MWANZO
Kuumba ulimwengu
IKatika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia. ^Na dunia ilikuwa
ukiwa na utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa kilindi; Roho ya Mungu
akatulia juu ya uso wa maji. ^ Mungu akasema: Nuru iwe: na nuru ilikuwa.
^ Mungu akaona nuru ya kama ilikuwa vizuri; Mungu akatenga nuru na giza.
5 Mungu akaita nuru Muchana na giza aliita Usiku. Na ilikuwa mangaribi na
ilikuwa asubui, siku moja.
6 Mungu akasema: Iwe nafasi katikati ya maji, itenge maji na maji. '^ Mungu
akafanya nafasi, akatenga maji yaliyo chini ya nafasi na maji yaliyo juu ya
nafasi; na ilikuwa hivi. ^ Mungu akaita nafasi Mbingu. Na ilikuwa mangaribi,
na ilikuwa asubui, siku ya pili.
9 Mungu akasema: Maji chini ya mbingu yakusanyike kwa pahali pamoja.
na inchi kavu ionekane; na ilikuwa hivi. lo Mungu akaita inchi kavu Inchi,
kusanyiko la maji akaita Bahari. Mungu akaona ya kama ihkuwa vema.
11 Mungu akasema: Inchi itoe majani, mboga ikitoa mbegu, na muti wa
matunda ukizaa matunda ya namna yake, mbegu yake iliyo ndani yake, juu ya
inchi; na ilikuwa hivi. 12 inchi ikatoa majani, mboga ikitoa mbegu ya namna
yake, na muti ukizaa matunda, mbegu yake iliyo ndani yake, ya namna yake.
Mungu akaona ya kama ilikuwa vema. ^^ Na ilikuwa mangaribi, na ihkuwa
asubui, siku ya tatu.
14 Mungu akasema: Iwe miangaza kwa nafasi ya mbingu ipate kutenga kati
ya muchana na usiku; nayo iwe kwa alama na kwa nyakati na kwa siku na kwa
miaka. ^^ Nayo iwe kwa nuru kwa nafasi ya mbingu, iangaze juu ya dunia; na
ihkuwa hivi. i^ Mungu akafanya miangaza miwih mikubwa; mwangaza muku-
bwa kutawala muchana na mwangaza mudogo kutawala usiku; na nyota
vilevile. i^ Mungu akaiweka kwa nafasi ya mbingu kuangaza juu ya dunia,
18 na kutawala juu ya muchana na juu ya usiku, na kutenga nuru na giza; na
Mungu ahona ya kama ilikuwa vema. i^ Na ilikuwa mangaribi na ilikuwa
asubui, siku ya ine.
20 Mungu akasema: Maji yajae kwa wingi na viumbe vilivyo hai, na ndege
waruke juu ya inchi kwa nafasi ya mbingu. 21 Mungu akaumba nyama wakubwa
za bahari, na kila kiumbe kilicho hai na kinachotembea, maji yaliyotoa wingi
kwa namna zao, na kila ndege kwa namna yake. Mungu akaona ya kama
ihkuwa vema. 22 Mungu akawabariki, akisema: Muzidi na kuongezeka, mujaze
maji baharini, na ndege wazidi inchini. 23 Na ilikuwa mangaribi, na ilikuwa
asubui, siku ya tano.
24 Mungu akasema: Inchi itoe kila kiumbe kilicho hai kwa namna yake,
ngombe na mutambazi, na nyama ya inchi kwa namna yake; na ihkuwa hivi.
25 Mungu akafanya nyama ya inchi kwa namna yake, na ngombe kwa namna
1:1 Yn 1:1, 3; Ebr 1:10; Yob 38:4; ha 44:24; Rom 1:20; Kol 1: 16; Ebr 11:3; Ufa 4:11. 1:2
Yer 4:23; Isa 40:12. 1:3 Zab 33:9. 1:5 Zab 74:16. 1:6 Yob 37:18; Zab 33:6; 136:5; Yer
10:12. 1:9 Yob 26:10; 38:8; Zab 33:7; 95:5. 1:11 Ebr 6:7; Lk 6:44. 1:14 Tor 4:19; Yob
25:3,5; Zab74:16; 136:7. l:17Zab8:l. 1:20 Zab 104:24. 1:24 Zab 104:18-23.
6 MWANZO 1, 2
yake, na kila mutambazi juu ya udongo kwa namna yake; Mungu akaona ya
kama ilikuwa vema.
26 Mungu akasema: Tufanye mutu kwa mufano wetu, mwenye sura yetu, na
watawale juu ya samaki za bahari na juu ya ndege za hewa na juu ya ngombe, na
juu ya inchi nzima, na juu ya kila mutambazi anayetambaa juu ya inchi.
27 Mungu akaumba mutu kwa mufano wake mwenyewe, kwa mufano wa Mungu
akamwumba; mume na muke akawaumba. ^^ Mungu akawabariki, Mungu
akawaambia: Muzidi na kuongezeka, na mujaze tena inchi na kuitiisha; na
mutawale juu ya samaki za bahari, na ndege za anga na kila kiumbe kina-
chotambaa inchini.
29 Mungu akasema: Tazameni, nimewapa ninyi kila mboga ikizaa mbegu
iliyo juu ya uso wa inchi, na kila muti ndani yake ni tunda la muti likizaa mbegu;
kwenu utakuwa kwa chakula,^^ na kwa kila nyama ya dunia, na kwa kila ndege
ya anga na kwa kila mutambazi juu ya inchi, uliyo hai; nimewapa majani yote
ya mboga kwa chakula; na iHkuwa hivi. ^^ Na Mungu aUona kila kitu ali-
chofanya, na tazama, kilikuwa kizuri sana. Na ilikuwa mangaribi, na ilikuwa
asubui, siku ya sita.
Edeni
2Mbingu na dunia zikamaUzwa, na jeshi lao lote. 2 Siku ya saba Mungu
akamaliza kazi yake aUyofanya, akastarehe siku ya saba katika kazi yake
yote aliyofanya. ^ Mungu akabariki siku ya saba, akaitakasa; kwa sababu
ndani yake alistarehe katika kazi yake yote Mungu aHyoumba na kuifanya.
4 Hivi ni vizazi vya mbingu na vya dunia wakati zilipoumbwa, kwa siku
BwANA Mungu alipofanya dunia na inchi. ^ Wala haijakuwa bado mbegu ya
shamba duniani, wala mboga ya shamba haijaota bado; kwani Bwana Mungu
hajanyesha bado mvua duniani wala mutu wa kulima udongo hakuwa; ^ lakini
umande ukapanda toka inchi, ukanyesha maji juu ya uso wote wa inchi.
'7 Bwana Mungu akafanya mutu wa mavumbi ya inchi, akapuliza pumuzi ya
uzima ndani ya pua yake; na mutu alikuwa nafsi ya uhai.
8 Bwana Mungu akapanda shamba kwa upande wa mashariki kwa Edeni,
akatia pale mutu aliyemufanya. ^ Toka udongo Bwana akaotesha kila muti wa
kupendeza macho, na muzuri kwa chakula; muti wa uzima vilevile uHkuwa
katikati ya shamba, na muti kujua uzuri na ubaya. ^^ Muto ukatoka katika
Edeni kunyesha maji shambani ; na toka kule ukatengwa na ulikuwa vichwa vine.
11 Jina lake la kwanza ni Pisoni; ndio unaozunguka inchi nzima ya Havila, pale
zahabu ilipokuwa. ^2 Na zahabu ya inchi ile ni nzuri, kule kuna bedola na kitcha-
frangi. ^^ Jina la muto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka inchi nzima ya
Etiopia. ^^ Jina la muto wa tatu ni Hidekeli, ndio unaotembea mbele ya Asuria.
Muto wa ine ni Furati. ^^ Bwana Mungu akatwaa mutu, akamutia shambani
mwa Edeni kuliHma na kulichunga. ^^ Bwana Mungu akaagiza mutu akisema:
Wa kila muti wa shamba unaweza kula; ^"^ lakini wa muti wa kujua uzuri na
ubaya usile kwa maana siku unapokula, hakika utakufa.
1: 26 Zab 100:3; Efe 4:24: Yak 3:9; Zab 8:6. 1:27 1 Kor 11:7; Efe 4:24; Kol 3:10 Mai 2:15; Mt
19:4; Mk 10:6. 1:28 Zab 127:3; 1 Tim 4:3; Mwa 9:1, 7; Law 26:9; Zab 128:3, 4. 1:29 Yob
36:31; Zab 104:14, 15; 136:25; 146:7; Mdo 14:17. 1:30 Zab 145:15, 16; 147:9; Yob 38:41. 1:31
Zab 104:24; 1 Tim 4:4.
2:2 Kut 31:17; Ebr 4:4. 2:3 Kut 16:22-30. 2:5 Zab 104:14; 65:9, 11. 2:8 Mwa 13:10, 2:9
Eze 31 ;8; Mwa 3:22; Ufu 22:2, 14. 2:10 Zab 46:4. 2:11 Mwa 25:18. 2:14 Dan 10:4.
MWANZO 2, 3 7
Hawa
ISBwANA Mungu akasema: Si vema mutu awe peke yake; nitamufanyia
musaidia anayefaa kwake. ^^ Na kwa udongo Bwana Mungu akafanya kila
nyama ya mwitu na kila ndege ya hewa, akawaleta karibu na mutu kuona
atakavyowaita; na sawasawa mutu alivyoita kila kiumbe cha uzima, hili jina
lake. 20 Mutu akawapa majina ngombe zote na ndege za hewa na kila nyama
ya mwitu, lakini musaidia kwa mutu hakuonekana. 21 Na Bwana Mungu
alileta usingizi muzito kuangukia mutu, akalala; akatwaa mumoja wa mifupa
ya mbavu zake, akafunga nyama kwa pahali penyewe; 22 na mufupa wa mbavu
Bwana Mungu alioondosha kwa mutu, akafanya mwanamuke, akamupeleka
karibu na mutu. 23 Adamu akasema: Huyu sasa mufupa wa mifupa yangu, na
nyama ya nyama yangu; ataitwa Mwanamuke kwa maana ameondoshwa katika
mume. 24 Kwa sababu hii mume ataacha baba yake na mama yake na ata-
fungana na muke wake; nao watakuwa mwili mumoja. 25 Nao wawili walikuwa
watupu, mume na muke wake, wala hawakuona haya.
Zambi ya kwanza
3Basi nyoka alikuwa na hila kuliko nyama zote za mwitu Bwana Mungu
aliofanya. Akamwambia mwanamuke: Ndiyo, Mungu amesema: Musile ya
miti yote ya shamba? 2 Mwanamuke akamwambia nyoka: Matunda ya miti ya
shamba tunaweza kula; ^ lakini matunda ya muti ulio katikati ya shamba Mungu
amesema: Musile yake wala musiyaguse, musife. '♦Nyoka akamwambia
mwanamuke: Hakika hamutakufa, ^ kwani Mungu anajua ya kama siku
mutakapokula matunda yake, macho yenu yatafunguliwa, na mutakuwa kama
Mungu mukijua uzuri na ubaya. ^ Na wakati mwanamuke alipoona ya kama
muti ulikuwa muzuri kwa chakula, na ya kama ulipendeza macho, na ya kama
ulikuwa muti wa kutamaaniwa, akatwaa ya matunda yake, akakula; akamupa
mume wake vilevile pamoja naye, naye alikula. ^ Nao wawili, macho yao yali-
funguliwa; wakajua ya kama walikuwa watupu; wakashona majani ya mutini,
wakajifanyia nguo. ^ Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu akitembea
shambani mangaribi; mume na muke wake wakajificha wenyewe mbele ya
macho ya Bwana Mungu katikati ya miti ya shamba. ^ Bwana Mungu akaita
Adamu, akamwambia: Wewe ni wapi? ^^ Akasema: Nimesikia sauti yako
shambani, nikaogopa, kwa sababu nilikuwa mutupu; nikajificha. ^^ Akasema:
Nani aUkuambia ya kama uHkuwa mutupu? Umekula wa muti juu yake nili-
kuagiza: Usile? 12 Mwanamume akasema: Mwanamuke uliyenipa awe pamoja
nami, yeye alinipa ya muti, na nilikula. i^ Bwana Mungu akamwambia mwana-
muke: Nini hii uliyofanya? Mwanamuke akasema: Nyoka alinidanganya, na
nilikula. i^ Bwana Mungu akamwambia nyoka: Kwa sababu umefanya maneno
haya, umelaaniwa kuliko nyama zote, na kuliko kila nyama ya mwitu; juu ya
tumbo lako utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; ^^ na
nitatia uadui katikati yako na mwanamuke, na katikati ya uzao wako na uzao
wake; ataponda kichwa chako, na wewe utaponda kisigino chake. 1^ Akamwa-
2:19 Zab 8:6. 2:21 Mwa 15: 12. 2:22 Mez 18:22; Ebr 13:4. 2:23 Mwa 29:14; Amu 9:2; 2 Sam
5:1; Efe 5:30; 1 Korll:8. 2:24 Zab 45:10; Mt 19:5; Mk 10: 7; 1 Kor 6:16; Efe 5:28-31. 2:25
Kut 32:25; Isa 47:3.
3:1 Mt 10:16; Ufa 12:2; 20:2. 3:3 Mwa 2: 16, 17. 3:4 2 Kor 11:3; 1 Tim 2: 14. 3:6 Rom 5:12-
19. 3:8 Yob 31:33; 38:1; Zab 139:l-12;Yer23:34;Amo9:3. 3:9Mwa4:9. 3:10Yob 23:15;
1 Yn 3:20. 3:12 Mez 28:13; Yak 1:13. 3:14 Isa 65:25; Mik 7:17. 3:15 Hes 21:6, 7; Rom 16:20;
Ebr 2:14; 1 Yn 3:8. 3:16 Yn 16:21; 1 Tim 2:15.
8 MWANZO 3
mbia mwanamuke : Nitazidisha sana uchungu wako na kuzaa kwako; kwa
uchungu utazaa watoto; kutaka kwako kutakuwa kwa mume wako, naye
atakutawala. ^^ Akamwambia Adamu: Kwa sababu umesikia sauti ya mwana-
muke wako, na umekula ya muti, juu yake niiikuagiza nikisema: Usile matunda
yake; udongo umelaaniwa kwa sababu yako; kwa uchungu utakula ya matunda
yake siku zote za maisha yako; ^^ michongoma na miiba utakuotesha; na
utakula majani ya shamba; i^kwa jasho ya uso wako utakula mukate, hata
utakaporudi kwa udongo; kwa maana umetwaliwa katikati yake; kwa sababu
mavumbi wewe, na utarudi kwa mavumbi. 20 Mwanamume akaita jina la muke
wake Hawa; kwa sababu alikuwa mama ya wote walio hai. 21 Bwana Mungu
akafanyia Adamu na muke wake mavazi ya ngozi, akawavalisha.
Adamu na Hawa wanafukuzwa toka Edeni
22 Bwana Mungu akasema: Tazama, mutu amekuwa kama mumoja wetu,
kwa kujua uzuri na ubaya; na sasa, isiwe anyoshe mukono wake na kutwaa
vile wa muti wa uzima, na kula, na kuishi milele; ^3 kwa hivi Bwana Mungu
akamutoa toka shamba la Edeni, ahme udongo pale alipotwaHwa. 24 Hivi
akafukuza mutu, akaweka Makerubi kwa mashariki ya shamba la Edeni na
upanga wa uUmi wa moto uliogeuka pande zote kuchunga njia ya muti wa uzima.
La Sainte Bible en swahili du Zaire
© Societe Biblique du Zaire
United Bible Societies
Africa Regional Centre
P O Box 42726
Nairobi, Kenya
UBS-EPF 1993-25M-R062 ISBN 9966 843 59