Skip to main content

Full text of "Elisi katika nchi ya ajabu"

See other formats


UA 
WAA WA 
ka wA pi Ui 


.. ia 
KA Aa 
UA 
- ,, KA 

YA yana Ww s 


Ka 


Ja 


NO YAWA 


- W IA 


ai y- kA 


" KRII 


TE 


ELISI KATIKA 
NCHI YA AJABU 


LEWIS CARROLL 


IMETAFSIRIWA NA 
ST Lo DE MALET 


(ALICE IN WONDERLAND: SWAHILI) 


LONDON 
THE SHELDON PRESS 
HOLY TRINITY CHURCH, MARYLEBONE ROAD, N.W.I. 


1967 


First published, 1940 


MADE IN GREAT BRITAIN 


YALIYOMO 


SURA UKURASA 
IJI. Pango LA SUNGURA - - - Sa 
II. KIidIimbwi CHA Machozi - - Sa 
III. Shindano La Kaka - - - - 28 
IV. NYUMBA YA SUNGURA - - 3 
V. MAsHAURI YA MDUDU - - -. 4 
VI. NGURUWE NA PILIPILI - 55 
VII. Karamu YA WENYE WAzIimu - - 66 
VIII. MachHeEzo YA MALIA - - - aa 
IK. Hadithi YA Kasa - - - Aa. 
K. Ngoma YA Kamba - - - - AA 
KI. Mwizi wA Maandazi - - - - 201 
ZII. Ushahidi WA Emsi - - - - 108 


ya - 
kai 


OMOYLIAY 
WAR KIA, kaa AA 
. 2 amua ka sa T 
, masia ano wami 
20007 maana aa amamdi VI 
; uiudii ay umeamza Mi .V 
- anuai aya aweanda JI. 
Swai IA waasadi TIC 
; " WAZA, AY usasa aa 


ki wa wiaarisi BRITAIK 


WAA ke 7 
n ; H y hi 5 . La 
| Y aa ya 


ZAMANI sana Mzungu mmoja 
Aliyependwa na watoto, 
Aliwahadithia kwa umoja 
Habari tamu sana za ndoto. 


Na mimi basi ninapenda 
Watoto Waafrika pia, 
Nimefikiri watapenda sana 
Kwa lugha yao nzuri kusikia 


Habari za mtoto yule 

Katika Nchi ya Ajabu. 

Tafsiri yake naam ni kazi kubwa 
Furaha yao kwangu ni thawabu. 


Njoni watoto na kaeni, 
Tutafurahi sana sisi ! 
Sikilizeni nitakaposoma 
Maneno na matendo ya Elisi. 


Ingawa mimi ni Mzungu 
Mniridhie; si mgeni, 

Mna bahati nami bila shaka. 
Sikilizeni sana, nyamazeni. 


E. V. St. L. C.-D. 


IK 


ajoma nyarsM BIGI IAA 
nioe za pwbasgovitA - 


siomu zwi sidiibadawilA 


moba 83 BABE urani hatali 


KA wai ai 


Ai adhisswW zai Wa 


Kia shaogataw 


situ kasa AA adgal swal r ; 


NTA vs0am as hadhi wa 


WANA BI UTE MAE 
#wdud kisi JA wasa EA mida 


kaa ha kamaa ani enu wa 


Aa ohasisor na asia? SW 


ayaseM ia atm swaga! 
Jasgm ia zsidhbhioM 
'nakada sii kasa waa, ujana 


aa Aa 


3 


Miji 
; HATI KUHUL, 
y Na aili ( 
/ Si wali KU, 


/ 


SURA 1 


PANGO LA SUNGURA 


Hapo kale palikuwa na mtoto mwanamke, jina 
lake Elisi. Wakati wa mwanzo wa hadithi hii 
Elisi alikuwa amekaa pamoja na dada yake 
katika kivuli cha mwembe; mara kwa mara 
alikuwa akitazama kitabu alichokuwa akisoma 
dada yake, lakini kilikuwa kitabu kisicho picha; 
Elisi akasema moyoni mwake, “Kitabu bila 
sanamu hakina faida ” akapiga mwayo akanena 
“Nataka niondoke nikachume maua, lakini 
nimechoka kabisa "! 

Hapo yule Elisi alishtuka kumwona sungura 


mweupe mwenye macho mekundu aliyekuwa 
11 


12 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


akikimbia; Elisi hakustaajabu hata alipomsikia 
yule sungura akisema, “ Ole wangu, ole wangu ! 
Nitachelewa kabisa.” 

(Halafu alikumbuka ya kwamba sungura 
hawasemi, lakini wakati wa hadithi hii haku- 
shangaa.) 

Sungura alitoa saa mfukoni mwake; mara 
Elisi akaondoka akasema “Lo! sungura ana 
kanzu na mfuko na saa! Naam hii ni ajabu 
kubwa!” Akapiga mbio, akamfuata shambani, 
na kwa bahati hakumpotea bali alimwona 
akiingia pangoni mwake. 

Elisi hakukaa kufikiri bali akaendelea ku- 
mfuata sungura. Pango liliendelea moja kwa 
moja kwa mwendo wa dakika kumi, kisha njia 
ikatelemka kwa ghafula kama inayoingia kisi- 
mani, na kwa sababu ya giza lililokuwako Elisi 
hakuliona lile shimo, akatumbukia; lakini haku- 
lia wala hakuogopa kwa kuwa hakuanguka 
kama jiwe, lakini alitelemka kama kwamba 
alikuwa akiruka hewani, alikuwa akianguka 
pole pole. 

Kwanza Elisi alijaribu kutazama chini, lakini 
hakuona kitu ila giza tupu, kisha akatazama 
kuta za kisima, na kumbe zilikuwa na makabati 
mengi na vibao vya kuwekea vitabu; huko na 
huko zimetundikwa ramani na sanamu. Katika 
kibao kimoja akaona chupa nyingi sana, aka- 
twaa moja akasoma katika cheti chake “ Ma- 
tunda ya Machungwa.” Halafu aliogopa kuia- 


PANGO LA SUNGURA 13 


ngusha akasema “Labda pana watu chini, 
nitawadhuru nikiiangusha chupa hii.” Lakini 
alijitahidi akairudisha katika kibao kingine. 

Elisi aliwaza, akasema moyoni ““ Basi, baada 
ya kuanguka namna hii sitaogopa tena kua- 
nguka, hata nikitoka juu ya dari ya nyumba, 
sitalia hata kidogo, jamaa zangu watafurahi 
na kufikiri kuwa mimi ni mtoto hodari sana !” 

Akatelemka! Akatelemka! Akatelemka ! 
Akasema “ Bila shaka nimetelemka maili nyi- 
ngi sana, labda chini ya kisima hiki ni kati kati 
kabisa ya dunia! Au labda hakuna mwisho, 
na kisima hiki kitatokea upande wa pili wa 
dunia; je, watu wa upande huo wanafanana na 
nini? Nikifika huko nitawasujudia, nitawa- 
uliza habari za nchi yao.” Elisi akakumbuka 
ya kwamba Mwalimu wa chuoni alipata kufu- 
ndisha ya kuwa nchi ya Amerika iko upande 
wa pili wa dunia, akasema ““ Labda nakwenda 
Amerika !” 

Akashuka! Akashuka! Akashuka! Elisi 
akaanza tena kujizungumza akasema “ Dina 
atanililia leo jioni!” ( Dina” ni jina la paka 
wa Elisi.) “Ewe Dina laiti ungekuwa nami 
kwa wakati huu! Lakini hewani hakuna pa.- 
nya! Labda ungependa kukamata popo kama 
ungekuwa hapa! Je, paka hula popo? Si- 
jui.” Macho yake Elisi yalikuwa mazito kwa 
usingizi, akaweweseka akawa kila mara ana- 
sema “Paka hula popo”? “Paka hula po 


14 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


po” na mara kwa mara “Popo hula paka”? 
“Haidhuru nikisema paka hula popo au niki- 
sema popo hula paka, mamoja kwangu, maana 
mimi sijui kuyajibu maswali haya.” 

Elisi akajiona amelala usingizi, akaota ya 
kwamba alikuwa akitembea pamoja na Dina, 
akamshika mkono akamwuliza sana akisema 
“Sasa Dina niambie kweli, unapenda kula 
popo ?” 

Kwa ghafula Elisi akajiona ameamka tena, 
naye amefika mwisho wa kisima; pana majani 
mengi sana makavu; na hapa kukawa mwisho 
wa kuanguka kwake. Elisi hakuumiwa hata 
kidogo, akaondoka mara moja akainua macho 
yake, lakini juu hakuona ila giza tu, na mbele 
yake pango liliendelea; na tahamaki akamwona 
yule sungura mweupe akitangulia kwa haraka. 
Elisi akajipa moyo, akapiga mbio sana apate 
kumkaribia, lakini alipokuwa karibu kabisa 
sungura akazunguka pembe ya njia, Elisi asi- 
mwone tena, bali alimsikia mbali kidogo aki- 
sema ““ Ole wa masikio yangu na mkia wangu ! 
nitakuwa nimechelewa sana ” Elisi akazunguka 
pembe lakini sungura akawa ametoweka kabisa. 

Sasa yule mtoto akajiona yumo katika chu- 
mba kikubwa, chembamba, chenye dari fupi; 
kiliangazwa na taa zilizotundikwa darini, na 
katika kuta za chumba ilikuwamo milango 
mingi sana. Elisi akajaribu kufungua kila 
mlango, lakini yote ilikuwa imefungwa. 


PANGO LA SUNGURA 15 


Kati kati ya chumba akaona meza ndogo ya 
kioo yenye miguu mitatu, na juu yake upo 
ufunguo wa dhahabu mdogo sana. Elisi aka- 
furahi akasema “Sasa naweza kufungua mi- 
lango,” akajaribu sana asiweze, ufunguo mdo- 
go na tundu kubwa, akakata tamaa. Mwisho 
akaona mlango mdogo kabisa ambao hajapata 
kuuona, akainama akatia ufunguo katika tundu, 


na tazama ukafaa! UElisi akafungua ule mla- 
ngo mdogo, akapiga magoti akachungulia nda- 
ni. Kulikuwa na pango kama la panya, na 
mwisho wa pango kulikuwa bustani nzuri ka- 
bisa, akatamani sana kutoka chumbani mle 
alimokuwamo kwenye giza, ili afike kwenye 
jua na maua na chemchemi bustanini; lakini 
hakuweza hata kupitisha kichwa pangoni, aka- 


16 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


sema “Kama ningeweza kujipunguza kuwa 
nyembamba mfano wa bomba ya baisikeli 
ningeweza kuingia bustanini.” (Wafahamu 
Msomaji, ya kuwa jinsi mambo mengi ya ajabu 
yalivyomtokea hata Elisi alidhani kwamba 
kwake yeye kila neno liliweza kutokea.) 

Elisi akarudi mezani, na sasa akaona chupa 
ndogo juu yake, na shingoni limefungwa kara.- 
tasi kwa uzi, na juu ya karatasi imeandikwa 


“Uninywe.” Elisi alikuwa mtoto mwenye 
akili, akasema, “Labda ni sumu” kwanza 
nitafute neno “ “sumu” ”; akatafuta sana lakini 


hakuliona, akafungua chupa akaionja kidogo 
dawa iliyokuwamo ndani yake; ladha yake 
tamu kama embe au nanasi au asali, akainywa 
upesi. 

Mara Elisi alipokwisha kunywa dawa aka- 
jiona kuwa amepungua kimo, akafumba macho 
akaogopa kidogo, akasema “ Labda nitatoweka 
kabisa kama nuru ya mshumaa inapozimwa.” 
Alipokwisha pungua alifumbua macho, akajita- 
zama sana, urefu wake ulikuwa kama kuku; 
akasema “ Nitaweza kuingia bustanini sasa 
hivi” Lakini, maskini Elisi, alishindwa kabisa, 
kwa kuwa amesahau ule ufunguo mdogo wa 
dhahabu, aliuacha mezani; yeye sasa mdogo, 
hakuweza kufika mezani, alijaribu sana ku- 
panda mguu wa meza bali alishindwa kwa ute- 
lezi wake, na alipochoka kwa kujitahidi alikaa 
kitako akalia sana; badaye akajilaumu aka- 


PANGO LA SUNGURA 17 


sema “ Basi, tulia sasa, haina faida katika kulia, 
nakuonya unyamaze upesi.” Elisi ilikuwa de- 
sturi yake kujipa mashauri mazuri, ingawa 
mara nyingi hakuyafuata. Mtoto akazidi ku- 
jiambia “Faida gani kusema peke yangu”? 
Mara Elisi akaona kisanduku chini ya meza, 
ndani yake ulikuwamo mkate mdogo, na ka.- 


tika ule mkate yameandikwa maneno wazi 
wazi, kwa herufi zilizofanyizwa kwa chembe za 
mtama: “UniLe.” Elisi akasema “Ni heri 
niule, halafu nitaona matokeo yake yataka- 
vyokuwa; labda utaniongeza urefu tena kama 
bomba ya baisikeli, nipate kutwaa ufunguo, na 


ukinipunguza zaidi nitaweza kutambaa chini 
2 


AIW—B 


18 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


ya mlango kama mdudu, niingie bustanini.” 
Akala kidogo ule mkate, akaweka mkono 
kichwani apate kuona wakati akipanda au aki- 
shuka, akashtuka kuona urefu wake ule ule, 
akacheka akasema “Kweli mkate si dawa ya 
kugeuza mwili, lakini hapa mahali pa ajabu, 
sina haja ya kushangaa nikigeuzwa na mkate.” 
Akazidi kula hata akaumaliza. 


SURA II 


KIDIMBWI CHA 
MACHOZI 


Euisi akapaza sauti Aa 
akasema “Hapa 3 uu 
mambo yote yana- 
zidi kunishangaza, 
kumbe najiongeza 
urefu kama bomba 
ya baisikeli kubwa 
kupita zote”! Aka- 
inamisha macho 
akajaribu  kuvita- 
zama vidole vyake 
vya miguu, akavi- 
ona viko mbali sana, 
akasema “Kwa 
herini miguu, labda 
hatutaonana tena, 
nitawapeni zawadi 
wakati wa siku- 
kuu.” Akacheka akasema “Sasa nitapuuza 
kila neno"! 

Elisi akajipiga kichwa darini, urefu wake 
ulikuwa kama wa watu wawili wakubwa, aka- 

19 


ya 


20 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


twaa ule ufunguo mdogo wa dhahabu, akaenda 
upesi kwenye mlango wa bustani. Maskini 
Elisi! Baada ya kujitahidi sana aliweza kuu- 
karibia mlango, akalala kifudifudi akatazama 
kwa jicho moja bustanini, lakini kuingia haku- 
weza; akakata tamaa kabisa, akakaa kitako 
akalia sana, akajilaumu tena akasema ““ Ni aibu 
kabisa kulia namna hii, wewe mtoto mkubwa 
sasa, nawe walia kama mtoto mchanga, tulia 
mara moja” Walakini akazidi kulia akatoa 
machozi mengi sana, hata yakatosha kujaza 
mitungi ishirini, akawa amekaa katika kidi- 
mbwi cha maji. 

Badaye kidogo Elisi alisikia mashindo ya 
miguu midogo njiani, mbali kidogo, akajifuta 
machozi apate kumwona yu nani ajaye. Ku- 
mbe ni Sungura Mweupe aliyekuwa akirudi, 
amevaa nguo za umalidadi wa Kizungu, ame- 
shika mkononi mwake upepeo na kofia, anapiga 
mbio akinungunika na kusema “ Atakasirika 
sana nikimkawilisha.” Elisi, kwa sababu ya 
hali yake mbaya, na katika kukata tamaa 
kwake alikuwa tayari kumwomba msaada mtu 
ye yote, basi alipomkaribia Sungura alisema 
kwa hofu na kwa sauti ndogo “ Shikamoo 
Bwana Sungura, Tafadhali .. .” Sungura 
akashtuka sana hata akaangusha vitu alivyo- 
kuwa navyo, akakimbia upesi gizani. 

Mle chumbani alimokuwamo €Elisi mlikuwa 
na joto kidogo, kwa hiyo alitwaa upepeo wa 


KIDIMBWI CHA MACHOZI 21 


sungura, aliouangusha akaanza kujipepea, aka-- 
jizungumza tena akisema “ Ole wangu, hii ni 
siku ya ajabu! Jana mambo yalikuwa sawa 


Aaa 
— AA aa 
PI 
HU! 
aa ——- za 
Ja ka — Zizi 
(AT ANITA my j 
| WUE NI zi 
HABA KAA niga ha 
if z : a > v ; . 5 ni 
Btihi KAABA NI AA A 
AA ataiti ja L 
WI 
ja Ki i Di 3 ! di 
UPANA aha ea ! ji 
i UA | 
YA NA ! 
ii 


sawa, labda niligeuzwa usiku, nadhani ya ku- 
wa nimesahau yote niliyofundishwa chuoni.” 
Akajaribu kusoma kwa moyo mashairi aliyo- 
jifunza zamani kidogo, akanena: 


22 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Kwa nguvu sana Mamba a— 
naling'arisha kila gamba 
Katika mto akang'aa 

Yu safi sana yule Mamba. 


Na Mamba alichekelea, 
Akatandika kucha zake. 
Samaki walipotembea 
Wakahesabu meno yake. 


KEY G. 
MA IAA AI KATA 
Kwa ngu-vu sa-na Mam-ba a-na-ling'-a-ri-sha ki-la 


il mimi:s WAN AA AA AA Kaa 
gam-ba Ka -ti-ka m-to a - kang'-aa Yu 


AA KA KA AI AAA AA WAA 
sa-fi sama yu - le Mam -ba. Na 


1| AYA WAA AA AA aa AA AA KAA 
Mam<-ba a-li-che-ke- le-a, A-ka-tan-di-ka ku-cha 


| m:imjo:s | Le: tape: ta | mf:mrim:s, | 
za-ke. Sa - ma-ki wa-—li - po-tem-be-a Wa- 


| 1,8,:1,4,14:r | dr:mf|s:s | 1.8: £f.m | r.m:f.s | 
ka-he-sa-.bume-no ya-—ke..., Sa - ma-ki wa-li- 


(II meunzides AA AA AI 
po-tem-be-a Wa - ka-he-sa-bu me-no  ya-ke. 


- 


KIDIMBWI CHA MACHOZI 23 


Kwa bahati njema wakati ule akaona ki- 
chwa na mkono, akashangaa kuona ya kuwa 
amevaa ile kofia ndogo ya Sungura, akasema 
“Nawezaje kuivaa kofia ndogo namna hii, 
ikiwa kimo changu ni kama kile cha watu wa- 
wili? Labda sasa nimepungua tena.” Akao- 
ndoka akaenda mezani apate kujipima penye 
mguu wake; na kumbe, urefu wake ulikuwa 
kama wa mtungi, tena alikuwa anazidi kupu- 


ngua; akatafuta sababu ya kupungua kwake, 
akaona ya kuwa ilikuwa ule upepeo wa Sungura 
alioushika, akauangusha upesi asizidi kupu- 
ngua, akasema “Bahati kubwa! Kama ni- 
ngaliendelea kuushika ningalitoweka kabisa.” 
Elisi akaogopa kidogo, lakini alifurahi ya 
kuwa maisha yake hayajaisha bado, akasema 
“ Vema, sasa nitakwenda bustanini.” Akapiga 
mbio akafika mlangoni, lakini umefungwa ka.- 
ma zamani, na ufunguo upo vile vile mezani. 


A 


24 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Akalia sana akasema ““ Mambo yamezidi kuwa 
mabaya tena ni mara ya kwanza katika maisha 
yangu kuwa mdogo.” Aliposema maneno ha- 
ya miguu yake ikateleza akaanguka akatumbu- 
kia katika maji ya chumvi mpaka kidevuni; 
kwanza alidhani ya kuwa ameanguka baharini, 
kisha akafahamu ya kwamba yale maji ya 
chumvi ndiyo kile kidimbwi cha machozi yali- 
yomtoka alipokuwa na urefu kama watu wawili, 
akasema “Adabu ya kulia ndio kufa ndani 
ya machozi !” 

Kwa ghafula Elisi akasikia kitu kinaruka 
majini, akaogelea karibu kidogo apate kuki- 
ona, kwanza alidhani ni kiboko, kisha akaku- 
mbuka udogo wake akaona ya kwamba ni 
panya tu, aliyeanguka majini kama yeye mwe- 
nyewe. 

Elisi akasema kimoyomoyo akinena “ Labda 
inafaa kusema naye, ikiwa sungura wanaweza 
kusema katika nchi hii, bila shaka panya nao 
wanaweza; Hebu! Nijaribu!” Akapaza sauti 
akasema ““ Ewe Panya, nchi kavu iko wapi? 
Nimechoka kuogelea.” Panya akamtazama 
mtoto kwa makini, akakonyeza jicho, bali ha- 
kujibu. Elisi akasema moyoni “ Labda hasi- 
kii Kiswahili, nitasema Kiingereza.” Hakujua 
ila maneno machache ya Kiingereza, akasema 
kwa sauti kuu “ Where is my cat ?” (Maneno 
haya ndiyo ya kwanza katika kitabu chake 
cha kujifunza Kiingereza, tafsiri yake “ Yuko 


KIDIMBWI CHA MACHOZI 25 


wapi paka wangu ?”) Aliposikia maneno haya 
panya akaruka akatoka katika maji, akitete- 
meka kwa hofu; Elisi akasema “ Niwie radhi 
Panya, nilisahau kabisa ya kuwa hupendi pa- 
ka.” Panya akajibu kwa sauti nyembamba 
akasema ““ Kweli sipendi paka; je, wewe unge- 
wapenda paka kama ungekuwa kama mimi ?” 
Elisi akajibu akasema ““ Ningekuwa kama we- 
we labda nisingewapenda, lakini nadhani unga- 
. Jimpenda paka wangu, kwani ni mpole kabisa, 
jina lake Dina. Kazi yake ni kukaa kitako, 
kutoa ngurumo na kujiramba, napenda sana 
kumbembeleza naye ni fundi kabisa wa kuka- 
mata panya. ... Niwie radhi! Nimesahau.” 
Panya alikuwa akitetemeka 'sana, Elisi aka- 
mwonea hurumu akasema “ Tusiendelee ku- 
zungumza juu ya paka.” Panya akajibu aka- 
sema ““ Wasema Sisi tusiseme habari za paka; 
kwangu mimi simtaji hata jina lake, watu wa 
kabila langu huchukia kabisa paka, wanyama 
wabaya, hawana adabu, wakali, nisisikie 
tena hata jina hilo!” Elisi akajibu akasema 
“Vema, sitalitaja tena. Tuzungumze mambo 
menging, je, wapenda mbwa?” Panya haku- 
jibu, Elisi akaendelea kusema “ Pana mbwa 
mzuri sana anayekaa penye nyumba yetu, 
nitapenda kukuonyesha, ana macho makubwa 
mazuri sana, rangi yake kama udongo, na 
kama ukitupa mpira anaudaka, bwana. wa 
mbwa 'huyo anamsifu sana, asema ni mbwa 


26 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


wa kufaa sana kunaanza panya wote nyu- 
mbani.” 

Panya akaogelea upesi kumwacha Elisi, na 
kwa hiyo naye akatambua ya kuwa amemwu- 
dhi, akamwita akasema “ Ee Panya mpenzi 
rudi! Natoa ahadi ya kuwa siwezi kusimulia 
tena habari za paka wala mbwa.” 


ukuaji 


L 
za 


AI 
i 
f 
' 


ai. 
Tai 3 


AAA 


AI 


Aliposikia haya panya akarudi pole pole, 
akasema kwa sauti ndogo ““ Twende nchi kavu 
kisha nitakuhadithia habari za maisha yangu, 
upate kufahamu jinsi ninavyowachukia paka 
na mbwa.” 

Bila shaka wakati wa kutoka kidimbwini 
ulikuwa umefika, maana wanyama wengi wa- 


KIDIMBWI CHA MACHOZI 27 


mekusanyika majini, waliotumbukia humo ka- 
ma Elisi na Panya. 

Palikuwa na bata mmoja, Doda mmoja, 
lauri mmoja, Tai mmoja na wanyama wengine 
wa ajabu. 

— Elisi akatangulia, wakaogelea wote mpaka 
nchi kavu. 


SURA III 
SHINDANO LA KAKA 


Lilikuwa kundi la ajabu sana lililokuwapo 
pwani; ndege wote manyoya yao yalikuwa 
yamelowa, na maji yalikuwa yanatiririka ka- 
tika ngozi za wanyama; wote wamenuna kwa 
hali yao mbaya; wote wakahitaji kukauka, 
kila mmoja akapiga kelele kupita wenzake ka- 
tika kutoa mashauri ya njia za kuweza kukau- 
ka. Elisi akafanya kelele kupita wote, ha- 
swa alishindana kwa maneno na yule Lauri, 
mpaka mnyama huyu akakasirika kabisa aka- 
kataa kusema, ila maneno yale, aliyoyasema 
mara nyingi sana, ndiyo: “Mimi nimekaa du- 
niani miaka mingi kupita wewe, kwa hiyo mimi 
najua zaidi.” Elisi akamwuliza umri wake, 
lakini akakataa kabisa kumwambia. 

Panya alichoka akamwuliza Elisi akasema 
“ Waendeleaje mwanangu? Umekwisha kau- 
ka?” Elisi akajibu “Sijakauka hata kidogo.” 
Doda akapaza sauti akasema ““ Kwa hiyo nawaa- 
muru wote wafikiri shauri jingine la kufaa, kwa- 
ngu mimi shauri ni kupiga “ Shindanola Kaka.” 
Elisi akauliza akasema “Shindano la Kaka ni 
nini?” Doda akasema “Namna ilyo bora ya 


kueleza kitu ni kukitenda.” 
28 


SHINDANO LA KAKA 29 


Kwanza Doda akapiga mstari chini kwa dua- 
ra mkubwa, hii ndiyo njia ya kutembelea, 
kisha wote wakasimama mstarini, huko na 
huko, wakakimbia wanapopenda, kwa hiyo 
ilikuwa si rahisi kujua kikomo cha shindano 
hilo; walakini wote walipiga mbio kwa nusu 
saa, na walipokuwa wamekwisha kukauka Do- 
da akasema kwa sauti kuu “ Shindano lime- 
kwisha.” Wote wakatulia wakamsogelea Doda 
wakitweta, wakamwuliza wakisema ““ Tuambie 
Doda, nani aliyeshinda ?” Doda akakaa aka- 
fikiri saaaaaana, kidole kinywani, na wote wa- 
likuwa wamengoja, mwisho Doda akapiga ke- 
lele kwa furaha akasema ““ Wote wameshinda, 
wote watapata tuzo.” Kwa sauti moja wa- 
nyama wakauliza wakasema “ Nani atakaye- 
toatuzo”? Doda akajibu “ Huyu.” Akamwe- 
lekezea kidole Elisi, makutano ukamgeukia 
Elisi wakasema “Tuzo! Tuzo! Twataka 
tuzo.” Elisi akaogopa kidogo lakini aliku- 
mbuka ya kuwa zamani kidogo alifunga senti 
chache za moja moja katika pembe ya shiti 
yake, akaifungua fundo upesi, akaona ya 
kwamba kwa bahati alikuwa na senti za kuto- 
sha kumpa kila mtu moja; akazitoa kwa uta- 
ratibu, wote wakapendezwa sana. Panya aka.- 
mwambia Elisi “ Wewe pia, lazima upate tuzo.” 
Doda akaitikia ““ Ndio, lazima upate tuzo vile 
vile; je, unazo nyingine fundoni mwa kanga ”? 
Elisi akajibu “Sina, ila pete tu”! Doda aka.- 


30 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


nena “Itafaa,nipe.” Elisi akampa ndege ile pete, 
huyu akamrudishia kwa heshima kuu akasema 
“ Pete hii iwe na kibali kwa Mama.” Na alipo- 


kwisha kusema maneno haya wote wakapiga 


Ni. 
4 WA 
Ww : AI UA 
Na ndi Wa f, Yaa v 
kaa AI v 


“ wa WA Na . 
NI pa wako v 
r zi Ka 


pa, 


ka 


AI 
NG 
by — 


Y, AI 
za . y WA 
WIN I Ia Aa WA z 
LIPIA > 
wa AH zi 
Nu 
.. WA 


makelele ya kushangilia. Elisi akafikiri kuwa 
matendo haya hayana maana, lakini akawasa- 
limu wanyama akapokea pete, akaivaa kidolini. 

Elisi akamwita Panya akamwambia kwa 
sauti ndogo akasema ““ Ewe Panya zamani ki- 


SHINDANO LA KAKA 31 


dogo uliahidi kunisimulia hadithi ya maisha 
yako, na kwa nini wachukia sana wanyama 
wa namna fulani (Siyataja majina yao),” Panya 
akamjibu Elisi kwa huzuni akasema ““ Hadithi 
yangu ndefu sana. Katika nchi yetu desturi 
ni hii: Fulani akiwa na mkia mrefu, husemwa 


ana bahati ya kuishi siku nyingi, tena ana ruksa 
kusimulia hadithi ya maneno mengi; mkia wa 
fulani ukiwa mfupi, maisha yake mafupi pia, 
na hadithi yake lazima iwe na maneno macha- 
che tu. Katika nchi yangu “ MKIA ' na ' HA- 
DITHI ' ni neno moja, nikisema '“ Mkia wangu 
mrefu ' au ' Hadithi yangu ndefu ” maana ya.- 
ke sawa sawa; na mkia wangu ni mrefu 
mno. “Hadithi” au “Mkia' wangu ni hii””:— 


32 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


“Mama yangu 
WA UA USAIOA 
Mbwa wali -- 


kuwa rafiki. 
Mbwa akamshtaki 


mama yangu. A- 
kasema, wewe 
umeiba cha-' 
AA AUA 
Bwana wa- 


ngu wewe mwivi 


nitakushtaki kweli 
serikalini -- 
Mwamuzi aka- 
sema “Kweli 
Panya wewe mtu 
mbaya sana, wa- 
stahili kuuawa 
Mbwa na paka 
wamepewa ruk- 
sa kukurarua, 
Mbwa na Paka 
wakafurahi 
wakamkamat 
a mama 
yangu, wa- 
kamwua u- 
pesi, tena 
wakawa- 
kamata 
ndugu za- 
ngu wote, 


mimi nilikaa peke 
yangu, nikihuzunika saaaana.” 


SHINDANO LA KAKA 33 


Panya akajikatiza maneno akamwambia Elisi 
akasema “ Husikilizi! Unafikiri nini?” Elisi 
akajibu kwa unyenyekevu akasema “ Sifikiri 
kitu Panya, nasikitika sana, tafadhali uni- 
samehe.” Lakini yule mnyama alikasirika ka- 
bisa akaondoka, Elisi na wanyama wengine 
wote pia wakamwita, lakini alikataa kurudi, 
akazidi kukaza mwendo. 

Elisi alisema “ Dina angekuwapo hapa ange- 
mrudisha upesi Panya.” Lauri akauliza “ Dina 
nani”? WElisi akajibu kwa furaha akesema 
“Dina ni paka wangu, ni hodari kabisa kuka.- 
mata panya, tena anaweza kukamata ndege, 
ni paka mwenye akili nyingi.” 

Maneno yake Elisi yaliwatia hofu wale we- 
nzake ndege; wengi wakaondoka wakaenda 
mara moja bila kuaga, wengine wakasema 
“Baridi kali sana, lazima turudi nyumbani.” 
Hawakumtaka Elisi awasindikize. Kwa saba- 
bu mbali mbali wote wakaenda zao; Elisi 
akabaki peke yake kabisa, akasema kwa huzuni 
“Wasa nasikitika ya kuwa nilisema habari za 
Dina, imebainikia ya kwamba wenyeji wa nchi 
hii wanamchukia, ingawa ni paka mwema kupita 
wote. Ee Dina nina haja nawe sasa, je, sitakuona 
tena?” Elisi akatoa machozi, maana amekuwa 
mpweke, mwenye huzuni, walakini baadaye 
kidogo alisikia tena mashindo ya miguu midogo 
njiani, akatulia akidhani kuwa ilikuwa Panya 


aliyekuwa anarudi. Kumbe halikuwa yeye! 
; : - 


AIW—C 


SURA IV 
NYUMBA YA SUNGURA 


ALIKUWA Sungura Mweupe aliyekuwa akirudi, 
akitafuta huko na huko alimokuwa akienda, 
kana kwamba amepotelewa na kitu, akanu- 
ng'unika akisema “Mama Mkubwa! Mama 
Mkubwa! Maskini miguu yangu, masikio na 
midomo yangu! Bila shaka nitakatwa kichwa! 
Nimeviangusha wapi?” Mara Elisi akabahati- 
sha ya kuwa alikuwa anatafuta upepeo na 
kofia yake, aliyoangusha zamani kidogo; aka- 
msaidia katika kutafuta kwake, bali hakuviona. 
Mahali pamebadilika tangu kuogelea kwake 
Elisi kidimbwini, na kile chumba kirefu chenye 
meza ya kioo, na mlango mdogo kimetoweka 
kabisa. 

Kitambo kidogo Sungura akamwona Elisi, 
ambaye alikuwa akitafutatafuta, akamwita 
kwa hasira akisema ““ Ewe Meriana, wafanyaje 
hapa? Rudi nyumbani upesi, kaniletee upe- 
peo na kofia nyingine.” 

Elisi akaogopa sana akakimbia kwa hima 
njia aliyoielekeza Sungura, hakukaa wala ha- 
kumwonyesha Sungura kosa lake, na alipo- 
kuwa akitembea alisema moyoni “ Amenidhani 


mimi ni yaya, atashtuka atakapoona kuwa si- 
3 


NYUMBA YA SUNGURA 35 


ye, lakini afadhali nimletee upepeo na kofia.” 
Kabla hajamaliza maneno akaona nyumba 
ndogo safi, na mlangoni imeandikwa na herufi 
za shaba: “ BWANA S. MWEUPE.” 

Elisi hakupiga hodi, akaingia nyumbani aka- 
panda ngazi kwa hofu, akadhani ya kuwa ata- 
kutana na huyu yaya mwenyewe, atupwe nje 
kabla hajapata upepeo na kofia ya Sungura. 
Elisi alicheka alipofikiri ya kwamba ametumwa 
na sungura, akasema “ Nitakaporudi kwetu 
labda Dina atanituma pia.” Akaingia ndani 
ya chumba kidogo, safi kabisa, chenye dirisha 
na meza; na mezani akaona upepeo na kofia 
ndogo. 

Elisi akafurahi, basi alipokuwa katika kuvi- 
twaa, aliona chupa mezani, na ingawa haina 
cheti cha maelezo kama cha ile ya kwanza, au 
neno “ uninywe ” aliinywa dawa iliyomo ndani, 
akasema ““ Sasa nitapata mambo gani?” Maa- 
na Elisi alifahamu siku zile kuwa anywapo 
cho chote hufikiwa na mambo mbali mbali. 
Elisi akasema “ Labda dawa hii itaniongeza 
urefu, nimechoka kuwa mbilikimo namna hii!” 
Dawa ilimfaa upesi kabisa, na kabla hajaweza 
kutoka chumbani alijidunda kichwa darini, 
akairudisha chupa mezani akasikitika ya kuwa 
amekunywa nyingi, sababu alikuwa hajaacha 
kukua, akakaa chini akanyosha mkono diri- 
shani, na mguu katika bomba la moshi, apate 
kuwa na nafasi, akasema ““ Nitokeje sasa ?” 


36 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Kwa bahati wakati ule ule nguvu ya dawa 
ilipungua, lakini alikuwa hana wasaa hata wa 
kugeuka, amebanwa kabisa, hakujua njia ya 
kuokoka, akasema moyoni “ Kwetu maisha 
yangu mazuri kupita ya hapa, huko siku- 
punguka wala sikuongezeka kila nilapo au 
niywapo, tena situmwi na sungura wala pa- 


AA AAA AA 


yi 
1 
“ 
j | 
j! 
i! 
i 
hi 
v 
Ba 
i 
iJ 
A 
YA 
“ 


AS RI 
Ny 


nya. Sasa nasikitika ya kuwa nimemfuata 
sungura pangoni, nasikitika kama sisikitiki. 
Zamani nilisoma hadithi za namna hii, siku- 
dhani ya kuwa mimi nitakuwa mtu wa hadithi. 
Ni heri kiandikwe kitabu juu ya habari hizi, 
au labda nitakiandika mwenyewe nitakapo- 
kuwa mtu mzima.” Kabla hajamaliza kusema 
akasikia sauti ya Sungura nje, aliyekuwa aki- 


NYUMBA YA SUNGURA 37 
mwita yaya, akisema “ Ewe Meriana, niletee 
kofia upesi!” Elisi akasikia mashindo ya mi- 
guu midogo ngazini, akatetemeka kwa hofu, 


akasahau ya kwamba yeye ni mkubwa kabisa 
kuliko Sungura na wenzake, wala hakuna 
haja ya kuogopa. Sungura Mweupe akafika 
mlangoni akajaribu kuufungua, bali alishi- 


38 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


ndwa, maana Elisi alikuwa ameuzuia kwa 
kisigino, mnyama akasema ““ Vema, nitaingia 
dirishani.” Elisi akajibu moyoni akasema 
“ Haingii, nitamzuia.” Akangoja mpaka aka- 
msikia nje, chini ya dirisha, akatoa mkono 
kwa kumdaka, lakini alimkosa, akasikia ki- 
shindo kama cha kuanguka kitu penye mitungi 
mingi, kikaivunjavunja, tena alisikia yowe 
ndogo, na halafu sauti kali, (Ilikuwa ile ya 
Sungura Mweupe.) akiita akisema ““ Ewe Patriki, 
umekwendapi?” MKisha Elisi akasikia sauti 
asiyopata kusikia, ya mtu mmoja akijibu aki- 
sema ““ Nipo Bwana, nafukua matunda.” Su- 
ngura akasema “Maana yake nini kufukua 
matunda? Mjinga we! Njoo upesi unisaidie 
nitoke katika mitungi.” Elisi akasikia tena 
kelele za vyombo vikivunjika; Sungura aka- 
sema “Sasa, niambie Patriki, waona nini 
dirishani ?” 

“ Naona mkono Bwana.” 

“ Haiwezekani! Sijapata kuona mkono mku- 
bwa namna hii. Mpumbavu we! Tazama 
umeenea dirisha lote !” 

“Kweli Bwana, lakini ni mkono ujapokuwa 
mkubwa.” 

“Vema, Lakini unafanya nini dirishani ? 
Hauna ruksa kuwapo huko, nenda kauondoe, 
kautupe.” 

“Mimi naogopa Bwana, tena sitaki kuutupa.” 

“ Fuata maneno yangu upesi, mwoga we!” 


NYUMBA YA SUNGURA 39 


Elisi akataka tena kumkamata Sungura lakini 
akashindwa, alisikia mayowe mawili memba.- 
mba, na tena ke- 
lele za mitungi 
inayovunjika, 
akasema kimoyo- 
moyo “ Mitungi 
mingi iko kule, 
haiwezekani mimi 
kuvutwa katika 
dirisha, lakini ni- 
mechoka kulala 
hapa.” Akasiki- 
liza sana, haku- 
sikia kitu, ila 
kimya tu, aka.- 
ngoja kwa dakika 
chache, halafu 
akasikia sauti 
nyingi za watu wa- 
liokaribia; mara 
kwa mara maneno 
yao yalifuatana, 
ndiyo: “Iko wapi 


ngazi?” “Lete 
mbili, kazifunge 
. pamoja.” “ We- 
we, shika kamba hii.” “lItafaa, ina imara.” 
“ Mathubuti kabisa.” “Nani atakayetelemka 


bombani?” “Si mimi.” “Mimi sitaki.” 


40 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


“Mimi naogopa.” “Mimi nakataa.” “Wi- 
lyam, hii ni kazi yako, umetumwa na Bwana, 
panda upesi!” , Wakumbuka Msomaji ya kwa- 
mba mguu wa Elisi ulikuwa bombani, kwa 
hiyo aliposikia shindo darini alisema moyoni 
“ Wilyam ndiye atakayeshuka bombani, lija- 
pokuwa jembamba nadhani ya kuwa naweza 
kumpiga teke.” Akaukweza mguu kama ali- 
vyoweza, akangoja mpaka akasikia mnyama 
bombani, ndipo akapiga teke kwa nguvu. 
Hakujua hata kidogo ni mnyama wa kabila 
gani. 

Palikuwa na ghasia kabisa nje, Elisi aka- 
sikia maneno haya: “ Tazama Wilyam!” “Loo 
anaruka kama ndege!” “ Uchawi gani huu ?” 
“ Mkamate Patriki we.” “Mimi nitampa da- 
wa.” “Mshike kichwa.” “Waonaje Kaka.” 
“Mambo gani umepata ?” “ Tuambie yote.” 
Wilyam akajibu kwa sauti ndogo akasema 
“Mimi siwezi kueleza, kiti kikubwa, kama 
mguu wa binadamu kimenipiga nilipokuwa 
bombani, nikatoka kama mshale uliotoka ka.- 
tika upindi.” Wenzake wakamjibu “ Kweli, 
umeruka kama mshale.” 

Sauti ya Sungura Mweupe ikasikilizana, wote 
wakanyamaza; Bwana Sungura akasema “ La- 
zima tuichome nyumba hii.” Elisia kapaza 
sauti sana akasema ““Mkichoma nyumba nita- 
mtuma Dina awakamate ninyi nyote.” Mara 
wote nje wakatulia, baadaye wakaanza tena 


NYUMBA YA SUNGURA 41 


kutembeatembea. Sungura Mweupe akasema 
“ Kikapo kimoja kitatosha kwanza.” Elisi aka- 
fikiri “Ndani ya kikapo mna nini?” Mara 
akatambua, maana mawe mengi madogo yali- 
ingia dirishani, machache yakampiga usoni; 
akasema ““ Tulieni sasa hivi.” Mara watu wa nje 
wakasita kuyatupa. Elisi akayatazama mawe 
yaliyokuwa chini, akaona ya kuwa yame- 
geuka kuwa pelemende, akadhani akasema 
moyoni “ Nikila pelemende labda urefu wangu 
utapungua.” Akaila moja, akafurahi sana kwa 
kuwa amepunguka mara, akawa mdogo wa 
kuweza kuondoka; akatoka nyumbani. 

Nje palikuwa na makutano ya wanyama na 
ndege; Wilyam alikuwa Mjusi, alikuwa kati 
kati ya kundi, akibembelezwa na Komba 
wawili, waliokuwa wakimpa dawa. 

Walipomwona Elisi wanyama wote wakapiga 
kelele sana, wakafukuza upesi wapate kumka.- 
mata; Elisi akapiga mbio akawashinda, aka- 
jificha kati ya miti mikubwa mizuri sana 
mwituni. 

Elisi alitembeatembea mwituni, akasema 
“ Kwanza afadhali nifikiri jinsi ya kutengeneza 
urefu wangu, niwe sawa sawa, kisha niingie 
katika bustani niliyoiona zamani kidogo.” Ma- 
shauri haya yalikuwa mazuri lakini Elisi haku- 
jua jinsi ya kuyatimiza. 

Ghafula yule mtoto alishtuka kusikia kilio 
cha mbwa juu yake, akainuisha macho akaona 


42 — ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


mtoto wa mbwa aliyekuwa akimtazama kwa 
makini; mbwa akanyosha mguu mmoja aka- 
jaribu kumgusa mtoto; Elisi akapiga uruzi 


au YA 
UNE 5. Ba | ) 


A 


akasema “Basi mbwa, pole pole!” Lakini - 
aliogopa sana akasema “ Akiwa na njaa ata- 
nila.” Akatwaa fimbo akacheza na mbwa 


NYUMBA YA SUNGURA 43 


akijilinda nyuma ya maua yenye miiba, aka- 
sema kimoyomoyo “Ni kama kucheza na 
tembo!” Akawa na hofu kuwa atavunjika 
na miguu yake, lakini hakuthubutu kukimbia 
mpaka mbwa akawa amechoka kabisa, alipo- 
kwisha kuchoka mbwa akalala akitweta sana, 
akafumba macho; mara Elisi akakimbia, na 
hakukaa mpaka kilio cha mbwa kilisikilizana 
kwa mbali sana. 

Elisi alipumzika penye kivuli cha njugu, 
akajipepea kwa jani moja, akasema “ Wala.- 
kini ni mbwa mzuri sana, bali mimi mdogo, 
sikuweza kumtiisha, lazima nijiongeze urefu, 
lakini hapa chakula hakuna, sijui nitakacho- 
kula.” Elisi akatafutatafuta bila kuona cha- 
kula hata kidogo. 

Mara Elisi aliona uyoga, urefu wake kama 
yeye mwenyewe, akatazama chini yake, hala- 
fu akataka kutazama juu ya ule uyoga, aka- 
chuchumia akaona juu Mdudu mkubwa wa 
rangi ya buluu, alikuwa amekaa amejikumbatia 
akivuta kiko cha Kihindi; hakujishughulisha 
na Elisi kwa neno lo lote. 


Kaa 
La, 
4 
IS 
4 
4 


II, 
Ki | KA 
N ” 


am LI 
aa SI 


SURA V 
MASHAURI YA MDUDU 


ELisi na yule Mdudu walitazamana kwa dakika 
chache, bila kusemezana. Mwisho Mdudu ali- 
toa kiko kinywani akasema kwa ulegevu “ Ja- 
mbo mwanangu, nani wewe?” Elisi akajibu 
kwa hofu kidogo akasema “Sijui Bwana, 
saa ile nimegeuka mara nyingi sana, na sasa 


labda ni mtu mwingine!” Mdudu akajibu 
4 


MASHAURI YA MDUDU 45 


“Sielewi, eleza tena.” Elisi akasema ““ Siwezi 
kueleza, maana sijifahamu mwenyewe, lakini 
najua hili, ya kuwa ni vigumu sana kuwa na 
urefu mbali mbali katika siku moja.” Mdudu 
akavuta kidogo akasema “Si vigumu.” Elisi 
akajibu “Wewe mwenyewe kama utakuwa 
kama kipepeo utafahamu kuwa ni vigumu.” 
Mdudu hakukubali akasema “La! Hasha!” 
Elisi akajibu akasema “Labda sisi mambo 
yanatudhihirikia, lakini kwangu mimi naona ni 
vigumu kugeuka.” Mdudu akamtazama Elisi 
kwa dharau akasema “Nani wewe?” Elisi 
akakasirika akasema ““ Umeturudisha mwanzo 
wa mazungumzo yetu, nadhani ni juu yako 
kwanza kuniambie habari zako.” Mdudu aka- 
mtazama akasema “Kwa nini?” ELlisi aka- 
shindwa kabisa kujibu, akaenda kidogo, lakini 
yule mdudu akamwita akasema “ Rudi. Nina 
neno.” Elisi akakubali akarudi. Mdudu aka.- 
sema “ Usikasirike. Basi.” Elisi akazidi ku- 
kasirika akasema “ Neno lako ndilo hili tu ?” 
Mdudu Mdudu akajibu “La.” Yule mtoto 
akafikiri ya kuwa anayo nafasi, kwa hiyo 
akangoja, apate kusikia maneno ya Mdudu; 
akakaa kwa uvumilivu; muda wote huyu 
Mdudu alikuwa akivuta kiko kwa pole pole, 
halafu alinyosha mkono akaondoa kiko mdo- 
moni akasema ““ Je, wadhani kuwa umegeuka ?” 
Elisi akajibu kwa huzuni akasema “ Kweli 
nimegeuka, kwa hiyo nasikitika sana, tena kwa 


46 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


sababu hii siwezi kukumbuka elimu niliyoji- 
funza chuoni, na urefu wangu umwbadilika 
mara nyingi.” Mdudu akamtiisha Elisi kama 
mwalimu, akasema “Soma kwa moyo “ We 
mzee Baba Wilyam.'” Elisi akasimama wima 
akajifunga mikono nyuma, akanena 


wi Y WI DI Y Mza 
Bi ya Y 5 LA 
SI f KUZUA j AN 
” NI 
TA - 
Nd ia 
YA EN WAL 
YA 
NI wa 
| N ua 
YA, 
A wa 
YA 


“We mzee Baba Wilyam,” 'kasema mwanake, 
“< Nyeupe kabisa nywele, 

Kusimama kwa kichwa imekufalia ? 

Je, utacheza. milele ?”” 


Baba Wilyam 'kajibu “ Katika utoto 
Nilihofu kudhuru ubongo, 

Bali sasa najua kichwani ni tupu, 
Nikazidi pindua mgongo.” 


MASHAURI YA MDUDU 47 


KEeEv g. 
Ma AA AA WATU AU | 
“Wem - zee Bamba Wil-yam,” 'ka - se- ma mwan- 


UJANA | aa Wa 
a-ke, “N-ye - u-peka - bi —- sany - we - le, 


| kani EN TUI 
Ku-si - ma-makwa ki-chwai - me- ku-fa- 


1| aw AWA NUNA 


-Ti - a? Je, u-ta - che-zami - le - le?” 
TI 
lA 
Jialaa 3 
KA Aa ” 
J7Ph ji ; 
j UE. 
C AI ; | ua Z 
v AU iji | AI Y . yA 
(mp i j ji ai l 
yy IJI Wi 


Mwana 'kasema ““ We mzee baba yangu, 
Kama nilivyosema zamani, 

Walakini ingia kwa kichwani chini 

Ni desturi ukija nyumbani.” 


48 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Mzee akasema ““ Katika utoto 
Nilijilainisha mwili 

Kwa dawa katika sanduku za chuma 
Na nitakuuza mbili.” 


WAS 


- ” 
Aa 


: 
— 
———— 
AI 


Kijana 'kasema “ Wewe kibogoyo, 
Huwezi kula ila wali, 

Lakini wameza mbuzi mzima 
Jinsi gani? Nijibu maswali.” 


“Nilikuwa Mwamusi zamani kidogo, 
Na Mwamusi ni mtu wa cheo, 

Kila siku mashauri, na tayani mwangu 
Nguvu hukaa hata leo.” 


MASHAURI YA MDUDU 49 


Kijana 'kasema ““ We mzee Baba Wilyam, 
Lakini najua, waweza 

Simamisha samaki mkubwa puani 

Namna gani mzee ? Nieleza.” 


Mzee akasema kwa nguvu na chuki 
“ Nimejibu maswali matatu, 
Itatosha mwanangu uache ujinga, 
Nenda! Nisikupige kiatu.” 


am VINA CIA wa SA 
YA Au YA YA 

ad KU ; AL 
4 ? nn 
YA ERA 

y AN A WI 

# AA 


; 
ka 
” 
- 


Ga 


ULA MITA 


TA 15 ” 
IT aa WI “ AU 
wai WA AZI 
” 


Ii 
A 


iE 


Mdudu akasema ““ Maneno haya si sawa sa- 
wa.” Elisi akajibu akasema “ Hata mimi nao- 
na si sawa sawa kabisa.” Mdudu akaitikia 
“Si sawa sawa hata kidogo.” Wote wawili 
wakanyamaza muda wa dakika chache, hala- 

> 


AIW—D 


50 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


fu Mdudu akasema “ Wataka kuwa na urefu 
gani?” Elisi akajibu “Habari za urefu ni 
mamoja kwangu, lakini sipendi kugeukageu- 
ka hivi. Umefahamu?” Mdudu akajibu “ Si- 
jui.” Elisi akanyamaza kwa kuwa maisha 
yake yote hajapata kupingwa na maneno na- 
.mna hii, akakasirika; Mdudu akamwuliza “ Je, 
u radhi sasa?” Elisi akajibu “ Ningependa 
kuwa mkubwa zaidi kidogo, maana kuwa na 
urefu kama uyoga tu si vizuri.” Mdudu aka- 
simama wima akasema kwa nguvu “ Urefu wa 
uyoga ni kimo kizuri kabisa ' (huu ndio urefu 
wa Mdudu mwenyewe). Elisi akapiga mguu 
akasema kwa hukumu “ Mimi sijazoea kuwa 
mdogo.” Akawaza ya kuwa vyumbe vya nchi 
aliyokuwamo hawakawii kuchukiwa. Mdudu 
akasema “Baadaye utazoea.” Akatia kiko 
midomoni akavuta. Elisi akangoja kwa uvu- 
milivu hata Mdudu aliposema tena. Mdudu 
akaendelea kuvuta tumbako, halafu akapiga 
mwayo mara mbili tatu, akajitetemesha, aka- 
shuka juu ya uyoga, akatambaa katika ma- 
jani; alipokuwa akienda akasema “ Upande 
mmoja utakuongeza, upande wa pili utaku- 
punguza urefu.” Elisi akasema ““ Asante Mdu- 
du.” Akanena kimoyomoyo. “ Pande za ni- 
ni?” Mdudu akajibu kana kwamba anawaza 
tu, akasema “ Pande za uyoga.” Akatoweka 
mwituni. 

Elisi akakaa akautazama ule uyoga, apate 


MASHAURI YA MDUDU 51 


kutofautisha pande zake, kazi hii ilikuwa ngu- 
mu maana uyoga ulikuwa mviringo kamili; 
akanyosha kabisa mikono akashika ukingo wa 
uyoga kwa mikono miwili akaumega vipande 
viwili, kimoja katika mkono wake wa kulia na 
kingine katika mkono wa kushoto, akajiu- 
liza “Kipande kipi kitaniongeza, na kipande 
kipi kitanipunguza ?”  Akala kidogo kile ki- 
pande cha mkono wa kulia, Kabla hajamaliza 
kula alijipiga vidole vya miguu kwa kidevu; 
akaogopa sana, akaanza upesi kula kile kipande 
cha mkono wa kushoto kazi hii ilikuwa ngumu 
sana maana kidevu kilikuwa kimekaribia sana 
vidole vyake vya miguu, ilikuwa hakuna nafasi 
ya kutafuna, lakini kwa shida akaweza, aka- 
sema kwa furaha “ Sasa kichwa kimeokoka.” 
Lakini kabla hajamaliza kusema aliogopa tena 
kwa kuwa hakuweza kuona mabega, hata 
kidogo, alipoinamisha macho hakuona kitu 
ila shingo tu; shingo ilikuwa refu sana kupita 
ile ya twiga, na shingo yenyewe ilitokeza juu 
ya majani ya miti, juu kabisa, kama mnazi 
katika mashamba. Elisi akafikiri “ Majani yale 
ya nini? Tena mabega yangu ya wapi? Si- 
wezi kujiona, hata mkono.” Alipokuwa aki- 
sema maneno haya alinyosha mkono lakini ha- 
kuuona, aliona tikisiko la majani tu. Kwa 
sababu hakuweza kuufikisha mkono kichwani 
alijaribu kuinamisha kichwa kifikie mikono, 
akaona furaha ya kuwa aliweza kuipindapinda 


52 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


shingo kama mwili wa nyoka, akaona ule 
uwanda wa majani, na kumbe ulikuwa vilele 
vya miti tu. 

Ghafula ndege kubwa aliruka usoni mwake 
Elisi, akampiga sana kwa mabawa, akasema 
kwa sauti nyembamba “Nyoka! Nyoka!” 
Elisi akajibu kwa hasira ““ Usinipige hivi, mimi 
si nyoka.” Lakini Ndege akazidi kufanya ma- 
tata na kusema “Nyoka! Nyoka!” Akatoa 
machozi akasema “Kila mahali nimetafuta, 
lakini hapana mahali pa kuwafalia watoto wa- 
ngu.” Elisi akajibu akasema “Sielewi hata 
kidogo.” Ndege akasema “ Nimejaribu ma- 
shina ya miti; nimejaribu dari za nyumba, ni- ' 
mejaribu maboma ya shamba, bali wale nyoka 
wabaya wamenifuata kila mahali.” Elisi aka- 
zidi kushindwa, lakina hakumkatiza maneno 
ndege, mpaka alipokwisha kusema. Ndege 
akaendelea kunena akasema “Ni kazi kubwa 
kuangua mayai, tena imenilazimu kuyalinda 
kutwa kucha, sikuupata usingizi tangu juma 
tatu, nimechoka kabisa.” Elisi akaanza ku- 
fahamu akamjibu akasema “ Nasikitika sana 
ya kuwa umesumbuka hivi.” Ndege akasema 
“ Wakati nilipouchagua mti mrefu kupita yote 
mwituni na nilipodhani ya kuwa mayai yangu 
yatakuwa salama mara nilimwona nyoka ali- 
yetoka mbinguni. ... Ewe Nyoka! Nenda 
zako.” Elisi akajibu akamwambia ““ Mimi si 
nyoka, mimi... mimi...mimi....” Ndege 


MASHAURI YA MDUDU 53 


akasema “Sasa nani we? Naona ya kuwa 
wajaribu kusingizia kitu.” Elisi akajibu “ Si- 
singizii; mimi binadamu.” Ndege akamtazama 
Elisi akacheka akasema “ Nimeona watoto 
wengi sana, lakini sijapata kuona mtu mwenye 
shingo refu kama yako, huwezi kukana ya 
kwamba wewe u nyoka, je, huli mayai?” 
Elisi akajibu “ Nala mayai, lakini ni desturi 
ya wanadamu kula mayai, kama ilivyo desturi 
ya nyoka.” Ndege akasema “ Sikusadiki, la- 
kini ikiwa kweli kwamba wanadamu wanakula 
mayai kama nyoka, basi mimi nawachukia 
kama nilivyowachukia nyoka.” Elisi akajibu 
akasema ““ Mimi sitafuti mayai yako, hata kama 
ningetafuta nisingependa yako, wala mimi sili 
mayai mabichi.” Ndege akatulia akasema 
“Vema, nenda zako.” Akarudi kiotani. Eli- 
si akaendelea kuinamisha kichwa kama alivyo- 
weza, ilikuwa kazi ngumu, maana mara kwa 
mara shingo yake ilikwama matawini. Mwisho 
akafaulu akakumbuka ya kwamba alikuwa 
ameshika vile vipande viwili vya uyoga. Akaa- 
nza kula, kimoja kwanza, kisha kingine mpaka 
urefu wake ukawa sawasawa, akajichangamsha 
akasema “Sasa limetimia shauri langu nusu 
yake, lililobaki kwangu ni kuona bustani.” 
Akatembeatembea mwituni. Kitambo kidogo 
Elisi akaona nyumba ndogo, kimo chake kiliku- 
wa kama cha meza; akajiuliza ““ Nyumba ya 
nani hii? Lakini haifai kabisa kupiga hodi, 


54 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


maana mimi mkubwa! Mwenye nyumba atao- 
gopa sana kama akiona jitu kama mimi?” 
Akala kidogo kipande kile cha uyoga cha 
mkono wa kulia, wala hakuthubutu kukaribia 
nyumba mpaka alipokuwa amejipunguza akawa 
na urefu wa inchi tisa. 


UMO 
YA ka 


SURA VI 
NGURUWE NA PILIPILI 


ELisi alisimama akatazama nyumba muda 
wa dakika chache, akaona kuwa ilikuwa nyu- 
mba ya Kizungu, safi kabisa; na alipokuwa 
akisimama akaona askari aliyetoka mbio mwi- 
tuni; alimjua kuwa ni askari kwa ajili ya ma- 
vazi yake; lakini usu wake ulifanana na ule 
wa samaki. Askari Samaki akaenda mlangoni 


akabisha sana, akapiga hodi mara nyingi; 
55 


56 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


mlango ukafunguliwa na askari mwingine mwe- 
nye uso wa chura, alitoka nyumbani. Elisi 
akasogea kidogo apate kusikia maneno yao. 
Askari wa kwanza alikuwa na barua kubwa 
sana, akampa askari wa pili kwa heshima 
akasema ““ Barua hii inatoka kwa Malkia Mzu- 
nguwapili, inakwenda kwa Mama Mkubwa, 
ataka acheze Kriketi naye.” Askari mwenye 
uso wa chura akayakariri maneno yale aka- 
sema ““ Barua hii inakwenda kwa Mama Mku- 
bwa, inatoka kwa Malkia Mzunguwapili, ataka 
acheze Kriketi naye.” Askari wakasujudiana 
sana, na kwa hiyo Elisi alicheka mno, akaki- 
mbia tena mwituni wasiweze kumsikia. Ali- 
potazama tena aliona ya kwamba Askari Sa.- 
maki alikuwa amekwisha kwenda, na mwingine 
alikaa penye mlango akitazama mbinguni ka.- 
na kwamba ni mpumbavu; Elisi akaenda mla- 
ngoni akabisha akapiga hodi; Askari Chura ha- 
kumzuia, akamwambia “Unapiga hodi bure 
kwa sababu mbili; ya kwanza kwa kuwa sisi 
sote wawili tupo upande wa nje wa mlango; 
ya pili kwa kuwa wale waliomo ndani wana- 
fanya kelele sana, hawawezi kusikia sauti yako.” 
Elisi akasikiliza na bila shaka palikuwa na 
ghasia kubwa ndani; alisikia kilio cha mtoto 
mchanga, na chafya nyingi, na mara kwa mara 
shindo kubwa kana kwamba sahani au birika 
limevunjwavunjwa. Elisi akasema “ Nataka 
kuingia.” Chura akajibu “ Mlango ungekuwa 


NGURUWE NA PILIPILI 57 


kizuio kati yetu ingefaa kupiga hodi.” Ali- 
pokuwa akisema Askari hakuacha kutazama 
mbinguni; Elisi akasema kimoyomoyo “ Labda 
na lazima afanye hivi, maana macho yake ni 
juu ya kichwa chake, lakini sharti anijibu.” 
Akapaza sauti akasema tena ““ Nataka kuingia.” 
Chura akajibu ovyo akasema “Mimi nitakaa 
hapa mpaka kesho.” Alipokuwa akisema mla- 
ngo ulifunguliwa na sahani kubwa (iliotupwa 
na mtu ndani ya nyumba) ikaruka ikampiga 
chura puani, ikavunjika penye shina la mti 
nyuma yake; Askari akaendelea kusema kana 
kwamba hakupigwa, akanena “... au labda 
kesho kutwa.” Elisi akajibu kwa hasira aka- 
sema, “Namna gani! Nipe ruksa kuingia.” 
Askari akanena “Je, umepewa ruksa kuingia 
na mwenye nyumba?” Elisi akanyamaza akao- 
na haya. Chura akaendelea kusema “Mimi 
nitakaa hapa mara kwa mara kwa siku nyingi 
sana.” Elisi akasema “ Na mimi je?” Aska- 
ri akapiga uruzi akasema ““ Fanya upendavyo.” 
Elisi akasema kimoyomoyo “ Hakuna faida 
kuzidi kusema naye, yeye mjinga kabisa.” 
Akafungua mlango mwenyewe akaingia nyu- 
mbani. 

Ndani palikuwa na jiko la Kizungu; lililotoa 
moshi nyingi sana. Mama Mkubwa alikuwa 
amekaa kitini akimbembeleza mtoto. Mpishi 
alikuwa akikoroga chakula katika chungu kiku- 
bwa. Elisi akaenda chafya akasema “ Zimo 


58 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Pilipili nyingi sana katika chakula!” Hata 
Mama Mkubwa alienda chafya mara kwa 
mara, na yule mtoto hakuacha kuenda 
chfaya na kulia. Walikuwa watu wawili tu 
waliokuwa hawaendi chafya, walikuwa Mpishi 
na Paka mkubwa aliyekuwa amekaa penye 


p 


Maa aa an 
AA 


moto akichekelea sana. Elisi akasema ““ Shi- 
kamoo Mama Mkubwa. Tafadhali niambie kwa 
sababu gani Paka wako ametoa meno hivi?” 
Mama Mkubwa akajibu akasema “ Kwa saba- 
bu ni Paka Mcheshi. Nguruwe We!” Alise- 
ma maneno yale ya mwisho kwa nguvu sana, 
Elisi akashtuka akadhani ya kuwa mama ame- 


NGURUWE NA PILIPILI 59- 


msema yeye ““ Nguruwe ”” lakini alifahamu ya 
kuwa amemwita yule mtoto, akajipa moyo 
aksema “ Sikujua ya kuwa paka huweza ku- 
chekelea!” Mama Mkubwa akajibu “Ana- 
weza. Tena wengi wametenda hivi.” Elisi 
akanena “Mimi sijapata kuona paka ache- 
kaye,” Mama Mkubwa akajibu “ Pana mambo 
mengi ambao wewe hujapata kuona.” Mpishi 
alikiepua chungu jikoni, akatwaa vijiko na 
sufuria na sahani akawatupia Mama Mkubwa 
na mtoto, Mama hakumjali mwanawe ambaye 
alikuwa akilia sana wakati ule wote, wala 
haikujulikana kama amepigwa ama siyo. Elisi 
akasema “ Angalia Mpishi wee umempiga mto- 
to!” Mama Mkubwa akasema “ Watu wote 
wakishika lao ulimwengu utaendelea vizuri.” 
Mpishi akarudi mekoni akakoroga chakula kwa 
nguvu, akazidi kunyunyiza pilipili. Elisi aka- 
sema ““ Tafadhali Mama, niambie ...” Ma- 
ma Mkubwa akamkatiza maneno akasema “ Usi- 
niudhi.” Akambembeleza sana mtoto aka- 
mwimbia akisema: 


Mkaripie mwana wako, 
Na akienda chafya, 
Atenda hivi kusumbua, 
Hajambo, ana afya. 


Wote, pamoja na Mpisha na Mtoto Mchanga 
wakaitikia: “ Wawawawawa ” Mama akaimba 
ubeti wa pili, akamrusha mno mtoto, aliyelia 


60 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


hata Elisi alisikia kwa shida maneno ya 
wimbo. 


Namkaripia mwana wangu, 
Nampiga akilia 

Apenda sana pilipili 

Na moshi chafu pia. 


Mama Mkubwa akamtupia Elisi mtoto mcha.- 
nga akasema ““ Mshike wee, maana imenilazi- 
mu nijiweke tayari kucheza Kriketi na Malkia 


KEY G minor. 


li ka IA WA AA AA 
M - kari - pi-e mwa-na wa-ko, Na 
MA kaa Aa .m|fimirid 
a-ki - en-da chaf-ya, A - tenda hi-vi 
l miri dis | AWA aaa KA kii | 
ku-sum-bua, Ha-jam-bo, a-na af - - ya. 


Mzunguwapili.” Akatoka chumbani, Mpishi 
akamtupia sufuria. 

Elisi alimshika kwa shida mtoto, maana ali- 
kuwa ajinyonganyonga, mwisho akamshika sa- 
na kwa mguu wake wa kushoto na sikio la 
kulia, akamchukua nje mwituni apate kupu- 
nga hewa, akasema “Lazima nimpeleke nje, 
wasimwue kule jikoni. Pole mwanangu, wa 
mekupiga sana sivyo? Watu hawa ni waji- 
nga kabisa, hawajui kukutunza.” Mtoto aka- 


NGURUWE NA PILIPILI 61 


guna kama kujibu, Elisi akamwambia “ Usi- 
gune! Si vizuri kuguna kama nguruwe.” Yule 
Mtoto akazidi kuguna, Elisi akamtazama sana 
kwa mashaka, pua yake yalikuwa kama. pua 
ya nguruwe, na macho yake yalikuwa madogo. 
Elisi akafikiri ya kuwa ni kwa sababu ya kulia 


yA. 


sana ndipo akavimba pua; akaendelea kute- 
mbea akasema “ Ukigeuka kabisa kuwa ngu- 
ruwe, basi wewe si mtoto wa kusuhubiana 
nawe.” Mtoto akaguna tena, Elisi akatulia 
akamtazama kwa hofu, na ilikuwa hakuna 
shaka, mtoto alikuwa amekwisha geuka kuwa 
mtoto wa nguruwe. Elisi akamsimamisha chi- 


62 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


ni, akafurahai kumwona anaweza kutembea, 
alimtazama akikimbilia mwituni. 

Elisi, alipokuwa peke yake akainuisha ma.- 
cho akashtuka kumwona Paka Mcheshi aliye- 
kuwa amekaa penye tawi la mti mbali kidogo. 
Elisi akamsogelea Paka, naye alikuwa ameche- 
kelea sana, yule mtoto akafikiri ya kwamba 
sura yake ilikuwa ya upole, lakini meno yake 
na kucha zake zilikuwa kali. Akasema kwa 
hofu kidogo “ Hujambo Paka Mcheshi?” “Wa- 
weza kunionyesha njia?” Paka Mcheshi aka- 
jibu akasema “ Wataka kwenda wapi?” Elisi 
akajibu “ Po pote nitakapo!” 

“Kwa hiyo habari ya njia pia mamoja 
kwako.” 

“ Afadhali nifike ahali pengine.” 

“Ukienda mbali, bila shaka utafika pe- 
ngine !” 

“ Watu gani wakaao hapa ?” 

Paka Mcheshi akaelekeza kwa mguu akasema 
“Huko amekaa Mwuza Kofia, na huko Kobe, 
nenda kamwamkie ye yote, wote wawili wana 
wazimu !” 

“ Lakini mimi sipendi kusuhubiana na watu 
wenye kichaa.” 

“ Kwako wewe mbwa ana akili ?” 

“ Naam anayo akili.” 

“Vema, mbwa hutikisa mkia akipendezwa 
na kitu, hunguruma akikasirika, na mimi, 
' nikikasirika natikisa mkia, nikifurai nanguru- 


NGURUWE NA PILIPILI 63 


Ao 
UC io 
Nhif 
Li 


aila ha wa YA 
Aa WA 


IA 


ma, kwa hiyo najua 
sana ya kuwa mimi ni 
mwenye wazimu.” 

“ Lakini wewe hungu- 
rumi! waguna tu.” 

“Sema kama upe- 
ndavyo. Je, utakwenda 
Kriketi na Malkia leo ?” 

“ Ningependa sana 
kucheza, lakini sikui- 
twa.” Paka Mcheshi 
akajibu akasema 
“Tutaonana tena 
huko.” Akatoweka 
mara. Elisi haku- 
shtuka kwani siku zile alikuwa amekwisha 
zoea mambo ya namna hii, na alipokuwa 


64 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


akitazama mahali alipokuwapo paka yule 
mnyama akarudi tena akasema “Je, nini ha- 
bari za mtoto? Nilisahau kukuuliza.” Elisi 
akajibu akasema ““ Amegeuka nguruwe.” Paka 
Mcheshi akacheka zaidi, akasema “Hii si 
ajabu kubwa.” Akatoweka tena. Elisi ali- 
ngoja kidogo akifikiri ya kuwa labda atarudi, 
lakini hakumwona; akatembea kidogo katika 


UA 
in 
. 


njia aliyoionyeshwa na Paka Mcheshi, kufikia 
penye nyumba ya Mwuza Kofia. Kitambo 
kidogo akainuisha macho, akamwona tena Paka 
Mcheshi aliyekuwa amekaa katika tawi jingine, 
yule mnyama akasema “ Ulisema “ Nguruwe ' 
au “Ngurubai”?” Elisi akajibu, “Nilisema 
“ Nguruwe,' tena usitoweke upesi hivi, imenitia 
kizungukizungu.'” Paka Mcheshi akasema 


NGURUWE NA PILIPILI 65 


“Vema!” Akaanza kutoweka pole pole, kwa- 
nza mkia, kisha mwili, halafu uso, na mwisho 
kinywa na kicheko; tena kinywa kilionekana 
kidogo baada ya kwisha kutoweka maungo 
yake. Elisi akasema “Haya! Zamani ni- 
liona paka bila kicheko, bali sijapata kuona 
kicheko bila paka!” 

Kabla hajaenda mbali sana Elisi akaona 
nyumba ya Mwuza Kofia, ilikuwa nyumba 
kubwa, na hakuthubutu kuikaribia mpaka 
alipokwisha kula kidogo kipande cha uyoga 
cha mkono wa kushoto, alichokifunga nguoni, 
ili apate kuongeza urefu kidogo. 

Urefu wake ukawa kama ule wa mtoto wa 
miaka miwili, akaikaribia nyumba, akasema 
“Naomba Mwuza Kofia awe hana kichaa sana.” 


AIW—-E 5 


SURA VII 
KARAMU YA WENYE WAZIMU 


PALIKUWA na meza chini ya mti, mbele ya 
nyumba; kwenye meza walikuwapo watu wa- 
tatu. Walikuwa: Kobe, Mwuza Kofia, na 
Komba. 

Komba alikuwa amelala usingizi na wenzake 
walimwagimia kwa visigino juu ya mgongo, 
walikuwa wakisema kwa kelele. Elisi akafikiri 
“Masikini Komba! Lakini kwa kuwa amelala 
labda si vibaya.” 

Ingawa meza ilikuwa kubwa watu wale 
watatu walikuwa wamekaa kwa kusongana 


sana penye pembe moja; na walipomwona 
66 


KARAMU YA WENYE WAZIMU 67 


Elisi wote wakapaza sauti, wakisema pamoja 
“ Hakuna nafasi, hakuna wasaa!” Elisi aka- 
jibu kwa hasira akasema “ Kuna nafasi tele.” 
Akakaa penye kiti kikubwa cha Kizungu. 
Kobe akasema “ Wapenda kunywa mvinyo?” 
Elisi akatazama mezani, hakuona kitu ila chai 
tu, akasema “ Sioni mvinyo!” Kobe akajibu 
akasema “ Hamna.” Elisi akasema “ Basi si 
vizuri kuniitolea.” Kobe akanywa chai aka- 
sema “Si vizuri kukaa penye meza yetu 
usipoitwa.” Elisi akaona haya kidogo, lakini 
kwa kuwa amejua ya kwamba wenzake wali- 
kuwa wana wazimu akajipa moyo ' akajibu 
“Sikujua kama ni meza yenu, tena pana na- 
fasi ya watu wengi zaidi ya watatu.” Mwuza 
Kofia akamtazama Elisi kwa makini akasema: 
“ Nitamwita mzuzi, nywele zako si sawa sawa.” 
Elisi akajibu “Shika lako. Huna adabu!” 
Mwuza Kofia akafumbua sana macho akasema 
“ Je, Kwa nini kunguru amefanana na meza ?” 
Elisi akafurahai akasema “ Haya! Mafumbo! 
Mimi najua maelezo yake.” Kobe akasema 
“ Wajua maana yake?” Elisi akajibu “ Ha- 
swa.” Kobe akamwambia yule mtoto aka- 
sema “Sema kama ulivyonia.” Elisi akajibu 
“ Kusema kama nilivyonia na kunia kama 
nilivyosema ni sawa sawa.” Mwuza Kofia 
akafikiri sana akasema “Ni mbali mbali ka- 
bisa. Je, kuona ninachokula na kula nina- 
choona ni sawa sawa? La!” Kobe akaitikia 


68 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


akasema “ Je, kupenda ninachopata, na kupata 
ninachopenda ni sawa sawa? La!” Komba. 
akafumbua macho akapaza sauti nyembamba 
akasema “Je, Kutoa pumzi nilalapo na kulala 
nitoapo pumzi ni sawa sawa?” Mwuza Kofia 
akajibu akasema “Kwako wewe Komba si 
mbali, maana siku zote umelala.” 

Wote wakanyamaza kidogo, Elisi akafikiri 
sana juu ya mafumbo ya kungura na meza, 
asielewe. Mwuza Kofia akasema “ Leo ni siku 
gani ya mwezi?” Alipokuwa akisema maneno 
haya akatoa saa mfukoni akaitazama sana, 
akaitetemesha akaiweka sikioni. Elisi aka- 
sema “Ni siku ya nne ya mwezi.” Mwuza 
Kofia akamwambia Kobe akasema “Saa hii 
imekosa majira kwa siku mbili. Nilikuambia 
ya kwambia siagi haifai kwa saa.” Kobe 
akajibu kwa unyenyekevu akasema “ Siagi 
ni nzuri sana.” Mwuza Kofia akasema “ Na- 
jua, lakini palikuwa na vipande vya mkate 
ndani yake, ulitia siagi kwa kisu cha kukatia 
mkate.” Kobe akatwaa saa, akaitazama kwa 
huzuni akaichovya katika kikombe chake cha 
chai, akaitazama tena, akazidi kusema ““ Lakini 
ilikuwa siagi nzuri kabisa.” Elisi pia aliita- 
zama saa, akasema kwa kustaajabu “Hii ni 
saa ya kabila gani? Inaonyesha siku za mwezi 
tu! Habari ya majira hakuna !” 

Mwuza Kofia akamwuliza Elisi akasema ““ Je, 
wewe unaya saa ya kuonyesha mwaka mzima ?” 


KARAMU YA WENYE WAZIMU 69 


Elisi akajibu akasema “Saa za kuonyesha 
mwaka mzima hazipatikani maana mwaka 
mzima ni kipindi kikubwa.” Mwuza Kofia 
akatazama mbinguni akafunga mikono aka- 
sema ““ Na mimi vile vile.” Elisi hakufahamu 
akasema “' Sielewi.” Mwuza Kofia hakumjibu 
Elisi, akawa anamtazama Komba, ambaye 


| | It 


YI / 
yi Ili 


amelala tena, akamwagia chai ya moto puani. 
Komba akajitetemesha akafumbua macho, aka- 
sema ““ Kweli ni kama ulivyosema.” Mwuza 
Kofia akamwuliza Elisi akasema “Je, ume- 
kwisha fahamu majibu ya mafumbo?” Elisi 
akajibu ““ Nimeshindwa kabisa, uniambie ma.- 
jibu yake.” Mwuza Kofia akapiga mwayo 
akasema “Mimi sijui hata kidogo.” Kobe 


70 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 
akaitikia “Wala mimi sijui.” Elisi akasema 
“Ni kupoteza nafasi kutoa mafumbo yasiyo- 
kuwa na majibu.” Mwuza Kofia akashtuka 
akatetemeka akasema “ Angalia mtoto! Uli- 
pomjua “Narasi” kama mimi nilivyomjua, 
ungalimtaja kwa heshima. Je, umepata ku- 
sema na Nafasi?” Elisi akajibu ““ Sijapata 
kusema naye.” Mwuza Kofia akajificha uso 
kwa mikono akasema “ Mimi niligombana sana 
na Nafasi, zamani kidogo, wakati wa Machezo 
ya Malkia Mzunguwapili, nilipomwimbia ... 
Ngoja! Nitawaonyesheni wimbo niliouimba. 


Popo popo unang'aje ? 
Niambie wafanyaje ? 


Je, unajua wimbo huu?” Elisi akajibu “ Nu- 
jua kidogo kidogo.” Mwuza Kofia akaendelea, 
akaimba hivi: 


“ Kama buli, kama kuni 
Unaruka mbinguni. 


“ Popo Popo unang'aaje ? 

Niambie wafanyaje. 

Popo Popo, niambie 
Wafanyaje ? 


Nimekuwa sijamaliza ubeti wa pili ila Malkia 
akaondoka akapaza sauti sana akasema “ Amme- 
uawa Nafasi. Akatwe kichwa.” Na toka saa 
ile Nafasi ni adui yangu, sina bahati naye, 


KARAMU YA WENYE WAZIMU 71 


hanisaidii hata kidogo, na tangu saa ile siku 
zote ni saa kumi na moja.” Elisi akacheka 
sana akasema ““ Sasa waeleza maana ya vyombo 
hivi vyingi mezani, vichache safi na vichache 
vichafu, kwa kuwa kila saa ni saa ya chakula 
cha jioni, na hakuna nafasi kuvisafisha.” Mwu- 
za Kofia akajibu akasema “Haswa! Hiyo 
ndiyo maana yake, nasi hatukai siku zote 


Key C. 

KIMA | ki WI kiio wide 
Po-po po-po u-nang'-aje? Ni-am -bi-e 
BB WA YA aa aa ia AA Wa AA KA AI ba wa Wa Wa 
wa - fan - ya - je. Ka-ma bu-li, ka-ma ku-ni 
Ui AA Kaa WA KAA 
U-na-ru-ka m-bing - u- ni. Po-po po-po 
(| SA AI AA AAA YA AA. 
u - nang'-aje? Ni-am-bi-e Wa-fan - ya-je? 


ie aili azi ii 
Po-po po-po, ni-am - bi-e Wa-fan-ya-je ? 


penye pembe hii ya meza, mara kwa mara 
tunazunguka mezani.” Kobe akapiga mwayo 
akasema “ Tafadhali Mama, tusimulie hadi- 
thi.” Elisi akaogopa akasema “Mimi sijui 
hadithi.” Kobe akasema “ Vema. Ni juu ya 
Komba. Ewe! Amka Kaka.” Kobe na 
Mwuza Kofia wakamfinya sana. Komba aka- 
fumbua macho kwa pole pole, akasema kwa 


72 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


sauti nyembamba “Mimi sikulala, nilisikia 
yote yaliyosemwa nanyi.” Kobe akasema “ Ve- 
ma. 'Tusimulie hadithi.” Elisi akaitikia “ Ha- 
ya, hadithi Bwana Komba.” Mwuza Kofia 
akasema .“ Tena endelea upesi, usilale kabla 
hujamaliza hadithi.” Komba akasema kwa 
haraka “ Hapo kale palikuwa na watoto wa- 
tatu wanawake, majina yao yalikuwa “ Lusi, 
Lesi na Tili”; wote watatu walikuwa wa- 
mekaa chini ya kisima.” Elisi akauliza kwa 
makini “Walikuwa wakila nini?” Komba 
akafikiri kidogo akasema ““Wamekula asali.” 
Elisi akasema ““ Wangalikuwa wakila asali tu 
wangalikuwa hawawezi. Lakini kwa nini 
walikuwa wamekaa chini ya kisima?” Kobe 
akamwambia €Elisi akasema “ Kunywa chai 
zaidi mwanangu.” Elisi akajibu akanena “Si- 
janywa chai baado, hata kidogo, kwa hiyo 
siwezi kunywa zaidi.” Elisi akatia chai katika 
kikombe akanywa, akauliza tena kwa nini 
watoto wale watatu walikuwa wamekaa chini 
ya kisima. Komba akafikiri sana akajibu “ Ki- 
likuwa kisima chenye asali” Elisi akasema 
kwa hasira “ Hakuna kisima chenye asali.” 
Komba akasema “Kama huwezi kuwa na 
adabu afadhali wendelee wewe na hadithi. 
Elisi akajibu kwa unyenyekevu akasema Nasi- 
kitika Bwana Komba, tafadhali endelea na 
hadithi, sitakatiza tena maneno yako, labda 

hupatikana kisima cha asali.” Komba aka- 


KARAMU YA WENYE WAZIMU 73 


vuta pumzi akaendelea akasema “ Watoto wa- 
tatu walikuwa wakijifunza kuteka” ... €Elisi 
alisahau ahadi yake aliyoitoa, akasema “ Ku- 
teka nini?” Komba akajibu kwa uvumilivu 
akasema ““ Waliteka asali.” Mwuza Kofia aka- 
sema “ Nataka kikombe safi, wote wabadili 
viti.” Wote wakasogea kulia, lakini Mwuza 
Kofia peke yake ndiye aliyepata faida, maana 


wengine walikuwa wamekaa katika viti vya 
wenzao. Elisi alikuwa amekaa katika kiti cha 
Kobe; sehemu yake ya meza haikuwa safi. 
Elisi hakutaka kumsumbua tena Komba, aka- 
sema kwa sauti ndogo “ Lakini sijafahamu, 
wameteka asali katika nini?” Mwuza Kofia 
akasema ““ Mjinga we! Waweza kuteka maji 
katika kisima cha maji, na waweza kuteka 
asali katika kisima cha asali.” Elisi hakuu- 


l 


74 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


dhiki akasema “Lakini komba alisema ya 
kuwa watoto wenyewe walikuwamo kisimani.” 
Komba akasema “ kweli, walikuwamo, tena 
walikuwa wakijifunza kuandika herufi “M.”” 
Elisi akauliza “Kwa nini “M' tu?” Kobe 
akajibu “ Maana “M' ni herufi nzuri.” Elisi 
akanyamaza, ““ Komba akafumba macho aka- 
lala usingizi.” Kobe na Mwuza Kofia wa- 
kamfinya, akaamka mara akaitikia “ Herufi 
“M.”” Elisi alikuwa amechoka na upumbafu 
huu, akaondoka, akawaaga wengine akaenda 
zake, Komba akazidi kulala. Alipokuwa mba- 
li kidogo Elisi aligeuka akamwona Kobe na 
Mwuza Kofia wakimtia Komba bulini. Yule 
mtoto akasema ““ Paka Mcheshi alisema kweli, 
wote wawili ni wana wazimu. Sitarudi kwao. 
Sijapata kuona karamu ya ujinga kupita hii.” 
Kabla hajamaliza maneno haya akaona shina 
la mti mkubwa lenye mlango; akaingia na 
kumbe, alijiona katika kile chumba kirefu 
chenye milango mingi, akafurahai sana aka- 
sema ““ Sasa naweza kuingia bustanini, lakini 
lazima nisisahau ufunguo.” Akautwaa katika 
ile meza ya kioo, akaufungua ule mlango 
mdogo, akala kidogo kipande cha uyoga mpaka 
urefu wake ukawa kama ule wa kuku, akaingia 
pangoni, .na mwisho akafika kwenye bustani 
nzuri yenye maua ya kila rangi na chemchemi 
ya maji baridi. 


SURA YAA 
MACHEZO YA MALKIA 


ALiPornGiA bustanini Elisi aliona mti wa ma- 
waridi, wenye maua meupe, lakini watunzaji 
bustani watatu walikuwa wakiyatia rangi nye- 
kundu. Elisi akakaribia kidogo, apate kuona 
vizuri kazi yao, akasikiliza mazungumzo, Mtu 
mmoja akasema “Sasa angalia Tano, usini- 
mwagie dawa hivi.” ” Tano akajibu kwa hasira 
akasema “Si kosa langu, Saba alinipiga kisi- 
gino.” Saba akajibu kwa kiburi akasema 
“Ni desturi yako kushtaki watu siku zote.” 

Tano akajibu “ Wewe huwezi kujisifu, juzi 
75 


76 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


nilimsikia Malkia akisema kuwa wastahili kuka- 
twa kichwa.” Mtunzaji wa kwanza akauliza 
“Kwa sababu gani?” Saba akajibu “ Nita- 
mwambia Tano. Sababu ilikuwa hii: Saba 
alimpelekea Mpishi viazi alipotumwa vitu- 
nguu.' Saba akaangusha burashi yake ya 
kupakia rangi akasema kwa uhasidi “ Sikusa- 
diki, maneno yako ...” Kwa ghafula yule 
Mtunzaji alimwona Elisi, akajikatiza maneno, 
akamsalamia sana, wengine wakamwamkia pa- 
moja. £Elisi akawauliza kwa makini akasema 
“ Niambie, ni kwa nini mmeyatia rangi maua ?” 
Tano na Saba wakanyamaza, wakamtazama 
Mbili, ambaye alikuwa akisema ““ Malkia ali- 
tuamuru kupanda miti ya mawaridi yenye 
maua mekundu, nasi tulikosa tukapanda miti 
yenye maua meupe, na sasa tunapaka maua 
rangi hiyo, makusudi kumdanganya Malkia, 
asitukate kichwa.” Alipokuwa akisema neno 
la mwisho Mtunzaji Tano akapiga yowe aka- 
sema “Tazameni! Malkia Mzunguwapili ! 
Malkia Mzunguwapili! Amekuja.” Watunza- 
ji bustani wakaanguka wote watatu wakalala 
kifudifudi, Elisi akasikia sauti nyingi kwa mbali 
kidogo, akageuka, apate kumwona Malkia. 
Watu wengi walikuwa wakifuatana kwa safu. 
Kwanza Askari kumi wenye rungu. (Askari ha- 
wa wamefanana na Watunzaji bustani isipo- 
kuwa mavazi yao, miili yao yalikuwa miraba 
batabata, miguu yao imetokeza pembeni cha 


MACHEZO YA MALKIA 77 
chini, na mikono imetokeza pembeni kwa 
juu.) 

Kisha katika mfuatano wakapita Mawakili 


Y 


nA 


ZI ai YA yA 


kumi, wamepambwa kwa alama ya Huru Ka- 
rata, wakaenda wawili wawili kiaskari, halafu 
wakaja watoto wa Mfalme Mzunguwanne ku- 


78 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


mi,. walikuwa wameshikiana mikono, wote wa- 
mepambwa alama ya kopa. Mwisho wakaja 
wageni, wote wafalme na malkia, na pamoja na 
hawa Elisi alimwona Sungura Mweupe aliye- 
kuwa amesemasema sana; lakini yeye haku- 
mwona Elisi akampita. Mzunguwatatu, Mja- 
nja wa Kopa akawatangulia Mfalme Mzungu- 
wanne na Malkia Mzunguwapili wa Kopa, naye 
alikuwa amechukua taji iliyowekwa juu ya 
takia, na mwisho kabisa wa maandamano ha- 
ya maarufu wakaja Mfalme Mzunguwanne na 
Malkia Mzunguwapili wa Kopa wenyewe. 

Elisi akaona shaka kidogo akafikiri ya kwa- 
mba labda ilikuwa desturi ya nchi ile ya ajabu, 
kulala kifudifudi mbele ya Mfalme na Malkia 
kama walivyolala Watunzaji bustani, lakini 
alitaka sana kuyatazama mavazi ya umalidadi 
na utukufu wa wakuu hawa, kwa hiyo alisi- 
mama kimya akangoja. 

Walipokuwa wamemkaribia Elisi, watu wote 
wakatulia, Malkia akamwelekeza kidole, aka- ' 
mwuliza Mjanja Mzunguwatatu akasema ““ Na- 
ni huyu?” Mjanja akasimama mbele ya Ma.- 
Ikia akacheka akanyamaza. Malkia akasita, 
akasema kwa hasira “ Mpumbafu we!” Aka- 
mwuliza Elisi mwenyewe akasema “ Jina lako 
nani mwanangu?” kElisi akajibu “ Jina langu 
Elisi.” Akafikiri akasema kimoyomoyo “ Ha- 
ya! Hawa wote ni watu wa karata tu, si- 
'waogopi.” 


MACHEZO YA MALKIA 79 


Malkia akawaona wale Watunzaji bustani 
watatu, hata wakate ule walikuwa wamelala 
kifudifudi, akawatazama akauliza “ Nani ha- 
wa ?” (Wafahanu Msomaji ya kuwa migongo 
yote ya Karata imefanana, na kwa hiyo Malkia 
alikuwa hakujua wa nani. Hakuweza kuwa- 
tambua kuwa walikuwa askari au mawakili 
au watoto wake mwenyewe.) r 

Elisi akajibu “Mimi sijui. Mimi nashika 
langu.” Malkia akatetemeka kwa hasira aka- 
mtazama Elisi kama mnyama ya mwitu, mwe- 
nye macho ya kung'aa, akapaza sauti akasema 
“Mkate kichwa! Mkate Kichwa! Mk...” 
Elisi akamkatiza maneno akasema “La! Ha- 
pana! Upumbafu gani huu?” Malkia aka- 
tulia, Mfalme akamgusa mkono akamwambia 
“Fikiri Mpenzi, huyu ni mtoto tu.” Malkia 
akageuka kwa haraka akamwambia. Mjanja 
“Wageuze hawa.” Mjanja akazigeuza zile 
karata tatu kwa mguu. Malkia akatoa sauti 
kuu akasema “Simameni.” Watunzaji wa- 
kaondoka mara, wakaanza kumsujudia sana. 
Malkia akasema ““ Tulieni, mnanitia kizungu- 
zungu.” Malkia akautazama ule mti wa ma- 
waridi akasema “ Mmefanyaje hapa?” Mbili 
akapiga magoti akasema “Shikamoo Malkia 
mtukufu, Tusamehe; tumejaribu ......” Ma- 
Ikia akamkatiza maneno akasema “ Naona 
maua,” nafahamu sana. Wakate kichwa !” 
Watu wengine wakaendelea kuandamana ili- 


80 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


kuwa imebaki Watunzaji bustani watatu, na 
askari watatu na Elisi. 

Watunzaji wakamkimbilia Elisi wapate ku- 
hifadhiwa naye. 6Elisi akawafariji akasema 
“ Nawapeni pole, hamtuuawa nanyi kamwe.” 
Akawaficha kwa upesi katika mtungi mkubwa 
uliokuwapo karibu. Askari wakawatafuta 
Watunzaji muda wa dakika chache, halafu 
wakakata tamaa wakawafuata wenzao. Malkia 
akapiga kelele akasema “Wamekatwa ki- 
chwa?” Askari wakajibu “ Vichwa vyao ha- 
vionekani.” Malkia akasema “ Vema.” Elisi 
akakaribia. Malkia akamwuliza Askari aka- 
sema ““ Huyu ajua kucheza Kriketi?” Askari 
akanyamaza. £Elisi akajibu mwenyewe aka- 
sema ““ Ndio, najua kucheza.” Malkia akasema 
kwa sauti kali “ Twendeni!” Wote wakaende- 
lea kuandamana; Elisi pia alijiona akitembea 
pamoja na Sungura Mweupe, ambaye alisema 
“Jua kali sana leo siyo?” Elisi akajibu 
“ Kweli ni kali. Je, umemwona Mama Mku- 
bwa?” Sungura akajibu “ Nyamaza mwana- 
ngu,” akamtazama kwa hofu Malkia aliye- 
kuwa akitembea nyuma yake, akachuchumia 
akamnong'oneza Elisi akasema “Kesho Mama 
Mkubwa atakatwa kichwa.” Elisi akasema 
“Amekosa nini?”  Sunguru akamwuliza 
“ Unamwonea huruma?” Elisi akamwambia 
“La. Ni mtu mbaya, astahili kukatwa ki- 
chwa, mnilikuuliza amekosa nini?” Sungura 


'MACHEZO YA MALKIA 81 


akasema ““ Amempiga kofi Malkia.”  Elisi aka- 
cheka sana, Sungura akatetemeka kwa hofu 
akasema “ Angalia, Malkia atakusikia; Mama 
Mkubwa alikuwa amechelewa kidogo, na. Ma- 
Ikia amemkaripia, na...” Malkia akamka- 
tiza maneno, akapiga kelele akasema “Kila 


mtu aende mahali pake.” Wote wakapiga 

mbio, wakaenda ovyo kabisa, wakasimama 

huko na huko, wakaanza kucheza. Ndiyo 

kwanza Elisi aone kiwanja cha Kriketi cha 

namna hiyo, kilikuwa matuta matupu. Badala 

ya kibau cha kupigia mpira walitumia korongo 
6 


AIW—F 


82 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


mwekundu, na mpira wenyewe ulikuwa kaka.- 
kuona, na vijiti vilikuwa askari watatu walio- 
kuwa wamesimama pamoja. 

Wakati wa zamu ya Elisi ya kupiga mpira 
aliona taabu kidogo kwa sababu ya korongo, 
alimshika kiwiliwili, na miguu yake ilikuwa 
inaning'inia nyuma; lakini kila mara akimnyo- 
sha shingo, yeye huikunja, kumtazama usoni, 
na Elisi alikuwa sharti acheke, tena mara kwa 
mara ule mpira kakakuona ulitembeatembea. 

Wachezaji walikuwa hucheza wote pamoja, 
hawakungojea kwa zamu, wote hugombana na. 
Malkia alikuwa amekasirika sana, alipiga kelele 
akajisemea ovyo mara mbili tatu kila dakika 
“Mkate kichwa! Mkate kichwa!” Elisi aka- 
ona shaka akasema kimoyomoyo. “Akiendelea 
hivi, halafu watakuwa wamekatwa kichwa wo- 
te, labda hata mimi pia!” Elisi akatafuta njia 
ya kutoroka bila kufanya matata, na alipokuwa 
akitafuta akaona wingu mbinguni, akalitazama 
sana, akaona winguni meno na kinywa chenye 
kutabusamu, akafurahi akasema moyoni “ Ha- 
ya! Yule Paka Mcheshi. Sasa nitakuwa na 
rafiki.” Kinywa chake kilipotosha kusema 
Paka Mcheshi akamwambia Elisi akasema ““ Wa- 
onaje mwanangu?” Elisi akangoja mpaka 
masikio yake yalikuwa yameonekana, akasema 
kimoyomoyo “ Si vizuri kumjibu mpaka masi- 
kio yake yameonekana pia.” Alikuwa haku- 
ngoja sana ila kichwa chote kilionekana; Paka 


MACHEZO YA MALKIA 83 


akafikiri ya kwamba kichwa kitatosha, kwa 
hiyo hapana haja ya maungo yake kuonekana. 
Elisi akasema “Hujambo Paka Mcheshi ? 
Watu hawa hawachezi sawasawa, tena wamego- 
mbana sana, na kanuni za machezo hawazifu- 
ati.” Paka akauliza ““ Je, unampenda Malkia ?” 
Elisi akajibu “Simpendi hata kidogo...” 
Akajikatiza maneno kwa haraka, kwa kuwa 
Malkia mwenyewe alikuwa amesimama karibu 
naye, akaendelea kusema kwa hila akasema 
“Kwa sababu amecheza vizuri sana, wote 
hawana bahati ila yeye.” Malkia akacheka 
akaenda zake. 

Mfalme akamkaribia Elisi akakitazama kile 
kichwa cha Paka; akamwuliza Elisi akasema 
“ Dude gani hili?” Elisi akajibu “ Ni rafiki 
yangu Bwana Paka Mcheshi.” Mfalme akane- 
na “ Simpendi hata kidogo! Lakini, akipenda, 
ana ruksa ya kunibusu mkono.” Paka Mche- 
shi akajibu “Sipendi.” Mfalme akakasirika 
akasema “ Usinitolee ujuvi !” akajificha nyuma 
yake Elisi, akasema “ Naogopa.” Elisi akajibu 
kwa kumfariji akasema “ Paka ana ruksa ku- 
mtazama Mfalme. Nimesoma maneno haya 
kitabuni.” Mfalme akasema “ Lazima aondo- 
lewe.” Akamwita Malkia akamwambia “ Wa.- 
mwona Paka yule? Lazima aondolewe.” Ma- 
Ikia hakujua njia yo yote kuwahamisha adui 
zake isipokuwa kuamuru wakatwe kichwa, kwa 
hiyo akasema “ Mkate kichwa.” Mfalme aka- 


84 ELISI, KATIKA NCHI YA AJABU 


sema ““ Nitamtafuta Askari mwenyewe.” Aka- 

enda zake kwa haraka. ziwa 
Elisi akarudi kiwanjani apate kuwaona wali- 

oshinda, lakini wote walikuwa wameendelea 


ZI masia 


PIA 


kucheza kwa wasi wasi, na wachezaji watatu 
walikuwa wamekwisha wekwa gerezani. Elisi 
akageuka akaona ya kwamba kundi kubwa 
la watu linamzunguka Paka; nalo lilikuwa liki- 
fanya shauri ya kumkamata kichwa; wote 


AI 


MACHEZO YA MALKIA 85 


wakawa wanasema pamoja, wakafanya kelele 
sana. 

Alipomwona £Elisi, Malkia akamwita aka- 
mwumuru yeye kufanya shauri. Shauri la 
Askari lilikuwa: “ Haiwezekani kumkata ki- 
chwa mtu asiyekuwa na mwili.” Shauri la 
Mfalme lilikuwa: “ Kila mtu mwenye kichwa 
aweza kukatwa kichwa.” Shauri la Malkia 
lilikuwa: “ Kazi hii isipotimizwa upesi watu 
wote watakatwa kichwa.” 

Elisi akafikiri kidogo akesama ““ Paka Mche- 
shi ni mali ya Mama Mkubwa, afadhali aitwe.” 
Malkia akasema ““ Amefungwa gerezani, mlete 
hapa sasa hivi.” Askari akaenda mbio na ufu- 
nguo mkubwa wa gereza. Kichwa cha Paka 
Mcheshi kilianza kutoweka. Basi Mfalme na 
askari wakakimbia huko na huko wakakita- 
futa, na wengine wakarudi kiwanjani. 


SURA IZY 
HADITHI YA KASA 


Mama Mkubwa alimsalimia €Elisi akasema 
“ Nafurahi sana kuonana nawe mwanangu.” 
Elisi pia akafurahi kuona ya kwamba Mama 
Mkubwa alikuwa mwenye hali njema, akafikiri 
ya kuwa labda hasira yake jikoni ilikuwa kwa 
sababu ya pilipili tu, akasema kimoyomoyo 
“ Nitakapokuwa mama mkubwa mimi, sita- 
kula pilipili hata kidogo, chakula bila pilipili 
si kibaya; labda pilipili ni sababu ya hasira 
yote duniani, mtu akila pilipili huwa na hasira, 
basi angekula kwinini angekuwa mchungu, na 
angekula sukari angekuwa tamu.” 

Kwa sababu ya mawazo yake Elisi alimsa- 
hau Mama Mkubwa, ambaye alikuwa ame- 
fuatana naye, akashtuka aliposika sauti yake. 
Mama Mkubwa akasema “ Unafikiri sana mwa.- 
nangu, kwa hiyo unasahau kusema; sasa hivi 
siwezi kukumbuka fundisho la maneno haya, 
lakini nitakumbuka bado kidogo.” Elisi aka- 
jibu “ Labda halina fundisho!” Mama Mku- 
bwa akasema “Hasha! Mwanangu, mambo 
yote yana mafundisho kama ungeweza kuya- 


fahamu.” Alipokuwa katika kusema ma- 
86 


HADITHI YA KASA 87 


neno haya akamjongelea sana Elisi, akamwekea 
kidevu katika bega lake, kijana hakupendezwa 
na tendo hili hata kidogo lakini hakutaka ku- 
mkataza, akasema ““ Sasa wanacheza kwa uta- 
ratibu.” Mama Mkubwa akajibu “ Kweli mwa- 
nangu, na fundisho lililokuambia ndilo: “ Elimu 
ndio mwanga yongozayo kila shani.” Elisi 
akacheka akasema ““ Nikukumbushe Mama ya 
kuwa zamani kidogo ulisema ya kwamba uli- 
mwengu umeendeshwa na watu walioshika 
yao.” Mama Mkubwa akasema “ Tofauti ba- 
ina ya kushika lako na Elimu si kubwa, na mi- 
mi nitapenda sana kukushika mkono, lakini 
naogopa korongo wako, nadhani ana hali mba- 
ya, je, nijaribu?”  Elisi akajibu akasema 
“Labda atakuuma.” Alisema kivi kwa saba- 
bu hakutaka kushikiana mikono na Mama 
Mkubwa; huyu akasema “ Kweli korongo ni 
ndege mkali—kama haradali, vyote viwili hu- 
uma, na fundisho lake ndilo: “Ndege wa 
kabila moja huruka pamoja.” Elisi akasema 
“Lakini haradali si ndege!” Mama Mkubwa 
akajibu “ Bila shaka haradali ni madini, pana 
shimo kubwa la haradali, wala si mbali sana 
na hapa, na fundisho lake ndilo hili: “ Paka 
akiondoka, panya hutawala.'” Elisi ”haku- 
jibu. Mama Mkubwa akasema “ Unazidi kufi- 
kiri?” Elisi akajibu kwa kuudhika “ Lazima 
nifikiri ” Mama akajibu kwa dharau akasema 
“Imekulazimu kufikiri kama ilivyomlazimisha 


88 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


29 


nguruwe kuruka hewani, na mafundisho .....” 
Wazungumzaji nawa wakamwona Malkia Mzu- 
nguwapili ambaye alikuwa amesimama mbele 
yao, wote wawili wakashtuka sana, Malkia 
amejikumbata mwenye sura mbaya kwa ha- 


sira. Mama Mkubwa akatetemeka kwa hofu, 
hata hakuweza kuwapasha wenzake habari za 
fundisho la maneno yake. 

Malkia alimtazama Mama Mkubwa kwa chu- 
ki; Mama alimsalimu sana, akasema kwa sauti 


ndogo “Shikamoo Bibi.” Malkia hakuitikia, 


HADITHI YA KASA 89 


akapiga meno aksema “ Nimekuonya sana, 
Mama Mkubwa, na sasa chagua. Wewe uende 
zako au kichwa chako kiende zake.” Mama 
Mkubwa hakukawia kuchagua, akapandisha 
nguo akakimbia upesi. Malkia akamwambia 
Elisi akasema ““ Twende tukaendelee kucheza.” 
Elisi hakuthubutu kukataa, akamfuata Malkia, 
wote wawili wakarudi kiwanjani. 

Wageni wengine walikuwa wakipumzika ki- 
vulini, lakini walipomwona Malkia waliondoka 
mara wakaenda mahali pao, wakaendelea ku- 
cheza kwa haraka, wakacheza muda wa saa 
nzima, na Malkia hakukoma kugombana na 
wenzake, na kuamuru fulani na fulani akatwe 
kichwa, mpaka wageni wote wakaondolewa, 
hakubaki mtu kiwanjani ila Mfalme na Malkia 
na Elisi. 

Malkia akawa amechoka sana, akawa ana- 
tweta, akamwambia Elisi “Je, umemwona 
Bwana Kasa Mliaji”? Elisi akajibu “ Siku- 
mwona.” Malkia aksema “Vema. Twende 
tukamwamkie! Tena ataweza kukuhadithia 
habari za maisha yake.” Walipokuwa waki- 
tembea pamoja Elisi akamsikia Mfalme Mzu- 
nguwanne mbali kidogo, akiwaambia wageni 
kuwa wamekwisha samehewa. Mtoto akafu- 
rahi sana. 

Malkia na Elisi wakazunguka pembe ya 
njia, wakakutana na Mbuzi, alikuwa amelala 
usingizi. Malkia akampiga Mbuzi akamwa- 


90 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


mbia “Ondoka mvivu we, mpeleke mtoto 
huyu kwa Bwana Kasa Mliaji, apate kusikia 
hadithi yake. Mimi lazima nirudi. Wageni 
wote watakatwa kichwa.” Akaenda zake, aka- 
waacha Elisi na Mbuzi pamoja peke yao. 
Elisi hakupenda sana sura ya Mbuzi yule, 
lakini kutofautisha baina ya ukali wa Malkia 
na ukali wa Mbuzi ilikuwa kazi ngumu. 

Mbuzi alimtazama yule mtoto kwa makini 
muda wa dakika chache halafu akageuka aka- 
mtazama Malkia ambaye alikuwa akienda, 
akasema “Kicheko kiko huko!” Elisi akau- 
liza “ Kicheko gani?” Mbuzi akajibu akasema 
“Malkia anadhani ya kuwa wageni wote wa- 
tauawa, lakini sivyo, hawatakatwa kichwa, 
hata mmoja! Twende!” Mbuzi akaondoka 
Elisi akamfuata. Kabla hawajaenda mbali 
wakamwona Kasa Mliaji; alikuwa amekaa peke 
yake penye mwamba mkubwa, akilia sana 
akitoa machozi. Bahari ilikuwa nyuma yake, 
na bahari ile ilikuwa machozi yake aliyoyatoa 
tangu zamani sana. Elisi akamwuliza Mbuzi 
akasema “Je, amefiwa, ana huzuni gani?” 
Mbuzi akajibu ““ Hana huzuni, wala hakufiwa, 
kama ungemwuliza sababu ya msiba wake 
asingeweza kujibu, ametumwa na Malkia ku- 
jaza bahari watoto wake wapate kuogelea 
ndani.” 

Walipomkaribia Kasa Mliaji, Mbuzi akamsa- 
limia akasema ““ Shikamoo Kasa Mliaji.” Kasa 


HADITHI YA KASA 91 


akafumbua macho na yakatoka machozi me- 
ngi sana, yanayotosha kujaza ndoo mbili, 
Elisi akarudi upesi asiingie maji. Kasa Mliaji 


yA 
; 
AA 
Aa WA 
8 Y 
| 4 
Aa. , A 
; i, 
Dat: 


aa 


NI 


uu 


ui 


B > 
AI 
O ai S - 
Wa li ui 
uu 
Ua 
UU , 
iliua 
Wa. Sa 


AA 


wa 
USI 


Aua 
Wa 


WA Aa aa AA aa 


NY 


akasema kwa shida “ Marahaba. Wataka nini 
rafiki yangu?” Mbuzi akajibu “ Tafadhali 
mhadithie mtoto huyu habari za maisha yako.” 


92 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Kasa Mliaji akatoa machozi zaidi akasema 
“Vema. Kaeni. Tena msinitietie mpaka ni- 
takapokuwa nimekwisha kusema.” Wote wa- 
kakaa kitako, wakanyamaza muda wa dakika 
chache. “Elisi akasema kimoyomoyo“ Asi- 
ngeanza kusema angekuwa hawezi kuisha !” 
Akangoja kwa uvumilivu. Kasa Mliaji aka- 
vuta pumzi akasema: 
“Hapo kale mimi na ndugu zangu tulikuwa 
tumekaa baharini, sisi sote tumehudhuria shule. 
Mwalimu. wetu alikuwa mzee.” Tulimwita 
“fundi.” Elisi akauliza “Kwa nini ulimwita 
“Fundi”?” Kasa akajibu akasema “ Kweli 
wewe mpumbafu! Tumemwita “ FUNDI” maa- 
na aliturundisha.” Mbuzi akasema “ Elisi 
mwanangu, sikujua kuwa wewe u mjinga kama 
hivi!” Elisi akaona aibu akanyamaza. Mbuzi 
akamwambia Kasa akasema “Endelea Kaka, 
sisi hatutaki kukaa hapa mpaka usiku.”. Kasa 
Mliaji akaendelea akasema “ Sisi tulifundishwa 
vizuri, tena tumekwenda kila siku chuoni.” 
Elisi akamkatiza maneno akasema ““ Usiwe na 
kiburi Bwana Kasa, mimi pia nakwenda kila 
siku chuoni.” Kasa Mliaji akauliza “ Ume- 
fundishwa lugha na ngoma?” Elisi akajibu 
“Najifunza kuandika na kusoma.” Kasa 
akaitikia ““ Kwetu sisi tulifundishwa kukandika 
na kuchoma, halafu namna mbalimbali ya 
Hesabu, ndizo: Haki, Kudanganya, Kubiidi- 
sha, na Karamu.” Elisi akasema “ Maneno 


HADITHI YA KASA 93 


yako ni kama mafumbo! Habari za masomo 
mengine?” Kasa Mliaji akasema “ Tumesoma 
“Kiburi cha thamani” (Habari za zamani).” 
Mbuzi akasema “Basi Kasa! Sasa tuambie 
kidogo habari ya machezo ya shule.” 


WA 


SURA Y 
NGOMA YA KAMBA 


Kasa akamwambia Elisi akasema “ Wewe je, 
umepata kukaa chini ya bahari?” Elisi aka- 
jibu “ Sijapata kufika huko hata siku moja.” 
Kasa akanena “Wawajua sana Kamba?” 
Elisi akajibu akasema “ Mara moja niliwao- 
nj !”  Akajikatiza maneno upesi, akasema 
“Siwajui.” Kasa akajibu “ Kwa hiyo huwezi 
kujua furaha ya ngoma ya Kamba?” Elisi | 
akauliza “ Ni ngoma ya namna gani?” Mbuzi 
akaeleza akasema “Kwanza Kamba huenda 
pwani, tena kushikiana mikono halafu wote 
huogelea baharini na kurudi.” Elisi akataba- 
samu akasema “ Ngoma nzuri sana!” Kasa 
akaondoka akasema ““ Twende. Tutakuonye- 
sha. Wanyama wawili wakasimama, wakashi- 
kiana mikono wakaanza kuchezacheza katika 
mchanga.” Wakamtisha sana £Elisi, mana 
miguu yao ilikuwa mikubwa, tena walikuwa 
hawachezi sawasawa. Ilikuwa hakuna ngoma 
lakini Kasa Mliaji aliimba kwa upole na hu- 
zuni; Hivi: 


94 


NGOMA YA KAMBA 95 
Key E) 
Il—:s£ | mm: ss AA EA AA WA 
-Che-wa a-mwa-mbia Ko-a, Ta-fa - dha-li ka-sa 
if aa: aa NAE BA KA USE US LE AA AA ae 
mwen-do, Nyu-ma yan-gu Pa.pa mku-bwa, ni-a ya-ke si ya 
i| Wa AA AA WA AA WA 
pen - do, Ta - za-ma ka-ma Kam-ba wo-te 


AA WA AUAWA AA 
wa-me-tan-gu - lia, Wo-te wa-na-che-za pwa-ni, na n- 


Aa Ua Wa WA UA AA 
go-ma na-si - ki - a.Wa- we-zache-za 'we-za che-za 


SA SA aa Ma WA Wawa KA SA waya ka AA WA SE Sa 
'we-za che-za na - si, 'we-za che-za 'we-za che-za 
WA NIA AA AAA JI 

'we- za che-za Au AAA 


Chewa amwambia Koa, “ Tafadhali kaza 
— mwendo, 
Nyuma yangu Papa mkubwa, nia yake si ya 
pendo, 
Tazama kama Kamba nio wametangulia, 
Wote wanacheza pwani, na ngoma nasikia. 


Waweza cheza 'weza cheza "weza cheza nasi. 
Waweza cheza 'weza cheza 'weza cheza 
nasi. 


Tukitupwa baharini tutaogelea sana,” 
Koa akatetemeka, akasema “ La! Hapana. 


96 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Itakuwa mbali mno, tena haiwezekani, 
Nenda peke yako Chewa, nitakungoja pwani. 


Siwezi cheza "wezi cheza "wezi cheza nanyi 
Siwezi cheza 'wezi cheza "wezi cheza nanyi.” 


Samaki akasema “ Pana pwani mpya "ng "a- 
mbo, Za. 

Haya! Jipe moyo Koa, sisi sote -hatuja- 
mbo; 

Mbali na Afrika ni i.karibu Bara Hindi 

Njoo, kacheza Koa, usipige we mapindi. 


Waweza cheza "weza cheza "weza cheza nasi, 
Waweza cheza 'weza cheza 'weza cheza 
nasi.” 


Walipokuwa wamekwisha kucheza Elisi aka- 
washukuru akasema ““ Asanti sana rafiki zangu, 
na sasa mmechoka, kaeni, na mimi nitawaha- 
dithieni matokeo ya leo, tangu asubuhi. Jana 
nilikuwa mtoto mwingine, kwa hiyo ni bora 
nianze hadithi yangu tokea alfajiri leo.” Elisi 
akasimulia matokeo yake, toka alipomfuata 
Sungura Mweupe katika pango lake na mpaka 
mwisho. Alipokuwa akihadithia jinsi alivyo- 
mtiisha Mdudu kwa kusoma shairi, Kasa aka- 
vuta pumzi akasema “Haya ni mambo ya 
ajabu. Sasa jaribu tena kusoma mashairi. 
Simama. Funga mikono nyuma. Useme shai- 


NGOMA YA KAMBA 97 


ri la “Ni sauti ya mvivu” na beti zifuatazo.” 
Elisi akasema kimoyomoyo “ Viumbe hawa 
wanitiishe! Ni kana kwamba niko chuoni!” 
Akaondoka akafunga mikono akasoma: 


KEY FF. 
i|s:s:sim:m:m|fififi UA AA Ja :m:mjd:d:d | 
Ni-na-si-ki-a sa-u-ti ya Kam-ba “ Ni-me-pi-kwa za-i-di, ta- 


Ka kui WA WA WAWA SARA AA IA 
-za-ma ma-gamba! Me-kun-du ka-bi-sa! 'si-ka-e mi-le-le, Ni-on- 


it, AA ANAE AA MIA WA AI 
-do-ke ka-ti-a su-ka-ri ny-we-le.” Ka-ti-ka m-cha-nga naam 


EA AA AA AA AA 
a-li-ji- ta-pa, Na A-ki-dha-ra-u ma - ta-ya ya Pa-pa. La- 


1| WAA KA | ui YA LA Aa sh 


-ki-ni wa-ka-ti wa. ma-ji ma - ku.--- 4 


aa, IA IA — | 
A-li-sa- ha-u u-ho-da-ri huu. 


Ninasikia sauti ya Kamba 

“ Nimepikwa zaidi, tazama magamba ! 
Mekundu kabisa! 'sikae milele, . 
Niondoke katia sukari nywele.” 


Katika mchanga naam alijitapa, 
Na akidharau mataya ya Papa. 
Lakini wakati wa maji makuu 
Alisahau uhodari huu. 


AIW—G 


98 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Mbuzi akasema “ Nilipokuwa mtoto mimi nili- 
jifunza kusoma maneno haya, kwa moyo, bali 
wewe umeyasoma vibaya!” Elisi hakujibu, 
akajikumbata akatazama bahari akafikiri sana 
juu ya matendo yake, na usahaulivu wake. 
Alikuwa amefadhaika. 

Mbuzi akasema “ Endelea mwanangu, sasa 
soma ubeti wa pili, maneno ya kwanza ndiyo 
“Niliona, njiani.” Elisi hakuthubutu kuka- 
taa. Akasoma hivi: 


Niliona njiani, nilipongoja, 

Chui na bundi wakila pamoja; 

Mnyama 'kaguna, akala kwa pupa 
Nyama, mchuzi na hata mifupa. 
'Kamwambia Ndege "Umekula zamani, 
Posho lako mwenzangu ndilo sahani; 
Na kwa ukarimu nakupa kijiko; 

Mali yangu ni kisu na uma. Na mwiko 
Wangu si bundi. Kwa ghafula ali- 

Mla Bundi na chumvi kwa meno makali. 


Mbuzi akasema “Basi! Sisi hatuwezi ku- 
fahamu hata neno moja, eleza.” Elisi aka- 
jibu “ Siwezi kueleza.” Mbuzi akaondoka aka- 
sema “Vema! Tucheze tena. Au labda uta- 
penda kusikia wimbo wa Kasa Mliaji?” Kasa 
akacheka akafikiri ya kuwa alikuwa amesi- 
fiwa, Mbuzi akasema “Uimbe wimbo wa 


NGOMA YA KAMBA 99 


chakula Kaka.” Kasa Mliaji akavuta pumzi 
akaimba: 


Key C. ; 
Il aria m|n-iru)rdl:-|driadm)m:-ire| 
Twen-demwe-nza-ngu, s-a-sasaa  Tu-le cha-ku-la, chaa 


iIrdl-|nfin:s)s:timt | mz): Ishi lthi dirii ra | 
ku-faa, I-ko na-fa-sina..wa-saa Tu-le cha-ku-u-la cha ku- 


ila Jama | AITA 
faa. — Chaku-faa, cha ku-faa, Tu-le cha-ku-la cha ku-faa. 


Twende mwenzangu, sasa saa 
Tule chakula, njoo kukaa, 
Iko nafasi na wasaa 

Kula chakula cha kufaa. 

Cha kufaa, cha kufaa. 

Kula chakula cha kufaa. 


Sisi mwenzangu mashujaa, 
Nasi twaona njaa. njaa. 
Tusitandike kitambaa, 
Tule chakula cha kufaa 
Chakula kizuri cha kufaa 
Tule chakula cha kufaa. 


Mbuzi akapaza sauti akasema “ Tuitikie !” 
Wote wakawa katika kuitikia wakiimba “ Tule 
chakula cha kufaa.” waliposikia sauti mbali 
kidogo, wakanyamaza wakasikiliza, halafu wa- 
kamwona Askari mmoja ambaye alikuwa aki- 


100 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


zitangaza amri za Mfalme Mzunguwanne. Ta- 
ngazo lenyewe lilikuwa hili: “ NJooni Wote! 
Hukumu Kuu Ni Tayari. NJooni. NJoo- 
NI.” Mbuzi akamshika Elisi mkono akasema 
“< Twende.” 

Elisi na Mbuzi wakaenda pamoja kwa ha- 
raka; lakini Kasa Mliaji hakuondoka, akaende- 
lea kuimba na kutoa machozi. 

Elisi alimsikia kwa mbali akiimba: 


Chakula kizuri cha kufaa 
Tule chakula cha kufaa. 


SURA ZI 
MWIZI WA MAANDAZI 


WALIPOKUWA wamefika Bomani Elisi na Mbu- 
zi walimwona Mfalme Mzunguwanne wa Kopa, 
na Malkia Mzunguwapili wa Kopa, walikuwa 
wamekaa penye viti vyao vya enzi, na mbele 
yao mkutano mkubwa wa viumbe. 

Mjanja Mzunguwatatu wa Kopa alikuwa 
amefungwa kwa minyororo, naye alikuwa ame- 
simama kati ya Askari wawili. 

Sungura Mweupe alikuwa akisimama, penye 
kiti cha enzi cha Mfalme, alikuwa akishika 


tarumbeta na cheti. 
101 


102 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Katikati kabisa ya Boma palikuwa na meza, 
na juu ya meza ilikuwa sahani kubwa yenye 
maandazi. 

Mfalme alikuwa mwamuzi, na alikuwa ame- 
vaa kofia ya ujaji na juu ya kofia ile, amevaa 
taji. Penye baraza ndogo wakakaa viumbe 
thenashara, ambao walikuwa wakiandika ka- 
tika vibao vyao kwa 
bidii. Elisi akamwu- 
liza Mbuzi akasema 
“ Wanaandika nini ?” 
Mbuzi akajibu “ Wa- 
naandika majini yao 


wasiyasahau.” Elisi 
akasema “Wapu- 
mbafu!” 


Sungura Mweupe 
akapiga sana taru- 
mbeta, akatangaza 
kwa sauti kuu aka.- 
sema “ Nyamazeni 
watu wote.” 

Mfalme akavaa miwani akatazamatazama, apa- 
te kuona ya kwamba wote walikuwa wametulia. 

Elisi akavitazama vibao vya viumbe the- 
nashara. Akacheka sana hawakujua hata 
mmoja kuandika sawasawa. Elisi akasema 
“kimoyomoyo “ Lakini hawa si binadamu. Nao- 
na mjusi mmoja, panya mmoja, chura mmoja, 
bata, kuku, kenge, komba na wengineo, si aja- 


MWIZI WA MAANDAZI 103 


bu kubwa ya kuwa hawajui kuandika.” Mfa- 
Ime akapaza sauti akasema “Soma mashtaka.” 
Sungura Mweupe akapiga tarumbeta mara tatu 
akatangaza mashtaka, akasema “Malkia ali- 
pika maandazi, 


Na yalikuwa mazuri bila shaka, 
Akaja mwizi alfajiri sana, 
Na aliyaondoa kwa haraka.” 


Mfalme akamwambia wathenashara “ Fiki- 
rini sana.” Sungura Mweupe akapiga tena ta- 
rumbeta akasema “ Mshahidi wa kwanza si- 
mana.” Mshahidi wa kwanza alikuwa Mwu- 
za Kofia. Akasimama, akakaribia kidogo kiti 
cha enzi, nyuma yake wakaja Kobe na Komba. 
Mwuza Kofia alikuwa akishika kikombe na 
kipanda cha mkate, akawasujudia sana Mfalme 
na Malkia, akasema ““ Niwieni radhi Bibi na 
Bwana, lakini nilikuwa sijaisha chakula cha 
jioni nilipoitwa nanyi.” Mfalme akasema 
“ Shauri hili mbaya; kwa sababu gani hujaisha 
kula? Ulianza kula lini?” Mwuza Kofia 
akamtazama Kobe akasema “ Tulianza kula 
chakula cha jioni terehe 14 Machi.” Kobe 
akasema “La! Terehe 15 Machi.” Komba 
akajibu “La! Ilikuwa 16 Machi.” Mfalme 
akawaambia wathenashara “ Andikeni maneno 
haya.” Viumbe wakaandika zile terehe tatu, 
wahazihesabu wakaandika jumla kana kwamba 
zilikuwa shilingi na senti. 


104 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


Mfalme akamwambia Mwuza Kofia akasema 
“Vua kofia yako.” Mwuza akajibu “Si kofia 
yangu.” Mfalme akapiga uruzi akasema 
“ Umeiiba ?” Akawaambia “ wathenashara 
“ Andikeni.” Mwuza Kofia akaeleza kwa ha- 
raka akasema “ Mimi mchuuzi, dukani mwa- 
ngu ziko kofia nyingi sana, lakini si zangu za 
kuvaa, naziuza tu.” Kwa ghafula Malkia aka- 
vaa miwani, akamtazama sana Mwuza Kofia. 


Huyo, alipoona kuwa Malkia alikuwa akimta.- 
zama alitetemeka kwa hofu. Mfalme akasema 
“ Toa ushahidi, wala usiogope ili nisikukate 
kichwa sasa hivi.” Mwuza Kofia akazidi kute- 
temeka na kubabaika, na katika kufadhaika 
kwake alikimegua kikombe badala ya mkate. 
Wakati ule ule Elisi aliona ajabu mwilini 
mwake, baadaye alifahamu ya kwamba aliku- 
wa akiongeza tena urefu; akawaza kuwa afa- 


MWIZI WA MAANDAZI 105 


dhali atoke Bomani, lakini halafu aliona ni 
heri azidi kukaa, kama ikiwapo nafasi. Ko- 
mba alikuwa amekaa karibu na Elisi akasema 
“ Usinisukume mwanangu, sioni wasaa hata 
wa kuvuta pumzi!” Elisi akajibu kwa unye- 
nyekevu, akasema “Sina budi nikusukume, 
sababu mimi naongezeka urefu.” Komba aka- 
sema "Huna ruksa kuongeza urefu hapa.” . 
Elisi akajibu “ Wewe unaongezeka pia.” Ko- 
mba akaondoka akasema “ Najua sana, lakini 
mimi nakua kwa pole pole, si kama wewe, kwa 
haraka sana.” Komba akamwacha Elisi aka- 
kaa mahali pengine. Komba na Elisi walipo- 
kuwa wakisemezana, Malkia alikuwa anazidi 
kumtazama Mwuza Kofia; akamwambia Askari 
mmoja akasema ““ Niletee karatasi yenye ma- 
jna ya waimbaji wa machezo ya terehe 13 
Machi.” Aliposikia maneno haya Mwuza Ko- 
fia akazidi mno kutetemeka mpaka viatu vyake 
 vikamtoka miguuni; Mfalme akasema “Toa 
ushahidi mara moja.” Mwuza Kofia akajibu 
akasema “ Uwe na rehema, mimi maskini, sina 
akili.” Mfalme akapiga kofi akasema ““ Nenda 
zako. Mjinga.” Mwuza Kofia akajibu “ Nipe 
ruksa kwanza niishe kula chakula cha jioni.” 
Alipokuwa akisema Malkia alikuwa akilitafuta 
jina lake katika majina ya waimbaji. Mfalme 
akasema kwa upole “ Mwuza Kofia we, nenda 
zako.” Malkia akapaza sauti akasema ““ Mka- 
te kichwa huko nje. Huyu ndiye aliye- 


106 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


mwua Nafasi zamani kidogo.” Mwuza Kofia 
hakukaa kuyasikia maneno haya, akaviacha 
viatu Bomani, akakimbia kwa haraka ka- 
ma umeme hata hakuweza kukamatwa na 
Askari. Mfalme akaondoka akasema kwa sauti 
kuu akinena “Mwita mshahidi wa pili.” 
Mshahidi wa pili alikuwa Mpishi wa Mama 
Mkubwa; alikuwa amechukua chupa ya pili 
pili. Mfalme akamwambia “Toa ushahidi 
wako.” Mpishi akajibu “Sitaki.” Sungura 
Mweupe akamwambia Mfalme akasema “ La.- 
zima umshurutishe aseme.” Mfalme akapiga 
chafya akafunga mikono akamtazama sana 
Mpishi akasema “Maandazi yalitengenezwa 
kwa kitu gani?” Mpishi akajibu “ Yalitenge- 
nezwa kwa pili pili.” Komba akaondoka aka.- 
sema kwa sauti nyembamba “ Yalitengenezwa 
kwa asali!” Malkia akanong'ona akasema 
“ Akatwe kichwa yule Komba.” Wote waka.- 
simama wakapiga mbio huko na huko, waka- 
jaribu kumkamata Komba; ilikuwa ghasia ka- 
bisa Bomani, lakini watu walishindwa. Komba 
akapanda darini. Watu wote walikuwa wame- 
choka, wakapumzika, na kumbe Mpishi naye 
alikuwa ametoroka! Mfalme akasema “ Hai- 
dhuru, mwite mshahidi mwingine.” Akamwa- 
mbia Malkia kwa sauti ndogo akasema “' Tafa- 
dhali mpenzi, wewe umwulize mshahidi huyu, 
kichwa kinaniuma.” 

Elisi akamtazama Sungura Mweupe, aliye- 


MWIZI WA MAANDAZI 107 


kuwa akitafuta jina la mshahidi wa tatu katika 
cheti chake. Sungura Mweupe akasimama wi- 
ma, akapiga sana tarumbeta mara tatu, aka- 
sema kwa sauti kuu: 


yi AA AI YA 


TTA 


SURA KZII 


USHAHIDI WA ELISI 


Eusi alishtuka sana kusikia jina lake likita- 

jwa; lakini akasimama mara akaitikia “ Sa!” 

Kwa sababu ya urefu wake mkubwa akaangu- 

sha baraza ya wathenashara. Akafadhaika 

sana akasema “ Niwieni radhi, niwieni ra- 
108 


USHAHIDI WA ELISI 109 


dhi!” Akawasaidia wanyama kutengeneza tena 
meza, na kutafuta vibao vyao na kalamu 
zao. 

Wote walipokuwa tayari Mfalme alimwuliza 
Elisi akasema “ Unajua nini katika mambo 
haya?” Elisi akajibu “ Sijui kitu.” Mfalme 
akawaambia wathenashara akasema “ Andi- 
keni ' Hajui kitu.” ”” Mfalme akamtazama Elisi 
akafadhaika akatoa kitabu kidogo katika mfu- 
ko akasoma, akakirudisha mfukoni, akamta- 
zama tena Elisi akasema “Sikilizeni. Amri 
ya arobaini na nne ya Boma hili ndiyo: “ Wote 
wenye urefu kupita mnazi wafukuzwe Bomani.” 
Wote wakamtazama €Elisi. Kijana akasema 
“ Urefu wangu si wa kupita mnazi.” Mfalme 
akajibu “ Ni kupita minazi miwili.” Elisi aka- 
sema ““Sitaondoka. Hii si amri ya tangu za- 
mani, umeizua sasa hivi katika haja yako ?” 
Mfalme akajibu akasema “Ni amri ya kale 
kupita zote kitabuni.” Elisi akacheka akasema 
“Ikiwa hivyo, basi sharti iwe ya kwanza, 
nawe ulikuwa ukitazama katika ukarasa wa 
mwisho kitabuni.” Mfalme hakujibu, akafa- 
dhaika kabisa, akaondoka katika kiti chake cha 
enzi, akapaza sauti akasema “ Wakubwa wa 
Baraza wakate shauri.” Malkia Mzunguwapili 
akaondoka akamwelekeza kwa kidole Mjanja, 
aliyekuwa mfungwa, akasema ““ Kwanza mkate 
kichwa huyu.” Elisi akasema “ Hapana Ma.- 
ma, Kwanza hukumu, halafu kuuawa, ikiwa 


110 ELISI KATIKA NCHI YA AJABU 


amestahili.” Malkia akanong'ona akasema 
“ Nyamaza we.” Elisi akajibu “Siwezi ku- 


, 
LA 


ZA HY A , j , AL 
Yu IA 
SIRA ZA JUA 


A ZIZINI 


ka 
? 


j , Mi 
MA : 
AA la LI 


nyamaza.” Malkia akasema Kwa sauti kali 
akanena ““ Mkate kichwa Elisi !” 


USHAHIDI WA ELISI 111 


Elisi akawatazama Askari akatabasamu kwa- 
ni hakutokea hata mtu mmoja wa kutimiza 
amri za Malkia. 

Elisi akajitazama, akaona kuwa urefu wake 
ulikuwa kama zamani, kama mtoto wa nchi 
wa Afrika. Akawatazama wenyeji wa Nchi 
wa Ajabu akasema: “ Siwaogope ... 


Ninyi Nyote Karata TU. 
UA WA WA II AA BE 


Kwa maneno haya karata zote zikaruka he- 
wani zikampiga usoni Elisi. 
Yeye akafumbua macho, akapiga yowe. ... 


Alipokuwa macho akajiona, na kumbe aliku- 
wa amelala chini ya mwembe! Dada yake 
alikuwa amekaa karibu akimfukuzia mdudu 
aliyekuwa ametambaa usoni, akasema “ Amka 
Elisi mwanangu, umelala sana.” Elisi akao- 
ndoka akajinyosha akasema “Kweli! Tena 
nimeota sana.” Akamsimulia Dada habari za 
ndoto yake. 

Alipokwisha kuhadithia ndugu yake aka- 
mwambia “Twende mwanangu, Mama ana- 
twanga, chakula cha jioni ni karibu tayari, na 
Dina anakulilia.” 


Mwisho. 


AA j " 


Ka 
v 


Ka ya z. 
KA 


ya 


Fara 


aa 
| Aa 
3 aa 
UA 

ea YA au 


ka Ai 
UA ka 
- aaa wi 


na 


WA 


Na 
ia 
”, Bia aa 

UE Ka, 


Wa 


ra