msomaji ya kuwa migongo
yote ya Karata imefanana, na kwa hiyo Malkia
alikuwa hakujua wa nani. Hakuweza kuwa-
tambua kuwa walikuwa askari au mawakili
au watoto wake mwenyewe.) r
Elisi akajibu “Mimi sijui. Mimi nashika
langu.” Malkia akatetemeka kwa hasira aka-
mtazama Elisi kama mnyama ya mwitu, mwe-
nye macho ya kung'aa, akapaza sauti akasema
“Mkate kichwa! Mkate Kichwa! Mk...”
Elisi akamkatiza maneno akasema “La! Ha-
pana! Upumbafu gani huu?” Malkia aka-
tulia, Mfalme akamgusa mkono akamwambia
“Fikiri Mpenzi, huyu ni mtoto tu.” Malkia
akageuka kwa haraka akamwambia. Mjanja
“Wageuze hawa.” Mjanja akazigeuza zile
karata tatu kwa mguu. Malkia akatoa sauti
kuu akasema “Simameni.” Watunzaji wa-
kaondoka mara, wakaanza kumsujudia sana.
Malkia akasema ““ Tulieni, mnanitia kizungu-
zungu.” Malkia akautazama ule mti wa ma-
waridi akasema “ Mmefanyaje hapa?” Mbili
akapiga magoti akasema “Shikamoo Malkia
mtukufu, Tusamehe; tumejaribu ......” Ma-
Ikia akamkatiza maneno akasema “ Naona
maua,” nafahamu sana. Wakate kichwa !”
Watu wengine wakaendelea kuandamana ili-
80 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
kuwa imebaki Watunzaji bustani watatu, na
askari watatu na Elisi.
Watunzaji wakamkimbilia Elisi wapate ku-
hifadhiwa naye. 6Elisi akawafariji akasema
“ Nawapeni pole, hamtuuawa nanyi kamwe.”
Akawaficha kwa upesi katika mtungi mkubwa
uliokuwapo karibu. Askari wakawatafuta
Watunzaji muda wa dakika chache, halafu
wakakata tamaa wakawafuata wenzao. Malkia
akapiga kelele akasema “Wamekatwa ki-
chwa?” Askari wakajibu “ Vichwa vyao ha-
vionekani.” Malkia akasema “ Vema.” Elisi
akakaribia. Malkia akamwuliza Askari aka-
sema ““ Huyu ajua kucheza Kriketi?” Askari
akanyamaza. £Elisi akajibu mwenyewe aka-
sema ““ Ndio, najua kucheza.” Malkia akasema
kwa sauti kali “ Twendeni!” Wote wakaende-
lea kuandamana; Elisi pia alijiona akitembea
pamoja na Sungura Mweupe, ambaye alisema
“Jua kali sana leo siyo?” Elisi akajibu
“ Kweli ni kali. Je, umemwona Mama Mku-
bwa?” Sungura akajibu “ Nyamaza mwana-
ngu,” akamtazama kwa hofu Malkia aliye-
kuwa akitembea nyuma yake, akachuchumia
akamnong'oneza Elisi akasema “Kesho Mama
Mkubwa atakatwa kichwa.” Elisi akasema
“Amekosa nini?” Sunguru akamwuliza
“ Unamwonea huruma?” Elisi akamwambia
“La. Ni mtu mbaya, astahili kukatwa ki-
chwa, mnilikuuliza amekosa nini?” Sungura
'MACHEZO YA MALKIA 81
akasema ““ Amempiga kofi Malkia.” Elisi aka-
cheka sana, Sungura akatetemeka kwa hofu
akasema “ Angalia, Malkia atakusikia; Mama
Mkubwa alikuwa amechelewa kidogo, na. Ma-
Ikia amemkaripia, na...” Malkia akamka-
tiza maneno, akapiga kelele akasema “Kila
mtu aende mahali pake.” Wote wakapiga
mbio, wakaenda ovyo kabisa, wakasimama
huko na huko, wakaanza kucheza. Ndiyo
kwanza Elisi aone kiwanja cha Kriketi cha
namna hiyo, kilikuwa matuta matupu. Badala
ya kibau cha kupigia mpira walitumia korongo
6
AIW—F
82 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
mwekundu, na mpira wenyewe ulikuwa kaka.-
kuona, na vijiti vilikuwa askari watatu walio-
kuwa wamesimama pamoja.
Wakati wa zamu ya Elisi ya kupiga mpira
aliona taabu kidogo kwa sababu ya korongo,
alimshika kiwiliwili, na miguu yake ilikuwa
inaning'inia nyuma; lakini kila mara akimnyo-
sha shingo, yeye huikunja, kumtazama usoni,
na Elisi alikuwa sharti acheke, tena mara kwa
mara ule mpira kakakuona ulitembeatembea.
Wachezaji walikuwa hucheza wote pamoja,
hawakungojea kwa zamu, wote hugombana na.
Malkia alikuwa amekasirika sana, alipiga kelele
akajisemea ovyo mara mbili tatu kila dakika
“Mkate kichwa! Mkate kichwa!” Elisi aka-
ona shaka akasema kimoyomoyo. “Akiendelea
hivi, halafu watakuwa wamekatwa kichwa wo-
te, labda hata mimi pia!” Elisi akatafuta njia
ya kutoroka bila kufanya matata, na alipokuwa
akitafuta akaona wingu mbinguni, akalitazama
sana, akaona winguni meno na kinywa chenye
kutabusamu, akafurahi akasema moyoni “ Ha-
ya! Yule Paka Mcheshi. Sasa nitakuwa na
rafiki.” Kinywa chake kilipotosha kusema
Paka Mcheshi akamwambia Elisi akasema ““ Wa-
onaje mwanangu?” Elisi akangoja mpaka
masikio yake yalikuwa yameonekana, akasema
kimoyomoyo “ Si vizuri kumjibu mpaka masi-
kio yake yameonekana pia.” Alikuwa haku-
ngoja sana ila kichwa chote kilionekana; Paka
MACHEZO YA MALKIA 83
akafikiri ya kwamba kichwa kitatosha, kwa
hiyo hapana haja ya maungo yake kuonekana.
Elisi akasema “Hujambo Paka Mcheshi ?
Watu hawa hawachezi sawasawa, tena wamego-
mbana sana, na kanuni za machezo hawazifu-
ati.” Paka akauliza ““ Je, unampenda Malkia ?”
Elisi akajibu “Simpendi hata kidogo...”
Akajikatiza maneno kwa haraka, kwa kuwa
Malkia mwenyewe alikuwa amesimama karibu
naye, akaendelea kusema kwa hila akasema
“Kwa sababu amecheza vizuri sana, wote
hawana bahati ila yeye.” Malkia akacheka
akaenda zake.
Mfalme akamkaribia Elisi akakitazama kile
kichwa cha Paka; akamwuliza Elisi akasema
“ Dude gani hili?” Elisi akajibu “ Ni rafiki
yangu Bwana Paka Mcheshi.” Mfalme akane-
na “ Simpendi hata kidogo! Lakini, akipenda,
ana ruksa ya kunibusu mkono.” Paka Mche-
shi akajibu “Sipendi.” Mfalme akakasirika
akasema “ Usinitolee ujuvi !” akajificha nyuma
yake Elisi, akasema “ Naogopa.” Elisi akajibu
kwa kumfariji akasema “ Paka ana ruksa ku-
mtazama Mfalme. Nimesoma maneno haya
kitabuni.” Mfalme akasema “ Lazima aondo-
lewe.” Akamwita Malkia akamwambia “ Wa.-
mwona Paka yule? Lazima aondolewe.” Ma-
Ikia hakujua njia yo yote kuwahamisha adui
zake isipokuwa kuamuru wakatwe kichwa, kwa
hiyo akasema “ Mkate kichwa.” Mfalme aka-
84 ELISI, KATIKA NCHI YA AJABU
sema ““ Nitamtafuta Askari mwenyewe.” Aka-
enda zake kwa haraka. ziwa
Elisi akarudi kiwanjani apate kuwaona wali-
oshinda, lakini wote walikuwa wameendelea
ZI masia
PIA
kucheza kwa wasi wasi, na wachezaji watatu
walikuwa wamekwisha wekwa gerezani. Elisi
akageuka akaona ya kwamba kundi kubwa
la watu linamzunguka Paka; nalo lilikuwa liki-
fanya shauri ya kumkamata kichwa; wote
AI
MACHEZO YA MALKIA 85
wakawa wanasema pamoja, wakafanya kelele
sana.
Alipomwona £Elisi, Malkia akamwita aka-
mwumuru yeye kufanya shauri. Shauri la
Askari lilikuwa: “ Haiwezekani kumkata ki-
chwa mtu asiyekuwa na mwili.” Shauri la
Mfalme lilikuwa: “ Kila mtu mwenye kichwa
aweza kukatwa kichwa.” Shauri la Malkia
lilikuwa: “ Kazi hii isipotimizwa upesi watu
wote watakatwa kichwa.”
Elisi akafikiri kidogo akesama ““ Paka Mche-
shi ni mali ya Mama Mkubwa, afadhali aitwe.”
Malkia akasema ““ Amefungwa gerezani, mlete
hapa sasa hivi.” Askari akaenda mbio na ufu-
nguo mkubwa wa gereza. Kichwa cha Paka
Mcheshi kilianza kutoweka. Basi Mfalme na
askari wakakimbia huko na huko wakakita-
futa, na wengine wakarudi kiwanjani.
SURA IZY
HADITHI YA KASA
Mama Mkubwa alimsalimia €Elisi akasema
“ Nafurahi sana kuonana nawe mwanangu.”
Elisi pia akafurahi kuona ya kwamba Mama
Mkubwa alikuwa mwenye hali njema, akafikiri
ya kuwa labda hasira yake jikoni ilikuwa kwa
sababu ya pilipili tu, akasema kimoyomoyo
“ Nitakapokuwa mama mkubwa mimi, sita-
kula pilipili hata kidogo, chakula bila pilipili
si kibaya; labda pilipili ni sababu ya hasira
yote duniani, mtu akila pilipili huwa na hasira,
basi angekula kwinini angekuwa mchungu, na
angekula sukari angekuwa tamu.”
Kwa sababu ya mawazo yake Elisi alimsa-
hau Mama Mkubwa, ambaye alikuwa ame-
fuatana naye, akashtuka aliposika sauti yake.
Mama Mkubwa akasema “ Unafikiri sana mwa.-
nangu, kwa hiyo unasahau kusema; sasa hivi
siwezi kukumbuka fundisho la maneno haya,
lakini nitakumbuka bado kidogo.” Elisi aka-
jibu “ Labda halina fundisho!” Mama Mku-
bwa akasema “Hasha! Mwanangu, mambo
yote yana mafundisho kama ungeweza kuya-
fahamu.” Alipokuwa katika kusema ma-
86
HADITHI YA KASA 87
neno haya akamjongelea sana Elisi, akamwekea
kidevu katika bega lake, kijana hakupendezwa
na tendo hili hata kidogo lakini hakutaka ku-
mkataza, akasema ““ Sasa wanacheza kwa uta-
ratibu.” Mama Mkubwa akajibu “ Kweli mwa-
nangu, na fundisho lililokuambia ndilo: “ Elimu
ndio mwanga yongozayo kila shani.” Elisi
akacheka akasema ““ Nikukumbushe Mama ya
kuwa zamani kidogo ulisema ya kwamba uli-
mwengu umeendeshwa na watu walioshika
yao.” Mama Mkubwa akasema “ Tofauti ba-
ina ya kushika lako na Elimu si kubwa, na mi-
mi nitapenda sana kukushika mkono, lakini
naogopa korongo wako, nadhani ana hali mba-
ya, je, nijaribu?” Elisi akajibu akasema
“Labda atakuuma.” Alisema kivi kwa saba-
bu hakutaka kushikiana mikono na Mama
Mkubwa; huyu akasema “ Kweli korongo ni
ndege mkali—kama haradali, vyote viwili hu-
uma, na fundisho lake ndilo: “Ndege wa
kabila moja huruka pamoja.” Elisi akasema
“Lakini haradali si ndege!” Mama Mkubwa
akajibu “ Bila shaka haradali ni madini, pana
shimo kubwa la haradali, wala si mbali sana
na hapa, na fundisho lake ndilo hili: “ Paka
akiondoka, panya hutawala.'” Elisi ”haku-
jibu. Mama Mkubwa akasema “ Unazidi kufi-
kiri?” Elisi akajibu kwa kuudhika “ Lazima
nifikiri ” Mama akajibu kwa dharau akasema
“Imekulazimu kufikiri kama ilivyomlazimisha
88 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
29
nguruwe kuruka hewani, na mafundisho .....”
Wazungumzaji nawa wakamwona Malkia Mzu-
nguwapili ambaye alikuwa amesimama mbele
yao, wote wawili wakashtuka sana, Malkia
amejikumbata mwenye sura mbaya kwa ha-
sira. Mama Mkubwa akatetemeka kwa hofu,
hata hakuweza kuwapasha wenzake habari za
fundisho la maneno yake.
Malkia alimtazama Mama Mkubwa kwa chu-
ki; Mama alimsalimu sana, akasema kwa sauti
ndogo “Shikamoo Bibi.” Malkia hakuitikia,
HADITHI YA KASA 89
akapiga meno aksema “ Nimekuonya sana,
Mama Mkubwa, na sasa chagua. Wewe uende
zako au kichwa chako kiende zake.” Mama
Mkubwa hakukawia kuchagua, akapandisha
nguo akakimbia upesi. Malkia akamwambia
Elisi akasema ““ Twende tukaendelee kucheza.”
Elisi hakuthubutu kukataa, akamfuata Malkia,
wote wawili wakarudi kiwanjani.
Wageni wengine walikuwa wakipumzika ki-
vulini, lakini walipomwona Malkia waliondoka
mara wakaenda mahali pao, wakaendelea ku-
cheza kwa haraka, wakacheza muda wa saa
nzima, na Malkia hakukoma kugombana na
wenzake, na kuamuru fulani na fulani akatwe
kichwa, mpaka wageni wote wakaondolewa,
hakubaki mtu kiwanjani ila Mfalme na Malkia
na Elisi.
Malkia akawa amechoka sana, akawa ana-
tweta, akamwambia Elisi “Je, umemwona
Bwana Kasa Mliaji”? Elisi akajibu “ Siku-
mwona.” Malkia aksema “Vema. Twende
tukamwamkie! Tena ataweza kukuhadithia
habari za maisha yake.” Walipokuwa waki-
tembea pamoja Elisi akamsikia Mfalme Mzu-
nguwanne mbali kidogo, akiwaambia wageni
kuwa wamekwisha samehewa. Mtoto akafu-
rahi sana.
Malkia na Elisi wakazunguka pembe ya
njia, wakakutana na Mbuzi, alikuwa amelala
usingizi. Malkia akampiga Mbuzi akamwa-
90 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
mbia “Ondoka mvivu we, mpeleke mtoto
huyu kwa Bwana Kasa Mliaji, apate kusikia
hadithi yake. Mimi lazima nirudi. Wageni
wote watakatwa kichwa.” Akaenda zake, aka-
waacha Elisi na Mbuzi pamoja peke yao.
Elisi hakupenda sana sura ya Mbuzi yule,
lakini kutofautisha baina ya ukali wa Malkia
na ukali wa Mbuzi ilikuwa kazi ngumu.
Mbuzi alimtazama yule mtoto kwa makini
muda wa dakika chache halafu akageuka aka-
mtazama Malkia ambaye alikuwa akienda,
akasema “Kicheko kiko huko!” Elisi akau-
liza “ Kicheko gani?” Mbuzi akajibu akasema
“Malkia anadhani ya kuwa wageni wote wa-
tauawa, lakini sivyo, hawatakatwa kichwa,
hata mmoja! Twende!” Mbuzi akaondoka
Elisi akamfuata. Kabla hawajaenda mbali
wakamwona Kasa Mliaji; alikuwa amekaa peke
yake penye mwamba mkubwa, akilia sana
akitoa machozi. Bahari ilikuwa nyuma yake,
na bahari ile ilikuwa machozi yake aliyoyatoa
tangu zamani sana. Elisi akamwuliza Mbuzi
akasema “Je, amefiwa, ana huzuni gani?”
Mbuzi akajibu ““ Hana huzuni, wala hakufiwa,
kama ungemwuliza sababu ya msiba wake
asingeweza kujibu, ametumwa na Malkia ku-
jaza bahari watoto wake wapate kuogelea
ndani.”
Walipomkaribia Kasa Mliaji, Mbuzi akamsa-
limia akasema ““ Shikamoo Kasa Mliaji.” Kasa
HADITHI YA KASA 91
akafumbua macho na yakatoka machozi me-
ngi sana, yanayotosha kujaza ndoo mbili,
Elisi akarudi upesi asiingie maji. Kasa Mliaji
yA
;
AA
Aa WA
8 Y
| 4
Aa. , A
; i,
Dat:
aa
NI
uu
ui
B >
AI
O ai S -
Wa li ui
uu
Ua
UU ,
iliua
Wa. Sa
AA
wa
USI
Aua
Wa
WA Aa aa AA aa
NY
akasema kwa shida “ Marahaba. Wataka nini
rafiki yangu?” Mbuzi akajibu “ Tafadhali
mhadithie mtoto huyu habari za maisha yako.”
92 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Kasa Mliaji akatoa machozi zaidi akasema
“Vema. Kaeni. Tena msinitietie mpaka ni-
takapokuwa nimekwisha kusema.” Wote wa-
kakaa kitako, wakanyamaza muda wa dakika
chache. “Elisi akasema kimoyomoyo“ Asi-
ngeanza kusema angekuwa hawezi kuisha !”
Akangoja kwa uvumilivu. Kasa Mliaji aka-
vuta pumzi akasema:
“Hapo kale mimi na ndugu zangu tulikuwa
tumekaa baharini, sisi sote tumehudhuria shule.
Mwalimu. wetu alikuwa mzee.” Tulimwita
“fundi.” Elisi akauliza “Kwa nini ulimwita
“Fundi”?” Kasa akajibu akasema “ Kweli
wewe mpumbafu! Tumemwita “ FUNDI” maa-
na aliturundisha.” Mbuzi akasema “ Elisi
mwanangu, sikujua kuwa wewe u mjinga kama
hivi!” Elisi akaona aibu akanyamaza. Mbuzi
akamwambia Kasa akasema “Endelea Kaka,
sisi hatutaki kukaa hapa mpaka usiku.”. Kasa
Mliaji akaendelea akasema “ Sisi tulifundishwa
vizuri, tena tumekwenda kila siku chuoni.”
Elisi akamkatiza maneno akasema ““ Usiwe na
kiburi Bwana Kasa, mimi pia nakwenda kila
siku chuoni.” Kasa Mliaji akauliza “ Ume-
fundishwa lugha na ngoma?” Elisi akajibu
“Najifunza kuandika na kusoma.” Kasa
akaitikia ““ Kwetu sisi tulifundishwa kukandika
na kuchoma, halafu namna mbalimbali ya
Hesabu, ndizo: Haki, Kudanganya, Kubiidi-
sha, na Karamu.” Elisi akasema “ Maneno
HADITHI YA KASA 93
yako ni kama mafumbo! Habari za masomo
mengine?” Kasa Mliaji akasema “ Tumesoma
“Kiburi cha thamani” (Habari za zamani).”
Mbuzi akasema “Basi Kasa! Sasa tuambie
kidogo habari ya machezo ya shule.”
WA
SURA Y
NGOMA YA KAMBA
Kasa akamwambia Elisi akasema “ Wewe je,
umepata kukaa chini ya bahari?” Elisi aka-
jibu “ Sijapata kufika huko hata siku moja.”
Kasa akanena “Wawajua sana Kamba?”
Elisi akajibu akasema “ Mara moja niliwao-
nj !” Akajikatiza maneno upesi, akasema
“Siwajui.” Kasa akajibu “ Kwa hiyo huwezi
kujua furaha ya ngoma ya Kamba?” Elisi |
akauliza “ Ni ngoma ya namna gani?” Mbuzi
akaeleza akasema “Kwanza Kamba huenda
pwani, tena kushikiana mikono halafu wote
huogelea baharini na kurudi.” Elisi akataba-
samu akasema “ Ngoma nzuri sana!” Kasa
akaondoka akasema ““ Twende. Tutakuonye-
sha. Wanyama wawili wakasimama, wakashi-
kiana mikono wakaanza kuchezacheza katika
mchanga.” Wakamtisha sana £Elisi, mana
miguu yao ilikuwa mikubwa, tena walikuwa
hawachezi sawasawa. Ilikuwa hakuna ngoma
lakini Kasa Mliaji aliimba kwa upole na hu-
zuni; Hivi:
94
NGOMA YA KAMBA 95
Key E)
Il—:s£ | mm: ss AA EA AA WA
-Che-wa a-mwa-mbia Ko-a, Ta-fa - dha-li ka-sa
if aa: aa NAE BA KA USE US LE AA AA ae
mwen-do, Nyu-ma yan-gu Pa.pa mku-bwa, ni-a ya-ke si ya
i| Wa AA AA WA AA WA
pen - do, Ta - za-ma ka-ma Kam-ba wo-te
AA WA AUAWA AA
wa-me-tan-gu - lia, Wo-te wa-na-che-za pwa-ni, na n-
Aa Ua Wa WA UA AA
go-ma na-si - ki - a.Wa- we-zache-za 'we-za che-za
SA SA aa Ma WA Wawa KA SA waya ka AA WA SE Sa
'we-za che-za na - si, 'we-za che-za 'we-za che-za
WA NIA AA AAA JI
'we- za che-za Au AAA
Chewa amwambia Koa, “ Tafadhali kaza
— mwendo,
Nyuma yangu Papa mkubwa, nia yake si ya
pendo,
Tazama kama Kamba nio wametangulia,
Wote wanacheza pwani, na ngoma nasikia.
Waweza cheza 'weza cheza "weza cheza nasi.
Waweza cheza 'weza cheza 'weza cheza
nasi.
Tukitupwa baharini tutaogelea sana,”
Koa akatetemeka, akasema “ La! Hapana.
96 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Itakuwa mbali mno, tena haiwezekani,
Nenda peke yako Chewa, nitakungoja pwani.
Siwezi cheza "wezi cheza "wezi cheza nanyi
Siwezi cheza 'wezi cheza "wezi cheza nanyi.”
Samaki akasema “ Pana pwani mpya "ng "a-
mbo, Za.
Haya! Jipe moyo Koa, sisi sote -hatuja-
mbo;
Mbali na Afrika ni i.karibu Bara Hindi
Njoo, kacheza Koa, usipige we mapindi.
Waweza cheza "weza cheza "weza cheza nasi,
Waweza cheza 'weza cheza 'weza cheza
nasi.”
Walipokuwa wamekwisha kucheza Elisi aka-
washukuru akasema ““ Asanti sana rafiki zangu,
na sasa mmechoka, kaeni, na mimi nitawaha-
dithieni matokeo ya leo, tangu asubuhi. Jana
nilikuwa mtoto mwingine, kwa hiyo ni bora
nianze hadithi yangu tokea alfajiri leo.” Elisi
akasimulia matokeo yake, toka alipomfuata
Sungura Mweupe katika pango lake na mpaka
mwisho. Alipokuwa akihadithia jinsi alivyo-
mtiisha Mdudu kwa kusoma shairi, Kasa aka-
vuta pumzi akasema “Haya ni mambo ya
ajabu. Sasa jaribu tena kusoma mashairi.
Simama. Funga mikono nyuma. Useme shai-
NGOMA YA KAMBA 97
ri la “Ni sauti ya mvivu” na beti zifuatazo.”
Elisi akasema kimoyomoyo “ Viumbe hawa
wanitiishe! Ni kana kwamba niko chuoni!”
Akaondoka akafunga mikono akasoma:
KEY FF.
i|s:s:sim:m:m|fififi UA AA Ja :m:mjd:d:d |
Ni-na-si-ki-a sa-u-ti ya Kam-ba “ Ni-me-pi-kwa za-i-di, ta-
Ka kui WA WA WAWA SARA AA IA
-za-ma ma-gamba! Me-kun-du ka-bi-sa! 'si-ka-e mi-le-le, Ni-on-
it, AA ANAE AA MIA WA AI
-do-ke ka-ti-a su-ka-ri ny-we-le.” Ka-ti-ka m-cha-nga naam
EA AA AA AA AA
a-li-ji- ta-pa, Na A-ki-dha-ra-u ma - ta-ya ya Pa-pa. La-
1| WAA KA | ui YA LA Aa sh
-ki-ni wa-ka-ti wa. ma-ji ma - ku.--- 4
aa, IA IA — |
A-li-sa- ha-u u-ho-da-ri huu.
Ninasikia sauti ya Kamba
“ Nimepikwa zaidi, tazama magamba !
Mekundu kabisa! 'sikae milele, .
Niondoke katia sukari nywele.”
Katika mchanga naam alijitapa,
Na akidharau mataya ya Papa.
Lakini wakati wa maji makuu
Alisahau uhodari huu.
AIW—G
98 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Mbuzi akasema “ Nilipokuwa mtoto mimi nili-
jifunza kusoma maneno haya, kwa moyo, bali
wewe umeyasoma vibaya!” Elisi hakujibu,
akajikumbata akatazama bahari akafikiri sana
juu ya matendo yake, na usahaulivu wake.
Alikuwa amefadhaika.
Mbuzi akasema “ Endelea mwanangu, sasa
soma ubeti wa pili, maneno ya kwanza ndiyo
“Niliona, njiani.” Elisi hakuthubutu kuka-
taa. Akasoma hivi:
Niliona njiani, nilipongoja,
Chui na bundi wakila pamoja;
Mnyama 'kaguna, akala kwa pupa
Nyama, mchuzi na hata mifupa.
'Kamwambia Ndege "Umekula zamani,
Posho lako mwenzangu ndilo sahani;
Na kwa ukarimu nakupa kijiko;
Mali yangu ni kisu na uma. Na mwiko
Wangu si bundi. Kwa ghafula ali-
Mla Bundi na chumvi kwa meno makali.
Mbuzi akasema “Basi! Sisi hatuwezi ku-
fahamu hata neno moja, eleza.” Elisi aka-
jibu “ Siwezi kueleza.” Mbuzi akaondoka aka-
sema “Vema! Tucheze tena. Au labda uta-
penda kusikia wimbo wa Kasa Mliaji?” Kasa
akacheka akafikiri ya kuwa alikuwa amesi-
fiwa, Mbuzi akasema “Uimbe wimbo wa
NGOMA YA KAMBA 99
chakula Kaka.” Kasa Mliaji akavuta pumzi
akaimba:
Key C. ;
Il aria m|n-iru)rdl:-|driadm)m:-ire|
Twen-demwe-nza-ngu, s-a-sasaa Tu-le cha-ku-la, chaa
iIrdl-|nfin:s)s:timt | mz): Ishi lthi dirii ra |
ku-faa, I-ko na-fa-sina..wa-saa Tu-le cha-ku-u-la cha ku-
ila Jama | AITA
faa. — Chaku-faa, cha ku-faa, Tu-le cha-ku-la cha ku-faa.
Twende mwenzangu, sasa saa
Tule chakula, njoo kukaa,
Iko nafasi na wasaa
Kula chakula cha kufaa.
Cha kufaa, cha kufaa.
Kula chakula cha kufaa.
Sisi mwenzangu mashujaa,
Nasi twaona njaa. njaa.
Tusitandike kitambaa,
Tule chakula cha kufaa
Chakula kizuri cha kufaa
Tule chakula cha kufaa.
Mbuzi akapaza sauti akasema “ Tuitikie !”
Wote wakawa katika kuitikia wakiimba “ Tule
chakula cha kufaa.” waliposikia sauti mbali
kidogo, wakanyamaza wakasikiliza, halafu wa-
kamwona Askari mmoja ambaye alikuwa aki-
100 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
zitangaza amri za Mfalme Mzunguwanne. Ta-
ngazo lenyewe lilikuwa hili: “ NJooni Wote!
Hukumu Kuu Ni Tayari. NJooni. NJoo-
NI.” Mbuzi akamshika Elisi mkono akasema
“< Twende.”
Elisi na Mbuzi wakaenda pamoja kwa ha-
raka; lakini Kasa Mliaji hakuondoka, akaende-
lea kuimba na kutoa machozi.
Elisi alimsikia kwa mbali akiimba:
Chakula kizuri cha kufaa
Tule chakula cha kufaa.
SURA ZI
MWIZI WA MAANDAZI
WALIPOKUWA wamefika Bomani Elisi na Mbu-
zi walimwona Mfalme Mzunguwanne wa Kopa,
na Malkia Mzunguwapili wa Kopa, walikuwa
wamekaa penye viti vyao vya enzi, na mbele
yao mkutano mkubwa wa viumbe.
Mjanja Mzunguwatatu wa Kopa alikuwa
amefungwa kwa minyororo, naye alikuwa ame-
simama kati ya Askari wawili.
Sungura Mweupe alikuwa akisimama, penye
kiti cha enzi cha Mfalme, alikuwa akishika
tarumbeta na cheti.
101
102 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Katikati kabisa ya Boma palikuwa na meza,
na juu ya meza ilikuwa sahani kubwa yenye
maandazi.
Mfalme alikuwa mwamuzi, na alikuwa ame-
vaa kofia ya ujaji na juu ya kofia ile, amevaa
taji. Penye baraza ndogo wakakaa viumbe
thenashara, ambao walikuwa wakiandika ka-
tika vibao vyao kwa
bidii. Elisi akamwu-
liza Mbuzi akasema
“ Wanaandika nini ?”
Mbuzi akajibu “ Wa-
naandika majini yao
wasiyasahau.” Elisi
akasema “Wapu-
mbafu!”
Sungura Mweupe
akapiga sana taru-
mbeta, akatangaza
kwa sauti kuu aka.-
sema “ Nyamazeni
watu wote.”
Mfalme akavaa miwani akatazamatazama, apa-
te kuona ya kwamba wote walikuwa wametulia.
Elisi akavitazama vibao vya viumbe the-
nashara. Akacheka sana hawakujua hata
mmoja kuandika sawasawa. Elisi akasema
“kimoyomoyo “ Lakini hawa si binadamu. Nao-
na mjusi mmoja, panya mmoja, chura mmoja,
bata, kuku, kenge, komba na wengineo, si aja-
MWIZI WA MAANDAZI 103
bu kubwa ya kuwa hawajui kuandika.” Mfa-
Ime akapaza sauti akasema “Soma mashtaka.”
Sungura Mweupe akapiga tarumbeta mara tatu
akatangaza mashtaka, akasema “Malkia ali-
pika maandazi,
Na yalikuwa mazuri bila shaka,
Akaja mwizi alfajiri sana,
Na aliyaondoa kwa haraka.”
Mfalme akamwambia wathenashara “ Fiki-
rini sana.” Sungura Mweupe akapiga tena ta-
rumbeta akasema “ Mshahidi wa kwanza si-
mana.” Mshahidi wa kwanza alikuwa Mwu-
za Kofia. Akasimama, akakaribia kidogo kiti
cha enzi, nyuma yake wakaja Kobe na Komba.
Mwuza Kofia alikuwa akishika kikombe na
kipanda cha mkate, akawasujudia sana Mfalme
na Malkia, akasema ““ Niwieni radhi Bibi na
Bwana, lakini nilikuwa sijaisha chakula cha
jioni nilipoitwa nanyi.” Mfalme akasema
“ Shauri hili mbaya; kwa sababu gani hujaisha
kula? Ulianza kula lini?” Mwuza Kofia
akamtazama Kobe akasema “ Tulianza kula
chakula cha jioni terehe 14 Machi.” Kobe
akasema “La! Terehe 15 Machi.” Komba
akajibu “La! Ilikuwa 16 Machi.” Mfalme
akawaambia wathenashara “ Andikeni maneno
haya.” Viumbe wakaandika zile terehe tatu,
wahazihesabu wakaandika jumla kana kwamba
zilikuwa shilingi na senti.
104 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
Mfalme akamwambia Mwuza Kofia akasema
“Vua kofia yako.” Mwuza akajibu “Si kofia
yangu.” Mfalme akapiga uruzi akasema
“ Umeiiba ?” Akawaambia “ wathenashara
“ Andikeni.” Mwuza Kofia akaeleza kwa ha-
raka akasema “ Mimi mchuuzi, dukani mwa-
ngu ziko kofia nyingi sana, lakini si zangu za
kuvaa, naziuza tu.” Kwa ghafula Malkia aka-
vaa miwani, akamtazama sana Mwuza Kofia.
Huyo, alipoona kuwa Malkia alikuwa akimta.-
zama alitetemeka kwa hofu. Mfalme akasema
“ Toa ushahidi, wala usiogope ili nisikukate
kichwa sasa hivi.” Mwuza Kofia akazidi kute-
temeka na kubabaika, na katika kufadhaika
kwake alikimegua kikombe badala ya mkate.
Wakati ule ule Elisi aliona ajabu mwilini
mwake, baadaye alifahamu ya kwamba aliku-
wa akiongeza tena urefu; akawaza kuwa afa-
MWIZI WA MAANDAZI 105
dhali atoke Bomani, lakini halafu aliona ni
heri azidi kukaa, kama ikiwapo nafasi. Ko-
mba alikuwa amekaa karibu na Elisi akasema
“ Usinisukume mwanangu, sioni wasaa hata
wa kuvuta pumzi!” Elisi akajibu kwa unye-
nyekevu, akasema “Sina budi nikusukume,
sababu mimi naongezeka urefu.” Komba aka-
sema "Huna ruksa kuongeza urefu hapa.” .
Elisi akajibu “ Wewe unaongezeka pia.” Ko-
mba akaondoka akasema “ Najua sana, lakini
mimi nakua kwa pole pole, si kama wewe, kwa
haraka sana.” Komba akamwacha Elisi aka-
kaa mahali pengine. Komba na Elisi walipo-
kuwa wakisemezana, Malkia alikuwa anazidi
kumtazama Mwuza Kofia; akamwambia Askari
mmoja akasema ““ Niletee karatasi yenye ma-
jna ya waimbaji wa machezo ya terehe 13
Machi.” Aliposikia maneno haya Mwuza Ko-
fia akazidi mno kutetemeka mpaka viatu vyake
vikamtoka miguuni; Mfalme akasema “Toa
ushahidi mara moja.” Mwuza Kofia akajibu
akasema “ Uwe na rehema, mimi maskini, sina
akili.” Mfalme akapiga kofi akasema ““ Nenda
zako. Mjinga.” Mwuza Kofia akajibu “ Nipe
ruksa kwanza niishe kula chakula cha jioni.”
Alipokuwa akisema Malkia alikuwa akilitafuta
jina lake katika majina ya waimbaji. Mfalme
akasema kwa upole “ Mwuza Kofia we, nenda
zako.” Malkia akapaza sauti akasema ““ Mka-
te kichwa huko nje. Huyu ndiye aliye-
106 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
mwua Nafasi zamani kidogo.” Mwuza Kofia
hakukaa kuyasikia maneno haya, akaviacha
viatu Bomani, akakimbia kwa haraka ka-
ma umeme hata hakuweza kukamatwa na
Askari. Mfalme akaondoka akasema kwa sauti
kuu akinena “Mwita mshahidi wa pili.”
Mshahidi wa pili alikuwa Mpishi wa Mama
Mkubwa; alikuwa amechukua chupa ya pili
pili. Mfalme akamwambia “Toa ushahidi
wako.” Mpishi akajibu “Sitaki.” Sungura
Mweupe akamwambia Mfalme akasema “ La.-
zima umshurutishe aseme.” Mfalme akapiga
chafya akafunga mikono akamtazama sana
Mpishi akasema “Maandazi yalitengenezwa
kwa kitu gani?” Mpishi akajibu “ Yalitenge-
nezwa kwa pili pili.” Komba akaondoka aka.-
sema kwa sauti nyembamba “ Yalitengenezwa
kwa asali!” Malkia akanong'ona akasema
“ Akatwe kichwa yule Komba.” Wote waka.-
simama wakapiga mbio huko na huko, waka-
jaribu kumkamata Komba; ilikuwa ghasia ka-
bisa Bomani, lakini watu walishindwa. Komba
akapanda darini. Watu wote walikuwa wame-
choka, wakapumzika, na kumbe Mpishi naye
alikuwa ametoroka! Mfalme akasema “ Hai-
dhuru, mwite mshahidi mwingine.” Akamwa-
mbia Malkia kwa sauti ndogo akasema “' Tafa-
dhali mpenzi, wewe umwulize mshahidi huyu,
kichwa kinaniuma.”
Elisi akamtazama Sungura Mweupe, aliye-
MWIZI WA MAANDAZI 107
kuwa akitafuta jina la mshahidi wa tatu katika
cheti chake. Sungura Mweupe akasimama wi-
ma, akapiga sana tarumbeta mara tatu, aka-
sema kwa sauti kuu:
yi AA AI YA
TTA
SURA KZII
USHAHIDI WA ELISI
Eusi alishtuka sana kusikia jina lake likita-
jwa; lakini akasimama mara akaitikia “ Sa!”
Kwa sababu ya urefu wake mkubwa akaangu-
sha baraza ya wathenashara. Akafadhaika
sana akasema “ Niwieni radhi, niwieni ra-
108
USHAHIDI WA ELISI 109
dhi!” Akawasaidia wanyama kutengeneza tena
meza, na kutafuta vibao vyao na kalamu
zao.
Wote walipokuwa tayari Mfalme alimwuliza
Elisi akasema “ Unajua nini katika mambo
haya?” Elisi akajibu “ Sijui kitu.” Mfalme
akawaambia wathenashara akasema “ Andi-
keni ' Hajui kitu.” ”” Mfalme akamtazama Elisi
akafadhaika akatoa kitabu kidogo katika mfu-
ko akasoma, akakirudisha mfukoni, akamta-
zama tena Elisi akasema “Sikilizeni. Amri
ya arobaini na nne ya Boma hili ndiyo: “ Wote
wenye urefu kupita mnazi wafukuzwe Bomani.”
Wote wakamtazama €Elisi. Kijana akasema
“ Urefu wangu si wa kupita mnazi.” Mfalme
akajibu “ Ni kupita minazi miwili.” Elisi aka-
sema ““Sitaondoka. Hii si amri ya tangu za-
mani, umeizua sasa hivi katika haja yako ?”
Mfalme akajibu akasema “Ni amri ya kale
kupita zote kitabuni.” Elisi akacheka akasema
“Ikiwa hivyo, basi sharti iwe ya kwanza,
nawe ulikuwa ukitazama katika ukarasa wa
mwisho kitabuni.” Mfalme hakujibu, akafa-
dhaika kabisa, akaondoka katika kiti chake cha
enzi, akapaza sauti akasema “ Wakubwa wa
Baraza wakate shauri.” Malkia Mzunguwapili
akaondoka akamwelekeza kwa kidole Mjanja,
aliyekuwa mfungwa, akasema ““ Kwanza mkate
kichwa huyu.” Elisi akasema “ Hapana Ma.-
ma, Kwanza hukumu, halafu kuuawa, ikiwa
110 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU
amestahili.” Malkia akanong'ona akasema
“ Nyamaza we.” Elisi akajibu “Siwezi ku-
,
LA
ZA HY A , j , AL
Yu IA
SIRA ZA JUA
A ZIZINI
ka
?
j , Mi
MA :
AA la LI
nyamaza.” Malkia akasema Kwa sauti kali
akanena ““ Mkate kichwa Elisi !”
USHAHIDI WA ELISI 111
Elisi akawatazama Askari akatabasamu kwa-
ni hakutokea hata mtu mmoja wa kutimiza
amri za Malkia.
Elisi akajitazama, akaona kuwa urefu wake
ulikuwa kama zamani, kama mtoto wa nchi
wa Afrika. Akawatazama wenyeji wa Nchi
wa Ajabu akasema: “ Siwaogope ...
Ninyi Nyote Karata TU.
UA WA WA II AA BE
Kwa maneno haya karata zote zikaruka he-
wani zikampiga usoni Elisi.
Yeye akafumbua macho, akapiga yowe. ...
Alipokuwa macho akajiona, na kumbe aliku-
wa amelala chini ya mwembe! Dada yake
alikuwa amekaa karibu akimfukuzia mdudu
aliyekuwa ametambaa usoni, akasema “ Amka
Elisi mwanangu, umelala sana.” Elisi akao-
ndoka akajinyosha akasema “Kweli! Tena
nimeota sana.” Akamsimulia Dada habari za
ndoto yake.
Alipokwisha kuhadithia ndugu yake aka-
mwambia “Twende mwanangu, Mama ana-
twanga, chakula cha jioni ni karibu tayari, na
Dina anakulilia.”
Mwisho.
AA j "
Ka
v
Ka ya z.
KA
ya
Fara
aa
| Aa
3 aa
UA
ea YA au
ka Ai
UA ka
- aaa wi
na
WA
Na
ia
”, Bia aa
UE Ka,
Wa
ra